Baraza la Mawaziri Limevunjwa! (2008)

Baraza la Mawaziri Limevunjwa! (2008)

Chuma mkuu wangu,mtake radhi Masatu bwana! tunakata issue tuu,mambo ya u-CCM hayapo hapa.
Mbona mama Kilango kazoza ile mbaya ndani ya jengo ilihali yeye ni CCM? Tunapambana na ufisadi kwa pamoja bila kujali itikadi.

Nafikiri Chuma HATAKIWI kumwomba radhi Masatu isipokuwa ni wa wakati wa Masatu kujihoji kuwa ni kwa nini baadhi ya wana JF wamemwona hana mvuto tena hadi issue zake watake zipitie kwa wengine.
Hili ni anguko.Ukistaajabu anguko la Lowassa utaona la nanihii.
Hahahahahhaha
 
JK kama ana nia ya kweli ya kuendeleza nchi yetu na nimsafi kweli basi PM ampe mpinzani kama Dr Slaa ,na kama akichagua CCM basi ampe mpinzani wa mtandao POMBE. aone mchakamchaka
 
Mimi kwa sasa sina imani kabisa na mtu yeyote ambaye amewahi kuwa ndani ya serikali ya CCM,Kansa ya ufisadi imeenea sana kwa sasa kujaribu kujua nani msafi nani si msafi ni kupoteza muda labda ukiwatoa wale ambao tayari wako kwenye List of shame ya Slaa na Mwakyembe,wengine wanaweza kuwa silent killers,wakipewa rungu wanaonyesha makucha.Kwa kuwa Tanzania sasa ni kichwa cha Mwendawazimu tusubiri huyo PM mpya akitunyoa ndio tutajua kama ni msafi au hapana.Ubaya ni kuwa tukija kushtuka kuwa hafai watu wengi watakuwa wameshakufa kwa malaria,UKIMWI na utapiamlo sababu pesa yote hazina itakuwa imepelekwa Dubai
 
JK kama ana nia ya kweli ya kuendeleza nchi yetu na nimsafi kweli basi PM ampe mpinzani kama Dr Slaa ,na kama akichagua CCM basi ampe mpinzani wa mtandao POMBE. aone mchakamchaka

Kweli unamtaka Pombe awe PM?
 
Inaonekana kama Jk ana imani na wasomi kwa kiasi flani. trends zinaonyesha amewapa nafasi za juu za kisiasa watu wengi wenye elimu ya juu. Ni ngumu kujua nani atakuwa PM lakini naweza kutabiri kuwa this time ataibuka na mtu mwenye atleast PHD.

Mungu atunusuru na wenye PH.D!!!
 
Kokolikoooooooooooo, kumepambazuka Tz...at last wenye uchu wa mali wamezidiwa kete, na huyo ni mwanzilishi wengine wafuate tena kwa mwendo wa "KUNYAKUA" waige mfano wa BOSS wao ...Wallahi, mwaka umeanza vyema huu, kweli nimeamini "kila jambo na wakati wake chini ya Mbingu"
JK wake up man...mwajibishe Lowassa na wote wengine hakuna kuoneana haya wakati ndio huu, tuutumie ipasavyo.Na huu ni mtihani mkubwa wa kiutendaji kwako kama Rais; kutokana na yote haya yanayoendelea tuna imani haba na wewe, PROVE US WRONG FOR ACTING ACCODINGLY! Lowassa alifikiri kujiuzulu ni kujisafi SISI tunaita Kusarender miguu juu na tunatakiwa tukufanyie kazi...kabla hajaota MBAWA,ataruka huyo na ndege yake Kwi,kwi,kwi,kwi..kulaleki!
At last I have a NEW YEAR gift from my lovely TZ, is kind of late but I'll take it anyway!!!!!VIVA TANZANIA
🙂
 
JK SHORT LIST YA PM NI KATI YA HAWA (5):

1.BENARD MEMBE (KUSINI)

2.MIZENGO PINDA (NYANDA ZA JUU KUSINI/MAGHARIBI)

3.STEVEN WASSIRA (KANDA YA ZIWA)

4.PHILIP MARMO (KANDA YA KASKAZINI)

**5.SAMWEL SITTA ( KANDA YA KATI)

***5. Mzee 6 Inaweza kuwa Ruled Out kutokuwa tayari Waziri, atakuwa mkristo kati ya hao, kutoka kanda kasoro Mashiriki, JK ni EAST tayari...Sio Mwanamke, ni Mwanaume!!
 
Kweli unamtaka Pombe awe PM?

Pombe hana tofauti sana na El, tofauti pekee ni kuwa yeye sio fisadi kama EL, la linalowafanya wafanane sana ni tendecies za kuwa na utawala wa kiimla.
Lowassa alikuwa analifanya bunge kama kindergaten na kulichezea kama alivyopenda, na kudanganya watu kuwa uchumi wa Tanzania unapa wakati uchumi wake yeye ndio ulikuwa unapaa!
 
kama nilivyosema juzi kuwa LOLOTE LITAKALOTOKEA LINA BARAKA ZA KIKWETE.....ALISHAAMUA KUMTOSA RAFIKI YAKE..

DURU ZINASEMA KUWA UHUSIANO WAO ULIKUWA UMELEGA SANA....NA HII KWA KIASI KIKUBWA INATOKANA NA AMBITION ZA URAIS ZA BAADHI YA WATU...NA PIA KUNA BAADHI YA WASHAURI WA RAIS [MARAFIKI]..WALIKUWA HAWAFURAHISHWI NA UTENDAJI WA PM KUMU OVERSHDOW JK.....

KUNA WALIOKUWA WAKIMPAKAZIA KWA JK KUWA HAFUATI MAAGIZO YAKE..BALI ANAJIFANYIA KAZI KWA UTARATIBU ANAOUTAKA YEYE....

VIONGOZI WENGI WANAPENDA KUWA NA WASAIDIZI DOWN LOW...KAMA WOTE NI MAARUFU KITAKACHOTOKEA NDIO KAMA HIKI CHA JK NA LOWASSA KUVUNJA UBIA RASMI......MKAPA ALIWEZA KUDUMU NA SUMAYE KWA SABABU AINA YA UTENDAJI WAKE ULIKUWA NI WA KUPOKEA MAAGIZO KAMA KAWAWA....

MNAWEZA KUONA MAWAZIRI WAKUU AGRESSIVE KAMA SOKOINE WALIVYOISHIA...HATA MTU KAMA MALECELA ILIKUWAJE!!!

LOWASSA ANA MAKOSA LAKINI LAZIMA MJUE KUANGUKA KWA LOWASSA NDIOO MWANZO WA KUMOMONYOKA KWA NGUVU ZA KISIASA ZA KIKWETE ...NA WATANZANIA WASIWE NA MATARAJIO MAKUBWA KUWA BAADA YA LOWASSA KUONDOKA SASA KILA KITU KITAKUWA SAWA NA MAISHA BORA YANAKUJA...LA HASHA!!!


Nafikiri cha kuangalia sasa hivi ni jinsi urafiki wa Lowassa na Kikwete utakavyo play..kama wataendelea kuwa marafiki wakubwa na Lowassa kuwa na no ill feelings then itakuwa a win win situation kwa Kikwete, lakini kama Lowassa na Kikwete wakiwa maadui kutokana na hii resignation, basi ninaamini asilimia 100% Lowassa atafanya kila awezalo ku sabotage Presidency ya JK. Ninamfahamu Lowassa ni mtu wa kulipiza visasi. Kule Monduli wakati wa uchaguzi wa ubunge mwaka 2005, alimfungia mwananchi mmoja bucha lake la nyama maeneo ya stendi ya basi Monduli kwa sababu huyo mwananchi alionesha nia ya kushindana na Lowassa kwenye kiti cha ubunge kwa tiketi ya chama pinzani. Cha kushangaza ni kwamba huyo mwananchi hakuwa na threat yeyote ile kwa mheshimiwa, ila kwa sababu jamaa anapenda kupita bila kupingwa ilibidi afanye ubabe. Baada ya kujitoa kwenye kinyang'anyiro huyo mwananchi aliruhusiwa kuendelea na biashara yake ya nyama.
Lowassa and Company...(ana ngome kubwa sana Arusha) wamefanya kazi ya nzuri sana ya ku raise hela na pia kumuuza Kikwete kwa wananchi japokuwa Kikwete alikuja na mvuto wake wa kipekee kutokana na wananchi kuchoka na regime ya Mkapa. Itakuwa interesting kuona..Ikiwa Lowassa atahama mji na atakuwa bitter basi Kikwete will have a very difficult time kumalizia term yake. Yetu macho.
 
Lowassa nje ya serikali si tishio kwa JK hata chembe! Akileta za kuleta wanaweza kumtoa kwenye ngazi zote za uongozi alizobaki nazo (ubunge na kwenye CCM) kwa tuhuma hizohizo zilizomtoa u-PM, kisha anashitakiwa, na mwishowe anasahauliwa kama Nalaila Kiula!
 
Kithuku...napenda kutofautiana na wewe. Sidhani kama JK ataweza kuupeleka uhusiano wao ufikie hatua hiyo ya yeye kufunguliwa mashtaka. Ninafikiri kuwa JK ana plan B kwa ajili ya swahiba wake Lowassa. Na nina imani kuwa atatumia kila awezalo kuhakikisha kuwa yuko karibu na EL japokuwa sio kwenye uongozi.
 
Kithuku...napenda kutofautiana na wewe. Sidhani kama JK ataweza kuupeleka uhusiano wao ufikie hatua hiyo ya yeye kufunguliwa mashtaka. Ninafikiri kuwa JK ana plan B kwa ajili ya swahiba wake Lowassa. Na nina imani kuwa atatumia kila awezalo kuhakikisha kuwa yuko karibu na EL japokuwa sio kwenye uongozi.

Sawa, lakini itabidi Lowassa naye abihevu, vinginevyo akimchokonoa swahiba wake atashindwa kumvumilia. Hadi hatua ya leo keshambeba sana, isingekuwa uswahiba angeshamtema siku nyingi. They are both standing on slippery ground, lakini JK anapo pa kushikilia asianguke, kwa hiyo Lowassa akitaka kumwangusha nina hakika uvumilivu utakosekana, itakuja ile ya "bora lawama", au wa mjini siku hizi wanasema "kama noma na iwe noma!"
 
Nafikiri cha kuangalia sasa hivi ni jinsi urafiki wa Lowassa na Kikwete utakavyo play..kama wataendelea kuwa marafiki wakubwa na Lowassa kuwa na no ill feelings then itakuwa a win win situation kwa Kikwete, lakini kama Lowassa na Kikwete wakiwa maadui kutokana na hii resignation, basi ninaamini asilimia 100% Lowassa atafanya kila awezalo ku sabotage Presidency ya JK. Ninamfahamu Lowassa ni mtu wa kulipiza visasi. Kule Monduli wakati wa uchaguzi wa ubunge mwaka 2005, alimfungia mwananchi mmoja bucha lake la nyama maeneo ya stendi ya basi Monduli kwa sababu huyo mwananchi alionesha nia ya kushindana na Lowassa kwenye kiti cha ubunge kwa tiketi ya chama pinzani. Cha kushangaza ni kwamba huyo mwananchi hakuwa na threat yeyote ile kwa mheshimiwa, ila kwa sababu jamaa anapenda kupita bila kupingwa ilibidi afanye ubabe. Baada ya kujitoa kwenye kinyang'anyiro huyo mwananchi aliruhusiwa kuendelea na biashara yake ya nyama.
Lowassa and Company...(ana ngome kubwa sana Arusha) wamefanya kazi ya nzuri sana ya ku raise hela na pia kumuuza Kikwete kwa wananchi japokuwa Kikwete alikuja na mvuto wake wa kipekee kutokana na wananchi kuchoka na regime ya Mkapa. Itakuwa interesting kuona..Ikiwa Lowassa atahama mji na atakuwa bitter basi Kikwete will have a very difficult time kumalizia term yake. Yetu macho.


Lowassa hana ujanja wowote wa kujifanya mtemi nchini Tanzania.
Ukiwa nje ya System Makende yote yananywea ndani kama mtu mwingine yeyote.

Watu wangapi walipo kuwa na vyeo serikali walionekana wana Hirizi ya Simba mla watu?

Wako wapi sasa hivi! Wamepotelea kwenye udhaifu wao wenyewe.

Wengine wamepat Stroke kwa kuzomewa kila wapitako.

Hata hizo biashara zake zitakufa moja baada ya nyingine, kama alipata tenda kwa sababu yeye ni waziri mkuu ajiandaye tu.

Na huyo mwanaye analelewa kama kinda la mwewe ni vema aanze kuota manyoya na kukomaa vipapatio, wakati wa kutapikiwa msosi na mzee wake mamvi umekwisha. Sasa inabidi aendeshe biashara kwa misingi ya faida na hasara siyo Spoon Feeding.

Bado tuna genge kubwa la Wahuni ndani ya serikali, kule wizara ya Fedha na wizara ya sheria wamejaa wahuni wengi ni lazima waadabishwe wote. Bila kusahau mama lao BOT.

Wizara ya mali asili nako kuna Genge la Mafia ambao wameuza serengeti kwa magaidi wa dunia na fedha yote kuitia ndani.

Tunataka nchi yetu tena tunaitaka yote siyo kipande.

Tukiiweka mikononi mwetu ninyi akina Lowassa msifikiri yamekwisha,
ni lazima tuwapeleke Mahakamani mkajibu mashitaka ya kuhujumu uchumi.

Hili la kuwashitaki tutalivalia njuga kweli kweli, anaye Save ni yule anayerudisha namba kwa Muumba tu kama yule mzee wa ENRON.
 
Quote:" Breaking News: Baraza la Mawaziri Limevunjwa!
Taarifa za sasa ni kuwa cabinet imevunjwa na Rais anapeleka jina la PM mpya bungeni kesho saa tatu asubuhi"
Watanzania embu amkeni, Raisi anapeleka jina la PM bungeni????anampelekea nani? hivi kwanini sisi tusipeleke jina la RAISI mpya Tanzania, tupelekee watu wanaotaka maendeleo yetu wananchi, siyo watu wanaotufanyia maisha ya watu 90% kuwa masikini na hali duni.we are really tired with wabunge kulala huko bungeni, we need to change people every corner. CCM dude ur not Tanzania, we the people ARE. stop the Top crimes, we need our money back JK from BOT, we dont need you to take the name of a new PM to the parliament. we can do without one, just use this month's PM's salary to build roads,we need technology,electricity,new education.
 
Fikiri, there is something called a constitution... And salary ya PM haitoshi kujenga barabara hata mita 5. your passion is admirable lakini lazima ifuate the rule of law. Bila hivyo we risk turning into radicals and dictators.
 
Madela wa Madilu:
Nakubaliana na maoni yako, ndio maana Benjamin Mkapa yuko very quite japokuwa magazeti nyumbani yanamwandika kwa pace wanayotaka wao. Wakati Mkapa alipokuwa madarakani media haikuwa na makucha waliyonayo sasa. I think Lowassa will chose to abide na whatever mkuu JK wants him to.
 
Kithuku...napenda kutofautiana na wewe. Sidhani kama JK ataweza kuupeleka uhusiano wao ufikie hatua hiyo ya yeye kufunguliwa mashtaka. Ninafikiri kuwa JK ana plan B kwa ajili ya swahiba wake Lowassa. Na nina imani kuwa atatumia kila awezalo kuhakikisha kuwa yuko karibu na EL japokuwa sio kwenye uongozi.

Makao Makuu,

Mara nyingine inabidi mtu ujiulize je urafiki huu una manufaa gani? If I were Kikwete, I would ask myself why keep ties with Lowassa if what he has done is an embarrasment and shameful? If he keeps him close, then he is burying himself. Best he can do is drop him out of sight, from CCM and let him free without going to Ukonga or Keko.

Huwezi kuwa na urafiki na mtu ambaye anafanya mambo ambayo yanaweza kuangamiza utu na heshima yako.
 
Hivi ndugu wananchi wenzangu tunavyosema humu kwamba fulani awe PM kwa sababu ana experience ya kutosha what do we really mean? si hawa hawa wenye experience ndo wametufikisha hapa tulipo? kwenye umaskini wa kutupwa? Labda mseme wanaexperience ya kuiba na namna ya kupindisha sheria!

Mimi nadhani we should completely build our argument on other basis not this experience thing..sijui mama Makinda, Membe etc..I wouldnt mind to see a smart young man being appointed as PM. Honestly for TZ, these politics of experience has cost us dearly.

Look here, Lowassa, Msabaha, Karamagi et al are just like any other Criminals and they should be dealt with in accordance with the laws of the nation. The man is talking of natural justice! hana hata aibu, yeye alitupa hiyo natural justice watanzania ambao wamepoteza maisha kwa magonjwa yanayotibika...? He is so out of touch with reality. Watanzania wengi tumemchoka! And I strongly believe, this is the end of this Bafoon politically!
 
Wana JF hii nimeitoa michuzi sasa ivi

BUNGENI LEO
MH. SPIKA AFUNGUA KIKAO NA KUSEMA JK AMEKUBALI OMBI LA KUJIUZULU KWA WAZIRI MKUU MH EDWARD LOWASSA NA KWA KUSEMA HIVYO BARAZA LA MAWAZIRI LIMEVUNJWA ATOMATIKALI NA NDIO KUSEMA HALIKO TENA.
NA KWA KUWA SERIKALI HAIKO MH. SPIKA AMESITISHA SHUGHULI ZA BUNGE HADI SAA KUMI NA MOJA AMBAPO KIKAO HICHO KITAENDELEA. SHUGHULI HII IMECHUKUA DAKIKA 6 TU

© Michuzi Tarehe: 8.2.08

Nafikiri hadi kufikia jioni tutakuwa tumeshajua pendekezo la JK ni nani...

Aluta kontinua...
 
Back
Top Bottom