Barua kwa Mhe. Zitto kutoka Mtwara

Barua kwa Mhe. Zitto kutoka Mtwara

Umetumwa wewe,Huna hoja unatapatapa tu.Ukiulizwa unachojadili ninini?kinamaendeleo gani kwa taifa hunajibu zaidi ya kuchekacheka.
Zitto ametukuka huko mtwara kapewa ujumbe wake,Wewe na nape kaeni chonjo,2015 ikulu hiyo


HIKI NDICHO ULICHOKILENGA KWENYE BANDIKO LAKO WALA SI KINGINE!
MIMI NI WA MTWARA , na ninaishi huko since 2005 huwezi kunidanganya kitu kaka. Hata huyo ndugu Komba MWANDISHI WA WARAKA HUO namfahamu vema,yupo kwenye asasi isiyo ya kiserikali iitwayo FAWOPA (Faidika Wote Pamoja).

Hata kama unamtaka ZZK, hii njia ulioamua kuitumia sio muafaka kwa sababu inakudhalilisha wewe kwa kuonekana hauko makini, pia umemdhalilisha aliyeandika waraka huo kwani anaonekana hafahamu nini alichokikusudia.
 
Ndugu yangu zitto,rais wa mioyoni mwa watanzania wana mtwara wamekuandikia barua kwamba uokoe jahazi sasa hayo maneno kwamba ushauriane na chama tena yanatoka wapi?
Kwanini usifanye kama vile ulivyofanya tanga?uliiandaa mwenyewe ukisema usubili chama utakwamishwa na kuundiwa mizengwe hata usifanikishe adhima ya wana mtwara!
Chonde chonde andaa ziara uende ataetaka kukujoin atakujoin mambo yakushauriana na chama ndo yale yale ya kutoa majibu ya "tupo kwenye mchakato"
Go go go zitto!
Your votes count!

We huna nia njema na CHADEMA........hizo sehemu nilizo underline zinaonesha wazi kuwa unataka kumfanya ZITO mtoto mdogo asiye uelewa......UNAMSHAURI AJITENGE NA CHAMA!AFANYE MAMBO KIVYAKE ILI MUANZE KUMSHAMBULIA NA HATA MJE KUTANGAZA KUWA HAELEWANI NA WENZAKE,MARA CHADEMA WAVURUGANA.
 
Tutashauriana na chama tufanye tena ziara kusini, ziara ya kusikiliza wananchi

Kweli wewe mburula,nimeamini wewe ni tatizo...kusifiwa tu na Mkeo TUNTEMEKE basi umefurahiiiiiii..ata huoani jamaa ka edit makala ya mtu kukufagilia wewe.Mh Zitto, Kinana ni kijana wako? Sipingani na wazo la ziara ya kusini ila tu ulimbukeni wako wa kupenda sifa.
 
Last edited by a moderator:
Hiyo barua kama ipo kweli sioni tatizo ikiandikwa kwa Zitto kama mbunge anayeshughulika na rasilimali za taifa.
Ameshafanya hivyo huko nyuma mara nyingi tu.

Tatizo linalojitokeza ni kuwa mleta mada anafahamika kama ''CDM Insider'' ambaye si tu amekuwa akishambulia viongozi wanaofanya kazi na Zitto bali amekuwa akileta sintofahamu kwa mabandiko yake yenye tuhuma za kufikirika bila ushahidi.

Mheshimiwa Zitto amejibu kuwa watalifanyia kazi suala hilo na chama.
Sina uhakika kama amehakiki usahihi wa hiyo barua.

Lakini muhimu sana Zitto alitakiwa kwanza ajitambue mwenyewe kama mbunge, mwenyekiti wa kamati ya bunge na Naibu Katibu mkuu wa CDM sio Rais. Hivyo alitakiwa ku-denounce hiyo title.

Kwa kuzingatia controversy zilizojitokeza huko nyuma nisingemshauri ZZK kukubali neno hilo.
Kibaya zaidi tuhuma za uhujumu wa chama zinazoendelea kwa kutumia BAVICHA hazimweki katika picha nzuri.

ZZK kama mwanachama wa CDM ana haki zote za kiuanachama kushiriki katika shughuli za chama.
Swali linabaki je anatumiaje hizo haki bila kuathiri mustakabali wa chama? Je, anatumia njia sahihi!

Kusema tu nitashauriana na chama inabeba tafsiri tofauti sana miongoni mwa jamii. ZZ alitakiwa aende mbali kukanusha hilo neno la Rais na hata kuwataka wahusika wafikishe suala hilo katika uongozi wa chama ambako naye ni mwanachama na kiongozi.
 
Kweli wewe mburula,nimeamini wewe ni tatizo...kusifiwa tu na Mkeo TUNTEMEKE basi umefurahiiiiiii..ata huoani jamaa ka edit makala ya mtu kukufagilia wewe.Mh Zitto, Kinana ni kijana wako? Sipingani na wazo la ziara ya kusini ila tu ulimbukeni wako wa kupenda sifa.
ni vema pia akajiuliza kama ameshawahi kuhutubia kamati ya ushindi Daslam na kusema maneno haya ''wao wakisema uongo tusipo jibu itaonekana ni kweli''
sijui ni kipi huwa kinamfanya awe anakubaliana ni mishen za huyu jamaa coz pamoja na huyu dogo kuonesha unafiki wa hali ya juu bado anamkumbatia tu.

I just wonder kama kweli huwa halioni hili, otherwise nashawishika kusema kuwa lisemwalo lipo...
Sijui labda tumuombe tena dada Ashadii atuulizie kama huyu ndiye yule Zzk tumzaniaye ama tumsubiri mwingine
 
Last edited by a moderator:
mlichagua kanga na vitenge sasa leo mnajuta,mliletewa sera nzuri ya majimbo watu wa magamba wakaipotosha kusini mkacheza ngoma ya nambari one eehee ni ccm,mnao hao ila 2015 second chance
 
Mi nashangaa hii topic jana ilianzishwa na muumini safi lakini leo naona ameanzisha Tuntemeke.Sielwi!
 
SIWEZI KUBISHANA NA WEWE KATU,KAMA UMESHINDWA KUNIELEWA KWAMBA HII BARUA NIMEKABIDHIWA KWA EMAIL IKIWA IMEANDIKWA MPATIE ZITTO MATATIZO YETU HAYA.
SASA NIKAPELEKE KWA JK ILI HALI NIMEAMBIWA NI MZIGO WA ZITTO?KUNA AKILI KWELI HUKO KICHWANI AU LA?
PILI UNAONA HOJA ZA KUJADILI HAPO CHINI?
ARDHI NA GESI NDIO HOJA..HOJA ULIOIZALISHA YA EDITING ZA HII CHAPA NI JUU YAKO.
MM ZITTO MWENYEWE WALLAH SIFAHAMIANI NAYE,HANIJUI SIMJUI.SILIPWI CHOCHOTE NA KUANDIKA JEMA AU BAYA LOLOTE JUU YAKE.
ZITTO KWANGU MM NI PICHA TU,HANA MSAADA WOOTE.LAKINI SINA UGOMVI NAYE NA SIMCHUKII ZAIDI YA KUMKUBALI SANA TENA SANA KUTOKANA NA SIASA ZAKE NA NAMNA ANAVYOJUA KUPAMBANUA JAMBO.
NASHUKURU MZIGO UMEFIKA SALAMA NDIO HUU HAPA TENA,KAZI KWAKO WEWE CCM INAKUUMA KWELI KUONA CHADEMA KUNAMTU ANAITWA RAIS,2015 SIO MBALI MMEKWISHA.
NANUKUU HAPA CHINI MAANDISHI YAKE
"No.. No..Situmi ujumbe huu kwa mtu yeyote kwa kuwa huu ni ujinga wetu wa kuuza kura kama chapati na sasa tunakumbuka shuka asubuhi, hivi kweli gesi hii ingekuwa katika jimbo la Mchungaji Msigwa, Mnyika"

Niko pamoja nawe hao roho na wivu wa kijinga unawasumbua.donge la nn bwana kama watu wanamkubali Zito muawache.pokea barua Mh rais mtarajiwa then fanyia kazi kama wananchi wa mtwara walivyokuamini
 
jamani huyo Zitto mnamfahamu vizuri lakini? Uraisi sio kuwa na bezi yaani sauti nzito, URAISI NI KUWA NA HESHIMA NA AKILI YA KIUTU UZIMA!!!
 
Mi sijaelewa jamani ina maana rais wa kusini ni zito?kama ni zito kwani yeye ndie aliwaambia wachague magamba na si walipewa kanga na pilau sasa wanalalamika nini?wacha gas ije dar wao wao wabaki kulalama tu,chezea mafisadi wewe

Mkuu jamaa ameweka kichwa cha habari as if anamu-address Mh.ZITTO ili avutie wasomaji, lakini lengo lake hasa ni kuisema Serikali ya awamu ya nne!

Labda niseme kitu, kuna mambo mengine nakubaliana naye kuhusu mapungufu fulani kwenye mkoa wao kwamba labda hawajatendiwa haki, lakini ukizunguka karibu mikoa mingi ya Tanzania ina matatizo yanayo fanana, ukienda mkoa wa Kagera utasema afadhali mikoa ya kusini ina unafuu wa aina fulani - mimi nafikili tumpe muda JK, anajitahidi kujaribu ku-address mapungufu ya hapa na pale, tukumbuke Tanzania ni nchi kubwa sana kuliko nchi yoyote East and Central Africa save DRC, niliwahi kumsikia akizungumzia suala la gas na jinsi wenyeji wanatavyo nufahika na nishati hiyo - kwa nini hampi muda akatekeleza ahadi zake bila ya kuwekewa unneccessary pressure/lawama after all one of his family member anatoka mikoa ya huko kusini, sina shaka anaelewa kila kitu?

Kitu cha mwisho, Watanzania wakati mwingine tuwe tunakuwa consistent - zamani niliwa kusikia mikoa ya kanda ya ziwa ikililalamika kwamba imejaliwa kuwa na natural resources nyingi kwa nini hawanufahiki na samaki/madini yanayo chimbwa huko, niliona mikoa mengine inawajia juu eti msitake kuigawa nchi, mali ni kwa manufaa ya Taifa lote; sasa hivi hilo alisemwi mnamugeuzia kibao JK mnasema mkoa wenye GAS unufahike kwanza mikoa mingine baadae, yaani napata impression kwamba ikiwezekana gas hisiwe pumped kwenda DAR kwa ajili ya ku-generate umeme wa kusambaza nchi nzima, hii ina maana gani!
 
Sijaelewa kwa Zitto ana uhusiano gani na kusini? Nani au kikao gani kilimteuwa kuwa mtetezi wetu sisi watu wa kusini? kwa nini unatumia matatizo yetu kumfanyia kampeni huyo Zito ambaye wewe unamwona kuwa anafaa kuwa Rais? Ifi aliekuambia gesi bila matumizi itawasaidia wana Mtwara kuondokana na umasikini wetu? Mbona gesi ilikuwepo iligundulika tangu mwaka 1982 pale msimbati tuliachiwa kabla Artumas kuja kuichimba mbona tulikuwa hatuitumii? Sasa Serikali wakiicha ndiyo tutaendelea hivyo ndivyo anavyojinadi Zitto kuwa ana wawekezaji wa gesi? Mbona sasa karibu miaka kumi tangu Artumas waanze kuichimba na wamekaa nayo tu mpaka wakauza na kamapuni hawajampata wa kumuuzia? Wanasiasa wasitutumie vibaya?
 
Nausikitikia Ufahamu wako pia! Hapa Tunazungumzia mstakabali wa nchi nzia wewe unaleta mambo ya Kigoma. Matatizo ya nchi yetu ni makubwa kuzizidi busara za ZK so sioni kwa nini watanzania wewe ukiwemo usitumie busara kidogo na kutambua ni aina gani ya kiongozi anahitajika kuleta ukombozi wa kweli tanzania na sio huu wa kwenye vyombo vya habari!
 
Kwa Mantiki hiyo sasa naielewa dhima ya topic hii!!!
 
Zitto anangekewa????Duhh kutoka Kigoma to Mtwara anaitwa Rais?Hongera zitto kabwe,unaonekana wewe si mtu wa kawaida nchini

Invisible unaweza kutuambia ni nini hiki??
Tokea jana naona hayo mambo akiquotiwa tuntemenke anakuja gwakisa au muumin safi???whats wrong ni mtu mmoja au?
 
Last edited by a moderator:
ZITTO. A.k.a Sangoma, a.k.a Tumtemeke kaumbuka...Sura zenu mtaficha wapi Prezzo !
 
ZITTO. A.k.a Sangoma, a.k.a Tumtemeke kaumbuka...Sura zenu mtaficha wapi Prezzo !

Daaah, Zitto nilikuwa namheshimu sana...

Sidhani kama nitavumilia kuendelea kuangalia TV kama sura yake ikitokea, kwa utoto huu wa kujizungusha kijinga namna hii...

Naamini Tuntemeke ndio Zitto, na aliibuka kwa kasi sana kuhujumu uchaguzi wa Arumeru ili Nassary asishinde, then Nassary akaenda Kigoma kum-endorse Zitto kwenye lile tamasha la Leka Tutigite, jambo usilolijua ni usiku wa giza.

Ahsante Ben Saanane..
 
Back
Top Bottom