BASATA Kuanza Kuhariri Nyimbo za Wasanii Bongo.

Chaliifrancisco

JF-Expert Member
Jan 17, 2015
23,517
70,333
Kuanzia tarehe 1 Mei 2021 BASATA wanaanza kutumia rasmi kanuni ya kuzipitia/kuchuja nyimbo mpya za Wasanii wote Tanzania kabla ya kupelekwa kwenye vituo vya Radio/TV

“hii sio sheria mpya, ilikuwepo kabla ila haikua imeanza kutekelezwa, wimbo ukipitishwa Msanii anapewa cheti”

Chanzo: MillardAyo

My take: Wasanii walijisahau sana kwa kutunga lyrics zisizokuwa na maadili na kusababisha mmomonyoko wa maadili nchini.

Nyimbo nyingi za kizazi kipya hazisikiliziki asilani kwa watu wenye kujielewa.
 
Kwahiyo kuanzia sasa BASATA wapo tayari kubeba lawama endapo kazi mbovu na tungo zisizo na maadili zitasikika?
Maana watakuwa wamehariri na kutoa go ahead.
 
Kuanzia tarehe 1 Mei 2021 BASATA wanaanza kutumia rasmi kanuni ya kuzipitia/kuchuja nyimbo mpya za Wasanii wote Tanzania kabla ya kupelekwa kwenye vituo vya Radio/TV

“hii sio sheria mpya, ilikuwepo kabla ila haikua imeanza kutekelezwa, wimbo ukipitishwa Msanii anapewa cheti”

Chanzo: MillardAyo

My take: Wasanii walijisahau sana kwa kutunga lyrics zisizokuwa na maadili na kusababisha mmomonyoko wa maadili nchini.

Nyimbo nyingi za kizazi kipya hazisikiliziki asilani kwa watu wenye kujielewa.
Safi sana, Pia wamulike na kwenye videos huko kuna watu wanacheza na vichupi vyenye kamba, tena kamba nyembamba
 
Safi Sana

Kweli aisee maaana nyimbo za siku hizi ziko offensive sana kuna wakati ukisikia mtoto anaimba mpaka unapata aibu ukimkataza anakuuliza kwann nisiimbe, wanaleta changamoto kwenye malezi pia na zile video zao za nudity wanaharibu upcoming generations
 
Yan hapo ni sawa na kukinga maji kwenye tenga..watazuia video ya bongo itarushwa nyimbo ya mambele ambayo ndo iko hovyo zaid!
 
Back
Top Bottom