KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,189
- 17,157
CHADEMA leo hii ipo, kwa sababu waliweza kuepuka mitego yote waliyowekewa ili wamalizwe moja kwa moja kama chama endapo wangetumia papara.Chairman, mmeonewa kiasi cha kutosha, mmenyanyaswa kiasi cha kutoshao sasa fanya jambo, tumechoka
Hatari hiyo haijaisha, ipo inaendelea sana hadi leo, kwa hiyo ni kazi kubwa wanayotakiwa CHADEMA kuendelea kuifanya kuepukana na mitego hiyo.
Nashukuru sana kwamba mada yako umejaribu sana kuepuka kuwachochea CHADEMA wafanye mambo yatakayosababisha chama kisambaratishwe kabisa.
Lakini pia, kumbuka bila uwepo wa viongozi kadhaa ndani ya chama hicho, hasa Mbowe mwenyewe, na wengine wachache, hawa wakizuiliwa, shughuli za chama ndipo zitakuwa zimefifia sana. Kwa hiyo, pamoja na kufanya kila linalowezekana katika kukataa uonevu huu wanaofanyiwa CHADEMA, ili CHADEMA iendelee kuwa kiongozi wa mageuzi, viongozi wake ni lazima wawe ni sehemu muhimu wa kuchochea mapinduzi hayo.
Ndiyo, ni kweli, Mbowe na baadhi ya viongozi wa juu wakiondolewa na kuwekwa ndani, dunia italichukulia tendo hilo kwa uzito wake na Tanzania haitakuwa tena nchi isiyokuwa na wafungwa wa kisiasa. Lakini kuondoka kwao katika uwanja wa mapambano kutakuwa kumefifisha sana mapambano hayo bila ya uwepo wa kuibuka kwa viongozi watakaochukua nafasi za kuendeleza mampambano hayo.
Naunga mkono hoja zako zote, niliyoandika hapa ni kutoa tahadhari tu ili ifahamike kwamba mapambano hayatafana bila kuwepo kwa viongozi wa kuyasimamia mapambano hayo.
Ningependa kuona viongozi wengi ndani ya chama hicho, na hasa vijana ambao wapo tayari kuchukua nafasi zao katika kuendeleza mapambano hata bila uwepo wa viongozi waliopo sasa.