Juzi usiku nimeona kwenye kituo kimoja cha TV serikali yetu ikitangaza mpango wa kujenga barabara nyingine ya kiwango cha lami itakayokuwa sambamba na ile iliyopo kutoka Segera hadi Tanga, hivyo basi moja itakuwa ina kwenda nyingine inarudi (double roads).
Serikali imesema inafanya hivyo kuepusha ajali nyingi zinazotokea katika barabara hiyo, na mradi huo utaanza hivi karibuni , utafanywa kwa awamu na utagharimu Tshs bilioni nne.
1.Jamani hizo hela kwanini zisiende kujenga barabara huko madongo kwinama ambako hakuna barabara za lami na hizo za vumbi zinahali mbaya kabisa?
2.Eti wanazuia ajali watu wasife!, mbona huko madongo kwinama watu wanakufa kwa kukosa usafiri wa kuwapeleka mahosipitliani kwa sababu barabara hazipitiki! nani atwasemea wananchi hao wanaoishi kama wakimbizi ktk ncnhi yao?
3. Mbona mazao ya wakulima yanaozea mashambani kwakukosa usafiri kutokana na ubovu wa barabara, hili serikali haliihusu?
4. Yaani wanataka kutuambia hiyo barabara ndiyo chanzo kikuu cha vifo vya watanzania kikiasi kwamba ndiyo inastahili kutengewa fungu hilo kubwa wakati kiukweli haihitaji hilo fungu!?
5 Au kwakuwa pia ni njia ya kwenda kwa Mkulu wa kaya!
Jamani mimi naona nchi yetu ni kweli inahitaji miundo mbinu, lakini ni kwenye maeneo yanayo stahili, hii ikoje? ahh......... nchi yetu "inanajisiwa"! na watu wajinga kabisa ambao ni viongozi wetu.
Naomba nianze kwa kusema huu ni mmojawapo wa miradi isiyohitajika na nchi yetu katika kipindi hiki cha maendeleo yetu. Hebu tuchukue ramani ya Tanzania ni tujaribu kuoanisha ukubwa wa nchi na miundombinu hai (current functioning infrastructure)
1. We have a non working central line which should have been the actual national transport backbone.
2. We are told Isaka-Nzega-Dar length of the CL will be upgraded to ISG - nobody seems to know when this will happen and while at it what will befall Nzega-Mwanza, Kigoma-Tabora and Ruvu-Tanga-Arusha pieces.
3. Between Dar and Tanga one can have four modes of transport, that is road, rail, air and sea. Of these the sea and rail routes have the potential to utilise mass transport modes. Instead of a parallell to the current road why not develop these routes which would serve Dar-Bagamoyo-Saadani - Tanga. It would cost us less in the long run.
4. Kwa nini tusiirudishie uhai reli ya Ruvu-Korogwe na matawi yake baada ya Korogwe ili kuhamisha heavy/mass transport kutoka barabarani?
5. Tukirudia ramani ya Tanzania, kwa nini tusiunganishe Mpanda-Sikonge-Nzega au Rungwa-Iringa badala ya kujenga njia ya pili kati ya segera na Tanga?
6. Inaleta hisia kuwa eneo hili lililoko kati ya bahari ya hindi na barabara ya Dar-Chalinze-Segera-Tanga limepewa kipaumbele cha kipekee katika awamu hii ya nne, maana tunasikia bandari/Bagamoyo (sijui bila reli mizigo itatokaje hapo) wakati Tanga (penye reli pana pwaya) is crying out for uplifting, uwanja wa ndege wa kimataifa (kwa ajiri ya Saadani National park ??)
Priorities za nchi yetu ni zipi?
Namna keki ya taifa ilivyogawiwa/inavyoendelea kumegwa kunaweza kukawa ni moja wapo ya vianzo vya kuyumbisha mshikamano wetu kitaifa.