Tunapokaribia uchaguzi wa 2020 hakuna ubishi kuwa ndani ya CCM kuna makundi, kwa elewa wangu kuna kundi la Bernard Membe aliyekuwa mgombea 2015 vile vile bado kuna masalia ya kundi la Lowassa. Ingawa Magufuli naye anajitahidi kutengeneza kundi lake lkn bado changa halina nguvu ya kisiasa nguvu yake inategemea vyombo vya dola.
Wasioamini siasa za fitina ndani ya CCM hasa uchaguzi unapokaribia wamuulize, Salim Ahmed Salim, John Malecela, Mohamed Bilali, na Jakaya Kikwete.
Baada ya jina la Membe kuanza kusikika kuwania urais tayari fitina zimeanza kutengenezwa na mitandao imeanza kujengwa, hofu kubwa ya CCM ni ndani ya chama kuliko nje ya chama, inawezekana kabisa kwa mara ya kwanza rais Magufuli akapata mpinzani.
Rais Magufuli anajua jinsi alivyopita kwenye tundu la sindano kwenye mchakato wa kura ya maoni, anajua fika nguvu ya Lowassa aliyokutana nayo, bila fitina za Mkapa nafikiri leo asingekuwa pale, ndiyo maana anafanya kila awezalo kumuweka Lowassa karibu na himaya yake, anajua Lowassa ni kiungo muhimu kati yake na wanamtandao, ni muda tu tutaanza kuona vijana wa CCM mitandaoni na kwenye majukwaa wakimsafisha Lowassa.
Kwa upande mwingine mtandao wa Membe ni mpana, ukimtaja Membe umemtaja rais msataafu Jakaya Kikwete umemtaja Pius Msekwa, umemtaja Hawa Ghasia, umemtaja Kinana, Nape, Rostam Azizi. Ana marafiki wengi ndani na nje ya nchi, anao marafiki Falme za Kiarabu, Mabalozi wengi wa western countries ni washirika wake.
Membe siyo Lowassa kuwa ukimfanyia figisu kidogo tu atakubali yaishe. Kosa alilofanya Lowassa ambalo sidhani kama Membe atalifanya ni kuhama chama, najua Membe atapambana ndani ya chama kwa kutumia uzoefu wake, ujuzi wake, na diplomasia yake.
Membe ni mwana usalama aliyefanya kazi ya intelijensia ndani ya system kwa muda mrefu na amepanda sana vyeo ndani ya idara hiyo nyeti na hivyo anazijua siri nyingi za serikali na namna nzuri ya kufanya umafia.
Tukumbuke tu kuwa aliyemfix Lowassa hadi kuamua kuondoka CCM ni komred Membe na mtandao wake wa akina Kinana, Nape, kwa hiyo CCM ya akina Bashiru Ally ijiandae kisaikolojia, isidhani itapata mtelemko itakapokuwa ina dili na mbobezi wa fitina Mh. Bernard Membe.