Barua ya wazi kwa Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe: CHADEMA Isikubali kuonewa

Chairman, mmeonewa kiasi cha kutosha, mmenyanyaswa kiasi cha kutoshao sasa fanya jambo, tumechoka
CHADEMA leo hii ipo, kwa sababu waliweza kuepuka mitego yote waliyowekewa ili wamalizwe moja kwa moja kama chama endapo wangetumia papara.
Hatari hiyo haijaisha, ipo inaendelea sana hadi leo, kwa hiyo ni kazi kubwa wanayotakiwa CHADEMA kuendelea kuifanya kuepukana na mitego hiyo.

Nashukuru sana kwamba mada yako umejaribu sana kuepuka kuwachochea CHADEMA wafanye mambo yatakayosababisha chama kisambaratishwe kabisa.

Lakini pia, kumbuka bila uwepo wa viongozi kadhaa ndani ya chama hicho, hasa Mbowe mwenyewe, na wengine wachache, hawa wakizuiliwa, shughuli za chama ndipo zitakuwa zimefifia sana. Kwa hiyo, pamoja na kufanya kila linalowezekana katika kukataa uonevu huu wanaofanyiwa CHADEMA, ili CHADEMA iendelee kuwa kiongozi wa mageuzi, viongozi wake ni lazima wawe ni sehemu muhimu wa kuchochea mapinduzi hayo.

Ndiyo, ni kweli, Mbowe na baadhi ya viongozi wa juu wakiondolewa na kuwekwa ndani, dunia italichukulia tendo hilo kwa uzito wake na Tanzania haitakuwa tena nchi isiyokuwa na wafungwa wa kisiasa. Lakini kuondoka kwao katika uwanja wa mapambano kutakuwa kumefifisha sana mapambano hayo bila ya uwepo wa kuibuka kwa viongozi watakaochukua nafasi za kuendeleza mampambano hayo.

Naunga mkono hoja zako zote, niliyoandika hapa ni kutoa tahadhari tu ili ifahamike kwamba mapambano hayatafana bila kuwepo kwa viongozi wa kuyasimamia mapambano hayo.
Ningependa kuona viongozi wengi ndani ya chama hicho, na hasa vijana ambao wapo tayari kuchukua nafasi zao katika kuendeleza mapambano hata bila uwepo wa viongozi waliopo sasa.
 
CCM inahodhi makundi hayo kwa sababu ni chama dola, hiyo ni teknic yao ya survival

Pamoja na yote hayo tusisahau kitu kimoja

INVISIBLE HAND

CCM wamejenga kiburi kuwa hakuna wa kuwagusa, kwamba nyumba yao ya mamlaka ni imara isiyotikisika na kwa kufanya hivyo wamekuwa na kiburi ndiyo maana walivuruga uchaguzi serikali za mitaa na uchaguzi mkuu.

Kwa Kiburi chao hiki wanaweza kujikuta wanakosa Kibali cha Muumba Mbingu na nchi, kwa hiyo tusiwabeze wapinzani kama watakuwa na nia njema na kupigania haki, wanahitaji kuwa consistent
Unapoweka mambo ya Muumba nadhani hata wapinzani siyo watakatifu.

Hasa linapokuja suala la fursa, na maslahi wanasiasa wote lao ni moja.

Hakuna mwanasiasa anaepambania HAKI out of nowhere, isiyo na attachment yoyote yenye maslahi yake.

Sasa hivi ukiwasikiliza wapinzani wote waliokuwa wabunge, ni kama bado wana hangover ya ubunge maana ni pesa za bure bure.

Mimi naamini watu wabaya wako vyama vyote na watu wema wako vyama vyote.

Mfano: Nyalandu aliyekuwa CCM ni binadamu mwenye utu kuliko Selasini au Mwita Waitara waliokuwa CDM.

Kitu kingine kinachoweza kusababisha CCM ipoteze uungwaji mkono mkubwa wa kutisha ni Rais kukatalia madarakani.

Ila kama wataendelea kuwa na 10 years limit, ni ngumu kuwatoa. Maana kisaikolojia binadamu ni mtu wa matumaini, ukiona watu wanaandamana kwa fujo maana yake wamekosa matumaini kabisa.
 
Mimi nadhani ushauri muhimu katika mada nzima iliyowasilishwa hapa ni kwamba, sasa ni lazima yawepo mabadiliko katika mbinu za upambanaji.
Kule kuendelea kuombaomba kumeshindikana, wanaoombwa hawana nia yoyote ya kuwepo kwa mabadiliko.
CHADEMA hawana jeshi la kupambana kivita na wenye silaha zote za wananchi wa Tanzania, ila wana watu ambao, kama wamedhamiria pawepo mabadiliko, hakuna silaha na jela zitakazozuia hilo lisitokee.

Akina Mbowe hawawwezi kwenda kupigwa risasi na kufia mbali kwa kuhimiza watu wakatae hadaa za watawala. Kwa kufanya hivyo watawekwa kizuizini, na kama wapo akina mbowe elfu hamsini, hawa wote watawekwa kizuizini? Hili ndilo litakalokuwa suluhisho la tatizo lililopo?

Kwa hiyo, kazi ya akina Mbowe sasa hivi ni kuhakikisha tu kwamba wapo akina Mbowe wengi watakaochukua nafasi zao wao watakapoondolewa na kuwekwa kizuizini.
 
Yaani wakiaandaa mkutano waandae kila kata nchi nzima tuone kama police wataweza kuwakamata kata zote Tanzania
Issue ni kwamba Police huwa wanayacontrol maandamano na kuyazima kabla hayajatokea kwa kupita mitaani na magari ya kutisha na gwaride plus mazoezi.

Siku ya maandamano hakuna anayetokeza.

Kwanza huyo anaye-organize mwenyewe atakamatwa hata siku ya maandamano haijafika.
 
Unapoweka mambo ya Muumba nadhani hata wapinzani siyo watakatifu.

Hasa linapokuja suala la fursa, na maslahi wanasiasa wote lao ni moja.

Hakuna mwanasiasa anaepambania HAKI out of nowhere, isiyo na attachment yoyote yenye maslahi yake.

Sasa hivi ukiwasikiliza wapinzani wote waliokuwa wabunge, ni kama bado wana hangover ya ubunge maana ni pesa za bure bure.

Mimi naamini watu wabaya wako vyama vyote na watu wema wako vyama vyote.

Mfano: Nyalandu ni binadamu mwenye utu kuliko Selasini au Mwita Waitara waliokuwa CDM.

Kitu kingine kinachoweza kusababisha CCM ipoteze uungwaji mkono mkubwa wa kutisha ni Rais kukatalia madarakani.

Ila kama wataendelea kuwa na 10 years limit, ni ngumu kuwatoa. Maana kisaikolojia binadamu ni mtu wa matumaini, ukiona watu wanaandamana kwa fujo maana yake wamekosa matumaini kabisa.
Muumba namuweka kwa ajili ya wananchi siyo wanasiasa, wanasiasa ni vyombo tu

Upande unaosimamia haki kwa dhati pamoja na mapungufu yake Mungu huuinua!
 
Unapoweka mambo ya Muumba nadhani hata wapinzani siyo watakatifu.

Hasa linapokuja suala la fursa, na maslahi wanasiasa wote lao ni moja.

Hakuna mwanasiasa anaepambania HAKI out of nowhere, isiyo na attachment yoyote yenye maslahi yake.

Sasa hivi ukiwasikiliza wapinzani wote waliokuwa wabunge, ni kama bado wana hangover ya ubunge maana ni pesa za bure bure.

Mimi naamini watu wabaya wako vyama vyote na watu wema wako vyama vyote.

Mfano: Nyalandu ni binadamu mwenye utu kuliko Selasini au Mwita Waitara waliokuwa CDM.

Kitu kingine kinachoweza kusababisha CCM ipoteze uungwaji mkono mkubwa wa kutisha ni Rais kukatalia madarakani.

Ila kama wataendelea kuwa na 10 years limit, ni ngumu kuwatoa. Maana kisaikolojia binadamu ni mtu wa matumaini, ukiona watu wanaandamana kwa fujo maana yake wamekosa matumaini kabisa.
Mkuu, sasa hivi kilicho wazi na kinachoonekana ni ubaya wanaofanya CCM, huo wa CHADEMA, pamoja na kwamba unaweza kuwepo ubaya kwao pia, hayo ni makisio yako tu?
Kama na wao au wengine wakipewa fursa ya kuongoza, wakifanya ubaya tutauona na itakuwa haki yetu kuukataa kama tunavyokataa huu sasa wanaofanya CCM.

Hatuwezi kuogopa kuwasema CCM ambao ubaya wao uko wazi, eti kwa kuogopa ubaya ambao CHADEMA hatujaona wakiufanya.
 
Issue ni kwamba Police huwa wanayacontrol maandamano na kuyazima kabla hayajatokea kwa kupita mitaani na magari ya kutisha na gwaride plus mazoezi.

Siku ya maandamano hakunana anayetokeza.

Kwanza huyo anaye-organize mwenyewe atakamatwa hata siku ya maandamano haijafika.
Hii ni Challenge kubwa ambayo wapinzani huwa wanakutana nayo!.

Njia ya kuvunja hii, ni maandamano ambayo ni incremental kwanza kabla ya kujenga momentum ya maandamano makubwa siku za baadae
Yaani watu waandamane sporadically katika makundi ya watu wachache wachache nchi nzima ili kuvunja hiyo myth kuwa watu huwa hawaandamani.

Kwa mfano show za Polisi hufanywa mijini, lakini pembezoni mwa miji na vijiji huwa hawafiki. Sasa maandamano ya Makundi ya watu yanaweza kufanywa huko pembezoni mwa miji na vijiji kama initial phase ya maandalizi ya maandamano makubwa.
Huko vijijini watu waandamane waende ofisi za serikali za vijiji, watendaji, etc
Baadae hiyo myth ikiwa shattered , itazidi kujenga awareness kwa raia wengi na baadae oneday umma utaingia mtaani tu!
 
Nimeanza kuogopa huenda Mbowe ni mamluki, kuna fursa nyingi kisiasa zinajitokeza lakini hazitumiwibipasavyo.
1. Tozo
2. Kukamatwa kwa wafuasi
3. Kuboronga kwa watawala kwa kutotii katiba hizi zote ni fursa kwa wapinzani kupata pa kuwaunganisha wananchi kupaza sauti kwa pamoja.
Mbowe ni mpinzani kweli au tunazugwa????
 
Unajua kipindi cha kudanganyana kimepita wanasiasa wote wanatafuta kula wao na familia zao ikibidi kusaza hakuna mtu asiye jua, mimi nampongeza Mbowe kwa kuwa muelewa wa mambo ya pesa, Unatoa ushauri mleta mada kama raia wa kawaida huko juu hari haiko hivyo.
Mboe anajua anachokifanya amekuwepo Ikulu tangia anamiaka 13 anasoma, anamsingi mkubwa na taifa hili muwe mnatafuta historia za watu kabla ya kuwaamini azawaizi anles mtakuwa mnapiga mak taimu.
 
Matukio ya ukaidi na kuto kutii sheria na utaratibu kwa maksudi yanayo fanywa na Chadema ni jambo baya sana kwa mustakbali wa vyama vya upinzani vyote.

vyama vingine vya upinzani ni lazima vikemee vikali tabia za kihuni na zenye nia ya kuvuruga amani ya nchi yetu kwani tabia hiyo inayo fanywa na Chadema inachafua taswira ya vyama vingine vya upinzani ambavyo vinaendesha siasa zao kistaarabu.

Mbowe amesikika mara kadhaa akichochea maandamano yasiyo halali, n.k nadhani ni wakati sasa kwa Msajili wa vyama Kukifuta hiki chama cha Chadema kwa maslahi ya Amani ya nchi yetu.

Amani ya nchi yetu ni muhimu zaidi kuliko Chadema.
Peleka akili zako za kuku kulee
 
Muumba namuweka kwa ajili ya wananchi siyo wanasiasa, wanasiasa ni vyombo tu

Upande unaosimamia haki kwa dhati pamoja na mapungufu yake Mungu huuinua!
Wananchi hawajahitaji mabadiliko. Wakiyahitaji yatakuja ndani ya wiki moja tu. Labda huwajui wananchi.

Na tatizo kubwa agenda za wapinzani hazina attachment kubwa na wananchi.

Fanya mikutano ya hadhara nzima uwasikilize wananchi, agenda zao ni tofauti kabisa.

Wengi watasema Afya, maji, elimu, ardhi, mafao, bei za mazao n.k.

Watu kama hao kuwaambia waandamane kwasababu ya katiba mpya siyo rahisi.

Mwananchi ambaye anaamka asubuhi anenda shambani, ziwani kuvua au kuchunga ng'ombe hawezi kuona ni kwa namna gani katiba mpya itamsaidia kwenye shughuli zake.

Kundi pekee litakalokwambia linataka Katiba mpya ni tabaka la kisiasa.
 
Mkuu, sasa hivi kilicho wazi na kinachoonekana ni ubaya wanaofanya CCM, huo wa CHADEMA, pamoja na kwamba unaweza kuwepo ubaya kwao pia, hayo ni makisio yako tu?
Kama na wao au wengine wakipewa fursa ya kuongoza, wakifanya ubaya tutauona na itakuwa haki yetu kuukataa kama tunavyokataa huu sasa wanaofanya CCM.

Hatuwezi kuogopa kuwasema CCM ambao ubaya wao uko wazi, eti kwa kuogopa ubaya ambao CHADEMA hatujaona wakiufanya.
Anyway, mimi sioni chochote wanachofanya CCM ambacho CDM hawajakifanya. Hasa kwenye eneo la Nepotism, Siasa chafu, ubaguzi, chuki, Impunity na Demokrasia.

Mwisho wa siku vitabadilika vyama, ila watu ni wale wale tu.

Uhuru Kenyatta wa KANU ndio huyo huyo wa Jubilee.

Hata Lowassa wa CCM ndio huyo huyo wa CHADEMA.
 
Wananchi hawajahitaji mabadiliko. Wakiyahitaji yatakuja ndani ya wiki moja tu. Labda huwajui wananchi.

Na tatizo kubwa agenda za wapinzani hazina attachment kubwa na wananchi.

Fanya mikutano ya hadhara nzima uwasikilize wananchi, agenda zao ni tofauti kabisa.

Wengi watasema Afya, maji, elimu, ardhi, mafao, bei za mazao n.k.

Watu kama hao kuwaambia waandamane kwasababu ya katiba mpya siyo rahisi.

Mwananchi ambaye anaamka asubuhi anenda shambani, ziwani kuvua au kuchunga ng'ombe hawezi kuona ni kwa namna gani katiba mpya itamsaidia kwenye shughuli zake.

Kundi pekee litakalokwambia linataka Katiba mpya ni tabaka la kisiasa.
EeenHeeee!,
Utaniwia radhi kama itaonekana ninakufuatilia kila sehemu, lakini naona mabandiko yako yana mvuto nisioweza kujizuia kuujibu.

Yaani mkuu, unasubili, au unayo matumaini ya wachuga ng'ombe/mbuzi/wavuvi, n.k., WOTE wafikie hatua ya kuingia barabarani ndipo waweze kushiriki kuleta mabadiliko?

Hali ya namna hiyo uliwahi kuiona wapi duniani?

Ninakuhakikishia, nchi hii wakipatikana watu laki tano, waliodhamiria kabisa kuleta mabadiliko, utayaona mabadiliko, na hao wengine watakuwa ni washiriki wakubwa kwenye hatua za kumalizia mapambano hayo.
Usitegemee wote hao uwaone leo barabarani, au kutowaona barabarani ukadhani kwamba hawataki mabadiliko.
 
Hii ni Challenge kubwa ambayo wapinzani huwa wanakutana nayo!.

Njia ya kuvunja hii, ni maandamano ambayo ni incremental kwanza kabla ya kujenga momentum ya maandamano makubwa siku za baadae
Yaani watu waandamane sporadically katika makundi ya watu wachache wachache nchi nzima ili kuvunja hiyo myth kuwa watu huwa hawaandamani.

Kwa mfano show za Polisi hufanywa mijini, lakini pembezoni mwa miji na vijiji huwa hawafiki. Sasa maandamano ya Makundi ya watu yanaweza kufanywa huko pembezoni mwa miji na vijiji kama initial phase ya maandalizi ya maandamano makubwa.
Huko vijijini watu waandamane waende ofisi za serikali za vijiji, watendaji, etc
Baadae hiyo myth ikiwa shattered , itazidi kujenga awareness kwa raia wengi na baadae oneday umma utaingia mtaani tu!
Vijijini watu wana maisha yao mengine kabisa.

Ni ngumu kwa mtu kuacha shughuli zake za kuchunga mifugo, kulima au palizi akaandamane kudai katiba mpya.

Unless kama utamwambia hiyo katiba itamsaidiaje kulinda mifugo yake na ardhi.

Ishtoshe vijijini kuna tawala tofauti na za kimila au Yowe zinazoheshimika sana, ambazo sidhani kama Chadema wana ushawishi huko.
 
Anyway, mimi sioni chochote wanachofanya CCM ambacho CDM hawajakifanya. Hasa kwenye eneo la Nepotism, Siasa chafu, ubaguzi, chuki, Impunity na Demokrasia.

Mwisho wa siku vitabadilika vyama, ila watu ni wale wale tu.

Uhuru Kenyatta wa KANU ndio huyo huyo wa Jubilee.

Hata Lowassa wa CCM ndio huyo huyo wa CHADEMA.
Mimi sijawaona CHADEMA waking'ang'ania kubaki madarakani, na hata kukataa kabisa kuboresha katiba ili kura za wananchi ziweze kuwa na nguvu ya kuwabakisha madarakani au kuwaondoa.

Katika mambo yote, pengine hili kwangu ni la muhimu zaidi.
 
Wote CCM hao... Uchaguzi wa 2020 ni fundisho kubwa kwa upinzani. They should be ready for a bigger sacrifice. Amani itapatikana kwa ncha ya upanga tu. Vinginevyo, watakuwa ni kama NGO ya mambo ya siasa hadi mwisho wa dunia. The timing is right. Inategemea na jinsi watavyocheza karata zao.
Hata mimi nashangaa, kuna watu Wanataka Chadema itii tu amri ambazo siyo za haki.

Chadema wakiikubali hii hali maana yake ni kuwa kamwe hakitopata fursa ya kuwafikia wwnanchi ipasavyo na kutafuta kuungwa mkono.

CCM wanataka kuilimit Chadema isikue
 
Ndugu Freeman!
Mara nyingi umesikika ukitaka sana siasa za uungwana, siasa za akupigaye shavu la kushoto basi mgeuzie la kulia. Hilo ni jambo zuri lakini hiyo falsafa yako inafanya kazi katika nchi za watawala ambao ni sober minded, siyo katika nchi ambayo watawala wameamua liwalo na liwe kwenye kusimika mifumo ya dhulma, uonevu ukandamizaji na kufanya lolote ilimradi waendelee kubaki madarakani hata kama si kwa ridhaa za wananchi.

Ndugu Mbowe
Tone yako ya kupenda maridhiano watawala wanaitafsiri kama uoga.

Huu uonevu mnaofanyiwa na watawala wa kunyimwa haki zenu za kufanya siasa kinyume cha katiba mtaendelea kufanyiwa mpaka siku mtakapoamua kusema sasa inatosha!

Ndugu Mbowe, Huu ni muda sasa wa kuvunja confidence hii ya watawala ambayo kimsingi wameshajiaminisha kuwa hamna uwezo, wala guts za kufanya chochote. Hii chain mkiifanikiwa kuivunja mtakuwa katika position nzuri za kuadvance haki zenu za kisiasa nchini.

Huu ni muda muafaka wa kuraise stake katika utawala wa nchi hii ili waone kuwa kutawala kinyume cha sheria na katiba ni kitu chenye gharama, kwa hiyo lazima ufanye yafuatayo:

1. Ni muda muafaka sasa wewe kuhimiza Wafuasi wako wasitii maagizo batili
Toa maagizo yako kwenye machinery nzima ya chama chako, Viongozi na wanachama wa chama chako wasitii maagizo haramu ya watawala katika maeneo yao. Kwa mfano kama Wamezuia mikutano, wewe waagize wafanye mikutano. Wewe usijali wala kuhofu maagizo yako yatafanyiwa kazi kwa kiwango gani, lakini wewe toa agizo la kichama, vikao na mikutano ifanyike. Katika hili kuna watakaofanikiwa kufanya hiyo mikutano kuna watakaoshindwa kwa sababu mbalimbali, lakini ni lazima tuvunje hii chain ya utii haramu wa maagizo haramu yaliyo kinyume cha sheria

2. Ni lazima CHADEMA iendelee kuwin huruma ya wananchi
Haya matendo mnayofanyiwa ya uonevu na ukandamizaji, wananchi wanayaona. Sasa ni muda muafaka wa kuyadocument vizuri, kuyaamplify ili wananchi wengi wayaone. Uonevu ambao watawala wanawafanyia kama mtaweza kuwashitakia, uungwaji mkono utakuwa ni mkubwa, na utaendekea kukua siku baada ya siku

3. Ndugu Mbowe ni muda wa Uongozi wa CHADEMA kusacrifice zaidi
Ndugu Mbowe, kama nilivyokueleza huko juu, kuna ulazima wa kuvunja chain hii ya uonevu, hili halitifanyika bila uongozi wa CHADEMA kujitoa mhanga(kusacrifice), Ni lazima uongozi wa CHADEMA uitishe mikutano ya wazi ambayo ni ya haki kisheria, ikizuiwa kinyume cha sheria Viongozi wa CHADEMA wasitii, Kubalini kusacrifice hata Jela lakini haki yenu kama Chama muipate. Na hii mikutano isiwe one day event, itisheni hii mikutano mara kwa mara mpaka watawala waone kuwa gharama za kupambana na CHADEMA ni kubwa kuliko kutenda haki.

Ndugu Mbowe, Hii chain ya nyie kuonewa hamtaivunja mpaka msacrifice, muwe tayari kwenda jela kwa ajili ya course hiyo

4. Ni lazima CHADEMA itumie fursa za serikali ya CCM kuboronga kwenye uchumi ili kuvuna sapoti ya wananchi
Ndugu Mbowe, Kimsingi, CCM wanajua measures zao za kiuchumi ni unpopular kwa wananchi, pia wanajua legitimacy yao ya kisiasa kwa wananchi ni ndogo sana, kwa hiyo wanachokifanya ni kujaribu kwa nguvu zote kuweka ukuta baina yenu na wananchi ili msiwape hao watawala kibano cha kisiasa. Ni lazima message yenu sasa muiegemeze katika ugumu wa maisha ambayo wananchi wanapitia na kwenye fact kuwa tumefika hapa kwa sababu ya utawaka mbovu wa CCM na wananchi hawana wawakilishi waliotokana na ridhaa zao. Tumieni kila opportunity, tengenezeni talking points za matatizo ya kiuchumi muzisambaze hadi huko chini kwa viongozi wenu wa ngazi za chini ili waweze kuwaeleza wananchi kwa ufasaha kabisa madhila ya utawala wa CCM kwenye maisha yao, na namna CCM inavyopekekea wao kuwa na maisha Magumu

5. Ni muda muafaka wa kumuomba kila mwanachadema afanye kazi ya kusambaza ujumbe wa Chama
Ndugu Mbowe, CCM wanadhani wanaweza kudhibiti moto wa CHADEMA kwa kuthibiti uongozi ambao uko structured, kwamba wakidhibiti let say viongozi wa matawi, mashina, kanda na viongozi Taifa basi wataweza kukithibiti Chama. Sasa ni muda muafaka wa Chadema kutoa muongozo kwa kila mwanachama na shabiki na Chadema kufanya kazi za chama za kusambaza jumbe na sera za chama. Agiza kila mtu, afikishe ujumbe na sera za chama kwa marafiki, kwa majirani n. k. Yaani kwenye suala la kusambaza jumbe za CHAMA isiwe muda wote centralized bali nyakati kama hizi ngumu mnazozuiwa kuorganise iwe ni decentralized. Hii itawezesha ujumbe kufika pale ambapo watawala hawataki mfike!

6. Ni lazima kuionyesha sura halisu ya Rais Samia, ajulikane kabisa kuwa naye anaenjoy "urahisi wa Udikteta" na anachukia "ugumu wa demokrasia"
Demokrasia siyo kazi nyepesi, inahitaji kutumia akili zaidi, kujizuia zaidi, kuwa na subira zaidi, maridhiano zaidi. Sasa hayo ni mambo magumu kuliko udikteta ambao madikteta hawataki kuumiza kichwa sana kwenye utawala, wao wanataka kutumia miguvuguvu tu
Sasa Samia inaonekana kabisa anataka kufuata njia za Mtangulizi wake, hataki tabu, anataka kutawala kwa mteremko. Lakini wakati huohuo anataka kuudanganya ulimwengu kuwa yeye ni mwanademokrasia, Hataki kuitwa "DICTATOR". Sasa CHADEMA isikubali kumpa hii blank cheque, kama anafanya Udikteta aitwe dikteta, asakamwe kwa udikteta wake.
Na hapa naungana na John Heche, Acheni kumuita Samia MAMA. hii inampa soft power, na moral authority ambayo connotation ya mama inabeba. Kiufupi kama anavunja katiba ya nchi basi haistahili kuendelea kutumia hilo jina mama, muiteni kwa jina lake halisi, kama ni dikteta basi aitwe Dikteta.

7. Madai ya Katiba mpya ni turufu inayopaswa kutumika kwa nguvu zote
Ndugu Freeman, katika vitu ambavyo wananchi wengi wanakubali, bila kujali mirengo yao ya kisiasa ni katiba mpya. Hii ni turufu kubwa ambayo hata CCM wanashindwa waihandle vipi. Sasa ni muhimu sana nyie kuiframe agenda hii kuwa ni kwa ajili ya masilahi ya wananchi zaidi, katika kufanya hivyo nashauri nyie kama chama mkae muandae points za namna gani Katiba mpya inagusa maisha ya watu moja kwa moja. Hizi talk points zisambazwe kwa makada wenu wote nchi nzima. Lengo hapa ni kuondoa ile spin kuwa nyie mnapigania katiba mpya kwa ajili ya madaraka tu.

Elezeni faida za bunge na mahakama huru, elezeni katiba mpya inapambanaje na ufisadi, elezeni katiba mpya ina uhusiano gani na maji yao, elimu ya, afya yao. Namna hii mtaweza kuwashawishi wananchi wawe active zaidi na zaidi katika kuidai na kuilszimisha serikali ya CCM ilete hiyo katiba mpya. Msiishie tu kuzungumzia ishu ya tume huru ya uchaguzi na madaraka ya rais jinsi yasivyo fair bali onyesheni jinsi vitu hivyo vinavyopelekea maisha ya watu kuwa magumu zaidi.

Mwisho kabisa ndugu Mbowe napenda kukwambia kuwa sasa ni muda muafaka wa kuraise joto la kisiasa nchini, lipandisheni kwa kugomea amri haramu. Fanyeni mikutano hata kama imezuiwa kinyume cha sheria. Hawa hawana mabomu, wala askari wa kutosha wa kuweza kupambana na HAKI

Chairman, mmeonewa kiasi cha kutosha, mmenyanyaswa kiasi cha kutoshao sasa fanya jambo, tumechoka!
Atanyea debe maisha yake yote, mdanganye!

Kwenu hakuna utawala ulio mzuri? Mkapa hakuwafaa, kikwete hakuwafaa kwamba alikuwa lazy, Magufuli kwenu alikuwa dictator, Madame president hafai tena kwenu?? mnataka nchi iongozwe na nani???

Kiukweli ni bora Tadea kuliko mawazo yenu, badilikeni...
 
Mimi sijawaona CHADEMA waking'ang'ania kubaki madarakani, na hata kukataa kabisa kuboresha katiba ili kura za wananchi ziweze kuwa na nguvu ya kuwabakisha madarakani au kuwaondoa.

Katika mambo yote, pengine hili kwangu ni la muhimu zaidi.
Ni nani anaeweza kumchallenge Mbowe leo akabaki salama.

Ni kwanini vifungu vya kikatiba vyote vilivyoonekana kumsumbua Mbowe alivibadili ?

Ni kwanini linapotokea jambo ambalo Mbowe huwa anaona lina maslahi kisiasa katiba huwa anaweka pembeni. Mfano halisi ni Lowassa kupewa fomu ya kugombea yeye peke yake.
 
Back
Top Bottom