Bara la Afrika na maajabu yake

Bara la Afrika na maajabu yake

Alloyce PR

JF-Expert Member
Joined
Nov 15, 2020
Posts
685
Reaction score
792
MAAJABU YA BARA LA AFRIKA.

"Tajiri yuko tayari kutoa mamilioni kufadhili sherehe yako ya kijinga, lakini ukimwomba TZS 500,000 ya mtaji, anapata 'stroke' ya ghafla.

Ni hapa pekee ambapo unaweza kuwa 'Most Wanted' (unatafutwa sana), si kwa sababu wewe ni jambazi, bali kwa sababu CV zako zimejaa kila ofisi hadi walinzi wanakujua kwa jina. Unasubiri 'fursa' kwa miaka 20 mpaka mvi zinaanza kuandika CV kichwani mwako, huku bado ukiwa umebeba bahasha ya kaki!"— Alloyce, P.R.​
 
MAAJABU YA BARA LA AFRIKA.

"Tajiri yuko tayari kutoa mamilioni kufadhili sherehe yako ya kijinga, lakini ukimwomba TZS 500,000 ya mtaji, anapata 'stroke' ya ghafla.

Ni hapa pekee ambapo unaweza kuwa 'Most Wanted' (unatafutwa sana), si kwa sababu wewe ni jambazi, bali kwa sababu CV zako zimejaa kila ofisi hadi walinzi wanakujua kwa jina. Unasubiri 'fursa' kwa miaka 20 mpaka mvi zinaanza kuandika CV kichwani mwako, huku bado ukiwa umebeba bahasha ya kaki!"— Alloyce, P.R.​
Hauwezi kumpangia mtu namna ya kutumia au kuwekeza pesa zake, kila mtu ana choices zake na ana priorities zake.
Shida/njaa za mtu akabiliane nazo mwenyewe na si kulalamikia watu wengine kisa tu hawamsaidii.
Kutoa msaada/misaada ni hiyari.
 
Ambacho kinanishangaza pia ni pale mgonjwa anaumwa akihitaji matibabu, akishafariki kwa kukosa huduma kwa wakati, ndipo utashangaa watu wanavyo gharamikia msiba, mwingine atasema chakula juu yangu, mwingine vinywaji, mwingine usafiri... kila mmoja akijitia ana uchungu sana na marehemu... mwingine atajaza gari lake mafuta hata ya milioni kisa tu asindikize msiba kijijini kwa marehemu...
 
Ukiwa na idea ya biashara peleka proposal ikiwezekana mfanye wote biashara acha ubinafsi. Wenye pesa wanaombwa na watu kila siku na wewe ukiwa mmoja wao kwahiyo kuwa tofauti kidogo atakuona useful. Pesa inahitaji discipline sio kugawa hovyo hovyo tu
 
Ambacho kinanishangaza pia ni pale mgonjwa anaumwa akihitaji matibabu, akishafariki kwa kukosa huduma kwa wakati, ndipo utashangaa watu wanavyo gharamikia msiba, mwingine atasema chakula juu yangu, mwingine vinywaji, mwingine usafiri... kila mmoja akijitia ana uchungu sana na marehemu... mwingine atajaza gari lake mafuta hata ya milioni kisa tu asindikize msiba kijijini kwa marehemu...
Hii inaumiza sana, ila watu wanaanza kubadilika taratibu. Kuna koo sasa hivi mtu akilazwa ndani ya siku kadhaa wanajichangisha na kutoa msaada kwa mgonjwa.
 
Hii inaumiza sana, ila watu wanaanza kubadilika taratibu. Kuna koo sasa hivi mtu akilazwa ndani ya siku kadhaa wanajichangisha na kutoa msaada kwa mgonjwa.
Kuna mzee alifariki wakati yupo hoi anaumwa familia ilipitia nyakati ngumu kiuchumi mpka pesa ya kuendelea kumtibia ilikosekana maana ugonjwa aliokua nao watu wa bima walikataa kumchangia japo mwanzo walimchangia ila baadae walisitisha

Mzee akarudishwa nyumbani huku familia imeishiwa basi baada ya mda mzee yule akafariki 😢

Ajabu sasa baada ya taarifa za msiba kila mtu alikua shock kumbe mzee ana ndugu wa kumwaga wenye pesa

Kila baada ya mda fulani inatinga gari hapo viroba vya mchele vinashushwa sijui viroba vya sukari mazagazaga kama yote🙌 aisee😢
 
Ukiwa na idea ya biashara peleka proposal ikiwezekana mfanye wote biashara acha ubinafsi. Wenye pesa wanaombwa na watu kila siku na wewe ukiwa mmoja wao kwahiyo kuwa tofauti kidogo atakuona useful. Pesa inahitaji discipline sio kugawa hovyo hovyo tu
Hivi wewe, ulishaandika proposal ukapeleka kwa individual person or company hapa Afrika, alafu wakazingatia na wewe ukanufaika?

Kama wakikupendelea utakuwa mtumwa wake au mtumwa wa Kampuni vinginevyo atachukua atakukatisha tamaa alafu ana implement kimya kimya. Wewe unabaki huna pa kwenda. Hiyo ndio Afrika.
 
Ambacho kinanishangaza pia ni pale mgonjwa anaumwa akihitaji matibabu, akishafariki kwa kukosa huduma kwa wakati, ndipo utashangaa watu wanavyo gharamikia msiba, mwingine atasema chakula juu yangu, mwingine vinywaji, mwingine usafiri... kila mmoja akijitia ana uchungu sana na marehemu... mwingine atajaza gari lake mafuta hata ya milioni kisa tu asindikize msiba kijijini kwa marehemu...
Shida ni ipo hivi mtu akiwa hai anakua na maamuzi ya hiki nataka au hiki sitaki mwingine akiwa hai kuna watu walikua wanataka kumsaidia kwa namna fulani ila yeye kwa sababu ya kuona aibu anasema hapana sitaki kusaidiwa na fulani acheni nitapambana mwenyewe mpaka nitatoboa sasa hapo ndipo shida inapokuja na akishakufa kunakua tena hakuna pingamizi kwa hio waliobaki watafanya bila kusikiliza maamuzi yake kwa sababu maiti hua haiongei na maiti haina ubishi utaipeleka popote hata isipopataka
 
Kuna mzee alifariki wakati yupo hoi anaumwa familia ilipitia nyakati ngumu kiuchumi mpka pesa ya kuendelea kumtibia ilikosekana maana ugonjwa aliokua nao watu wa bima walikataa kumchangia japo mwanzo walimchangia ila baadae walisitisha

Mzee akarudishwa nyumbani huku familia imeishiwa basi baada ya mda mzee yule akafariki

Ajabu sasa baada ya taarifa za msiba kila mtu alikua shock kumbe mzee ana ndugu wa kumwaga wenye pesa

Kila baada ya mda fulani inatinga gari hapo viroba vya mchele vinashushwa sijui viroba vya sukari mazagazaga kama yote aisee
Kuna watu wanajizima data kabisaaa, mtu aumwe ushindwe kumsaidia akiwa anaumwa, anafariki unakuja na gari la hadhi kinoma na vitu kama gunia la mchele/ viroba vya sukari, ivi uyo mtu anapata wapi ujasiri wote huo ilihal unakuta alipewa na taarifa kuna mgonjwa, sijui ni shida ya akili !
 
Kuna watu wanajizima data kabisaaa, mtu aumwe ushindwe kumsaidia akiwa anaumwa, anafariki unakuja na gari la hadhi kinoma na vitu kama gunia la mchele/ viroba vya sukari, ivi uyo mtu anapata wapi ujasiri wote huo ilihal unakuta alipewa na taarifa kuna mgonjwa, sijui ni shida ya akili !
Na wengi ambao wanaleta ubishi huo ni walala hoi. Anategemea afanye kazi alipwe ila anadhulumiwa kila siku na mwenye utajiri.
 
Shida ni ipo hivi mtu akiwa hai anakua na maamuzi ya hiki nataka au hiki sitaki mwingine akiwa hai kuna watu walikua wanataka kumsaidia kwa namna fulani ila yeye kwa sababu ya kuona aibu anasema hapana sitaki kusaidiwa na fulani acheni nitapambana mwenyewe mpaka nitatoboa sasa hapo ndipo shida inapokuja na akishakufa kunakua tena hakuna pingamizi kwa hio waliobaki watafanya bila kusikiliza maamuzi yake kwa sababu maiti hua haiongei na maiti haina ubishi utaipeleka popote hata isipopataka
Kama kuna watu wanapendekeza kumsaidia mtu kwa ajili ya kujiinua kiuchumi ni 1 kati ya 1000 mkuu au isiwepo kabisa Afrika hii.😂😂
 
Kuna watu wanajizima data kabisaaa, mtu aumwe ushindwe kumsaidia akiwa anaumwa, anafariki unakuja na gari la hadhi kinoma na vitu kama gunia la mchele/ viroba vya sukari, ivi uyo mtu anapata wapi ujasiri wote huo ilihal unakuta alipewa na taarifa kuna mgonjwa, sijui ni shida ya akili !
Hata mimi nashindwa kuelewa
Lakini tukisema ni shida ya akili ni uongo uliotukuka mimi naona
Ni ubinafsi
Roho mbaya
Kukosa huruma
Kutokua na upendo
Nashauri kama mtu aliuchuna wakati kama huo wa kuuguza basi hata ikitokea msiba hakuna haja ya mbwembwe zote hizo
 
Toa kabisa tuache kujifariji
Kwa sababu huku africa hakuna kitu kama hicho na ikitokea ujue huyo mtu anajua atanufaika na wewe
Kweli kabisa. Afrika tumekuzwa na ukatili, ulimbukeni, maonyesho ya hovyo, kutaka kundi fulani liabudu wenye nacho. Ukitaka kujiinua unapigwa mawe hadi unabakia kuwa omba-omba. Bara la laana hili.
 
Back
Top Bottom