Barabara za Dar ni Machinjio Usiku

Barabara za Dar ni Machinjio Usiku

Mkuu hizi mambo zilinifanya kuanzia 2015 siendagi kwenye harusi hata siku moja na sitoki tena kwenda viwanja.Nilikoswa mara mbili moja sam mujoma road jamaa aliachia altezza yake ile kumkwepa tu mbele nikasikia ajali,pili ilikuwa mataa ya ubungo gari zimeruhusiwa kabisa mtu alitokea huko kimara sijui ilikuwaje ni fuso alivyonikosa Mungu alisaidia.Ajali zinakuwa nyingi hasa morogoro road ,bagamoyo road na mwai kibaki.Kuna haja polisi usiku kupima kilevi
 
niliwahi kuwa mataa ya ubungo kama mara nne au zaidi kuanzia saa saba usiku, yani taa za pale ni kama urembo maana hakuna anae zingatia kabisa.
 
Ukiwa kama mwanadsm na Mtanzania unayependa maslahi ya nchi yako unashauri nini kifanyike kutatua tatizo hili?
Walevi wanaoendesha magari na pikipiki waanze kwa kuwafutia leseni na faini kubwa then akikutwa hana leseni na anaendesha jela slowly but aggressively mayb tutaokoa maisha
Ni kweli. Jumamosi usiku nikiwa zangu mitaa ya sinza kuna jamaa kidogo anitangulize mbele za haki. Jamaa alikuwa na kivitz chake anatokea kule La Chaaz. We jamaa wa kivitz cha kijivu kama unasoma hapa pokea p.u.m.b.a.vu zako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi usiku kunakipindi nilikua nakaa chamanzi mwaka 2014 ulikua usiku kama saa7 hivi naendesha pikipiki narudi hom afu kuna mvua mbele linakuja serela la mchanga barabara inamashimo maeneo ya mfenesini pale lile scania taa moja ndio inawaka tena yakulia nikajua pikipiki inakuja ikawa nakwepa shimo jamaa akaniletea alinipush nangao nikazama kwenye dimbwi exsos ilinichoma derva akasimamisha kuja pole yangu ni matusi yasio kuwa na mwisho akanivuta akaniweka pemben yeye akaondoka mungu amtandike bakora yule derva

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa uchnguzi wangu mdogo barabara za dar ni moja ta sehemu hatari sana hasa nyakati za usiku.

Pengine kwa sababu muda huo kunakua hakuna matrafiki na watu wengi wanakuwa wametoka kupata moja moto ukitembea huwezi kukosa wastani wa ajali 3-5 huko mabarabarani na zingine zinagharimu maisha ya watu kwa sababu watu wanajiachia sana barabaran muda huo. Mwanadsm beware na safari usiku.

Sent using Jamii Forums mobile app
Makonda ana taarifa?
 
Mchana uwa naendesha kama kichaa, Usiku wa manane naendesha kama LENA.
 
Yaani hadi huruma.

Nyingi za ajari hizo husababishwa na shetani pombe.

Anyway, kila mtu atavuna alichopanda.

Acha wafe tu, hakuna namna.

Raha yako is equal to kifo chako
Mkuu hata traffic police anaku charge fine sababu unahatarisha usalama wa wengine,ingekuwa wewe mwenyewe wangekuwa wanapotezea tu.
 
Ukiwa kama mwanadsm na Mtanzania unayependa maslahi ya nchi yako unashauri nini kifanyike kutatua tatizo hili?
Kwakweli ili kuanza kupunguza tatizo,nashauri serikali ifunge bar zote kuanzia ijumaa mpaka jtatu asubuhi. .

Nafikiri tutakuwa tumepunguza tatizo angalau 60%.
 
kweli kabisa aisee....juzi tu nikitoka kimara nampeleka mgonjwa muhimbili, nikiwa hapo kibo nimekuta ajali ya kizembe sana nashukuru Mungu walipona, ni jamaa alikuwa speed kali sana akagonga gari iliyokuwa mbele yake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna jamaa moja lilikuwa limelewa mida ya saa kumi na moja alfajiri siku ya jumamosi halafu linaendesha gari njia nzima kaitawala yeye tulishuka kwenye gari tulimpa vitasa hadi kituo cha polisi pombe zilikata.

Sent using Jamii Forums mobile app
Safi,ila sio vizuri kujichukulia sheria mkononi labda kwa hicho kipondo jamaa roho ingeacha mwili inamaana nyinyi mngeingia matatizoni.

-Ndumilakuwili-
 
Yaani hadi huruma.

Nyingi za ajari hizo husababishwa na shetani pombe.

Anyway, kila mtu atavuna alichopanda.

Acha wafe tu, hakuna namna.

Raha yako is equal to kifo chako
kwani wewe hujawahi tembea usiku, KISHONDO kumbuka kifo hakina mtu, usiwaombee wenzio kifo ndugu yangu, zaidi sana kama ni mwamini Mungu kama mimi, tuombee hizi roho za ulevi, zimeteka sana watu si tu tz duniani kwa ujumla

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom