Baraza la Maaskofu Katoliki kuhamia Dodoma

isupilo

JF-Expert Member
Jan 25, 2015
303
1,254
BARAZA la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) limethibitisha kuwa lina mpango wa kuhamisha makao yake makuu kutoka Kurasini jijini Dar es salaam kwenda Dodoma. Hayo yameelezwa na Makamu wa Rais wa TEC ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma Mhashamu Beatus Kinyaiya, wakati wa Misa Takatifu ya kilele cha jubilei ya miaka 100 ya upadri Tanzania, iliyofanyika katika kituo cha hija cha Mbwanga, Dodoma.

Akitoa salamu za TEC katika maadhimisho hayo yaliyohudhuriwa na mamia ya waamini, Askofu Kinyaiya amesema kuwa baraza lina mpango wa kuhamisha makao yake makuu yaende Dodoma na mchakato huo utaanza baada ya kufanya mazungumzo na serikali ya kupata ardhi itakayotumiwa na shughuli za TEC.

“Tuna mpango wa kuhamisha makao yetu makuu yaje Dodoma. Bado tunaongea na serikali ili tupate kipande cha ardhi, ambapo leo pia tumebariki jiwe la msingi la kikanisa kitakachojengwa mahali hapo” ameeleza Askofu Kinyaiya.

Kwa upande wake mwakilishi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika sherehe hizo, ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, George Simbachawene, ametoa agizo kwa serikali ya Mkoa wa Dodoma ihakikishe inafanya mazungumzo na TEC ili ndani ya siku 10 kiwanja kiwe kimepatikana kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Makao Makuu ya TEC.
“Maamuzi ya kubariki jiwe la msingi la kikanisa cha TEC kama ishara ya kuhamia Dodoma ni ujumbe mzito sana kwa serikali ya awamu ya tano na serikali ya Dodoma. Ninaagiza ndani ya siku kumi zoezi la upatikanaji wa kiwanja sehemu wanapohitaji liwe limekamilika. Sisi tutawapa kila aina ya msaada kwa haraka, nasi wana Dodoma tutoe ushirikiano” ameeleza.
Awali akitoa salamu za Mkoa wa Dodoma, Mkuu wa Mkoa huo Jordan Rugimbana amesema kuwa TEC imebariki wazo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli la kuhamishia Makao Makuu ya nchi mkoani Dodoma.
Aidha Rugimbana amesema kuwa serikali ya mkoa huo itatoa mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa makao makuu hayo mapya ya TEC.
 
Kanisa katoliki mna kesi ya kujibu na misalaba minene shingoni isiyokuwa na manufaa kwa watu! Mko kimya kama mmebwi maji mdomoni! Kila kitu kipo sawa na utawala huu, hamna pa kukemea? mbona JK mlimsakama sana au kwa vile ni dini ingine?
 
Wanachofanya wanamsapoti mtukufu maana akianza kuwataifishia rasilimali zao Pengo ndio atakufa kabisa
Wanampooza mtukufu kimtindo japo ni wenzetu
Tumlinde Pengo kwa pamoja
 
Lazima nao wahamie Dodoma kama serikali inavyotaka kufanya. Haiwezekani TV iwe Dodoma halafu remote control iwe Dar:D.

Pia ahadi ya serikali ya mkoa kutoa mifuko 100 ya saruji ni kutaka kutugombanisha na FaizaFoxy hata tusio wakatoliki:p. Anyways, ndugu zangu maustaadh na maustaadhat msilaze damu, changamkeni muende nao sambamba hawa wenzetu.
 
Lazima nao wahamie Dodoma kama serikali inavyotaka kufanya. Haiwezekani TV iwe Dodoma halafu remote control iwe Dar:D.

Pia ahadi ya serikali ya mkoa kutoa mifuko 100 ya saruji ni kutaka kutugombanisha na FaizaFoxy hata tusio wakatoliki:p. Anyways, ndugu zangu maustaadh na maustaadhat msilaze damu, changamkeni muende nao sambamba hawa wenzetu.
USIWE MWEPESI WA KUSAHAU, CHUO KIKUU CHA WAISLAM MOROGORO MAJENGO YALE YALIKUWA NI YA TANESCO, MALI YA UMMA, RAIS MKAPA AKAWAPA WAISLAM WAFANYE CHUO KIKUU CHAO, MBONA WAKRISTO HATUKUSEMA? NYINYI VIMFUKO VYA SIMENTI MIAMOJA AMBAVYO HATA MILIONI MBILI HAIFIKI TAYARI MSHAANZA KELELE!KWELI MNAROHO MBAYA SANA
 
Kanisa katoliki mna kesi ya kujibu na misalaba minene shingoni isiyokuwa na manufaa kwa watu! Mko kimya kama mmebwi maji mdomoni! Kila kitu kipo sawa na utawala huu, hamna pa kukemea? mbona JK mlimsakama sana au kwa vile ni dini ingine?
Kwani JK alikuwa dini gani?!!
 
Lazima nao wahamie Dodoma kama serikali inavyotaka kufanya. Haiwezekani TV iwe Dodoma halafu remote control iwe Dar:D.

Pia ahadi ya serikali ya mkoa kutoa mifuko 100 ya saruji ni kutaka kutugombanisha na FaizaFoxy hata tusio wakatoliki:p. Anyways, ndugu zangu maustaadh na maustaadhat msilaze damu, changamkeni muende nao sambamba hawa wenzetu.
Kina ff wenyewe wameanza ujenzi wa makao makuu pale kinondoni!
 
Lazima nao wahamie Dodoma kama serikali inavyotaka kufanya. Haiwezekani TV iwe Dodoma halafu remote control iwe Dar:D.

Pia ahadi ya serikali ya mkoa kutoa mifuko 100 ya saruji ni kutaka kutugombanisha na FaizaFoxy hata tusio wakatoliki:p. Anyways, ndugu zangu maustaadh na maustaadhat msilaze damu, changamkeni muende nao sambamba hawa wenzetu.
Ah ah wanatugombanisha na da Fay wakati mifuko100 hata choo haitatosha....

Tec mmeanza siasa aisee
 
Back
Top Bottom