Kama mnavyofahamu Mh.Bashe anedhalilishwa sana jana mjini Dodoma katika vikao vya CCM akituhumiwa kupinga mabadiliko ya Katiba ya CCM. Mh.Bashe aliwekwa ndani kwa amri ya ngazi za juu. Habari zilizoenea zinasema kwamba kosa ilikuwa kupinga mabadiliko ya katiba ya CCM. Hakuna taarifa tofauti zilizotolewa
Mh.Bashe amedhalilishwa kwa kutumia hali yake kikatiba na kidemokrasia lakini ajabu ameonekana sio mwenzao. Ni wengi wanaopinga mabadiliko haya isipokuwa uchumia tumbo na kuwekewa vikwazo ndio kinachowafunga midomo
Kwa tunaojua misimamo ya Bashe hili sio jambo la ajabu. Bashe ana akili za ki Chadema Chadema hivyo anatakiwa kwenda kwenye kundi la ndege anaofanana nao
Bashe amekuwa hivyo ndani na nje ya bunge. Bashe ametishiwa kufukuzwa kwa kosa la kusimamia demokrasia na Chadema ni chama cha Kidemokesia-Chama cha Demokrasia na Maendeleo
Kwa niaba ya makamanda ninasema Bashe CCM sio mahali pako,usisubiri uvuliwe uanachama,jiuzuru na ujiunge na makamanda wenzao wa Chama cha Demokrasia.Muulize Mh.Esta Bulaya utamu wa Chadema
Hata huko CHADEMA hakuna Demokrasia kama unavyowanasibu.
Chama kimebadilika si kama kilivyokuwa awali.
Bila pesa hupati nafasi ya kuwawakilisha wananchi, waliokijenga chama kwa muda mrefu wanaachwa kwenye Chaguzi kwa njia za kibabe mathalani Bashe akifukuzwa CCM akaja CDM atapewa nafasi ya kugombea na kumsahau mpinzani aliyekuwepo Uchaguzi uliopita (CCM hawafanyi hayo). Yuko wapi Lembeli? Kawakosesha CDM Jimbo!
Kuna Wabunge walijulikana hawapiti baada ya kushinda chaguzi zilizopita (2010). Je, kulikuwa na Uchaguzi wa ndani kupitisha Wagombea? Hakuna zaidi ya kauli ya Mwenyekiti tu, hawa waacheni waendelee basi.
Mpeperusha Bendera ya Chama kwenye Urais je? Yaleyale, kupiga kura kwa kusimama kikanda pale Mwanza (Seriously!)
Mwisho nimalizie kwa Ushauri.
1. CDM ibadilike kwa kutendea Hali nafasi walizopata, tusiende mbali sana, Serikali za Mtaa. Kugonga mhuri tu unalipia kama ilivyokuwa awali chini ya CCM, Migogoro ya ardhi kutopungua na huduma zingine za kijamii.
2. CDM ijisafishe na skendo ya Ukabila na ukanda
3. Msingi wa kupata Wagombea iwe Demokrasia kweli, maana wanaopiga kura chamani ndiyo wapiga kura kwenye jamii pia wapiga kampeni.
4. Kupokea wanachama toka CCM sawa lakini wasipewe nafasi za juu. Hapa nikazie kidogo, hivi ukiambiwa leo Lowasa kuwa CDM ni mpango wa CCM kuwadhoofisha utakubali?
Tufanye siyo kweli, jiulize tena CCM inashindwa nini kumuandaa MTU atakayekuwa machachali kwa kuwapinga kisha akahama ili kuja kuwadhoofisha bila ninyi kujua (kuvujisha mbinu zenu kwa Wapinzani)?