Baraza la mashauriano ya kisasa la China linapanua ushiriki wa watu kwenye demokrasia

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG111426243486.jpg


Mikutano Miwili ya China yaani Bunge la Umma la China NPC na Baraza la Mashauriano ya Kisasa la China CPPCC inaendelea hapa Beijing. Hivi ni vyombo viwili vikubwa vya uwakilishi wa umma katika mambo ya utungaji wa sheria na mashauriano ya kisiasa. Uwepo wa vyombo hivi viwili kwa pamoja, ni sehemu ya umaalum wa mfumo wa kisiasa wa China unaohakikisha wananchi wanakuwa na uwakilishi wa kutosha na wenye ufanisi katika usimamizi wa nchi yao.

Tofauti na nchi za magharibi, China inafuata mfumo wa Demokrasia ya umma ya mchakato kamili, kwa maana kuwa wawakilishi katika ngazi ya shina wanachaguliwa kwa njia ya upigaji kura wa moja kwa moja, na wawakilishi hao wanapewa jukumu la kuwachagua wawakilishi wengine ambao pia wanakuwa wawakilishi wa wawakilishi waliopigiwa kura moja kwa moja, hao ndio wanakutana kwenye ukumbi wa mikutano ya umma mjini Beijing na kuwa wawakilishi wanaojadili mambo ya taifa. Hata hivyo uwakilishi wa namna hii una upungufu wake, kwani kimsingi umejikita kwa wanasiasa na watu walio ndani ya chama peke yake, na wale wasio ndani ya chama hawana nafasi ya moja kwa moja mbali na kutegemea wawakilishi. Kutokana na kutambua hili, uliwekwa utaratibu wa Baraza la Mashauriano ya Kisiasa ambalo uwakilishi wake umepanuliwa na unaweza kupanuliwa wakati wowote kwa mujibu wa mahitaji ya wakati, ili kuwe na uwakilishi mpana na wa kina.

Hii ni moja ya dosari kubwa kwenye mfumo wa kibunge wa nchi za magharibi, ambapo siasa ni kazi ya wanasiasa na wapiga kura kazi yao ni kupiga kura tu na kusubiri hadi uchaguzi mwingine. Kupitia Baraza la Mashauriano ya Kisasa, utaratibu wa uwakilishi hasa kwenye kutoa mapendekezo kwa chama tawala na serikali, umepanuliwa. Watu wasio wanasiasa wanaweza kukaa na kujadili mambo yanayohusu sekta zao tangu ngazi ya shina hadi ngazi ya taifa, na mambo wanayojadili yanaratibiwa na kuchujwa na kufikishwa kwenye vyombo ya juu vya maamuzi kupitia njia zilizowekwa kisheria.

Kuna baadhi ya wakati watu wa nje ya China walikuwa wanashangaa kuona aliyekuwa nyota wa mpira wa kikapu Yao Ming, kuwa mjumbe wa baraza la mashauriano ya kisasa. Lakini ukweli ni kuwa sekta ya mpira wa kikapu ya China inaweza kuwakilishwa vizuri na mtu mwenye weledi na uzoefu kwenye jambo hilo, na sio mwanasiasa ambaye asiye na weledi kwenye jambo hilo. Hali kama hii ipo kwenye sekta zote, iwe ni sanaa, michezo, ulinzi, elimu, viwanda, utamaduni, mazingira na hata diaspora.

Jambo lingine pia linaloshangaza watu ni kuwa, Mikutano Miwili ya China inapofanyika, inafanyika katika hali shwari bila wajumbe kuvutana masharti au kurushiana makonde, kama ilivyo kwenye vyombo vya uwakilishi vya nchi nyingine hasa nchi za magharibi. Undani wake ni kwamba kupitia mfumo mpana wa uwakilishi na majadiliano, mambo yanayohusu maslahi ya wananchi yanajadiliwa kwa kina toka ngazi ya shina, mengine yanashughulikiwa hata kabla ya kufika ngazi ya juu, na yale yanayofika ngazi ya juu, kikubwa ni kuyajadili kwa kujibu wa mazingira ya kisera na kuangalia utekelezaji wake.
 
Hata hivyo uwakilishi wa namna hii una upungufu wake, kwani kimsingi umejikita kwa wanasiasa na watu walio ndani ya chama peke yake, na wale wasio ndani ya chama hawana nafasi ya moja kwa moja mbali na kutegemea wawakilishi. Kutokana na kutambua hili, uliwekwa utaratibu wa Baraza la Mashauriano ya Kisiasa ambalo uwakilishi wake umepanuliwa na unaweza kupanuliwa wakati wowote kwa mujibu wa mahitaji ya wakati, ili kuwe na uwakilishi mpana na wa kina.
Hii yote ni bure as long as hawaruhusu vyama vya kisiasa apart from CCP ie upinzani wa kukwambia hapa hapana siko!
 
@idleo huwezi kuwa na demokrasia kenye chama kimoja ambapo mweyekiti ni Mungu!
 
Demokrasia gani unayoizungumzia wakati minorities hawana haki kabisa kwenye taifa.

Chama na selikari ndo vinakontrol kila kitu mpaka mienendo ya watu. Mpaka sasa mmebadilisha katiba ya ccp na selikari kwamba mtu au kampuni inatakiwa kutoa taarifa za kiintelijensia kwa SERIKALI ikitakiwa.

Na ndomana hata tiktok itakuwa banned kwenye nchi nyingi za ulaya na Amerika
 
Hii yote ni bure as long as hawaruhusu vyama vya kisiasa apart from CCP ie upinzani wa kukwambia hapa hapana siko!
China wana vyama ila huwa havishiriki kila kitu. Unaweza ukakuta NCCR wao wanaruhusiwa kuongrlea mambo ya elimu tu na menginryo. Chama kingine kinapewa kuongelea kilimo tu na hadi wizara wanaweza wakapewa
 
China wana vyama ila huwa havishiriki kila kitu. Unaweza ukakuta NCCR wao wanaruhusiwa kuongrlea mambo ya elimu tu na menginryo. Chama kingine kinapewa kuongelea kilimo tu na hadi wizara wanaweza wakapewa
ASANTE KWA KUNIJUZA HILO. HUO NDIO USHENZI NA UKORA WA UKOMUNISTI.
 
Back
Top Bottom