Bank M-Connecting the dots...

Bank M-Connecting the dots...

Swali ninalojiuliza, hata kama walipewa hizo pesa kifisadi, kwanini hata wasingewekeza kama walivyokubaliana kwenye kupewa hizo pesa? Kwasababu at least tungenufaika kama Taifa na wananchi wangepata ajira nk. Kuna waliodai ni viwanda vya ngozi nk. Ingekuwa kweli uchumi ungeimarika! Na wangewekeza kwa wakulima pia ingewanufaisha wananchi walio wengi ambao ni wakulima wenye vipaji vidogo ama masikini.

Heshima nyingi kwako mkuu!

Ukilielewa jambo vizuri na kulizungumzia, watu watakuelewa tu hata kama litakuwa ni jambo lisiloeleweka kirahisi.
Baada ya zile kelele, JK aliwaambia baadhi yao(hao wa EPA ya pili), kuwa wazirudishe na kwamba wakulima watapewa hizo pesa! Hadi leo hakuna anayejuwa status ya hizo zilizopatikana kwenye hii EPA ya pili. Kumbuka EPA ya kwanza ni hiyo ya miaka ya 90 kabla hawajaanza mpango rasmi wa kuzichota kutoka kwenye akaunti maalum iliyofunguliwa.
 
I think some of these things surface in a good faith. For people to know. For people to think. And come up with solutions that same things will never happen again.
As a nation, if we stay put or stagnant, we could close in our world and forget about it. Life is short and our time is limited.
Our leaders should clean up the mess some few people, for so long have created. We can't attain our proper poaition in the world if the same people who still and work on annihilating the nation still enjoy the status of VIP.
There is a spanish say....al maestro cuchillada...To the master goes the knife....We have the master and he has the knife... lets wait and see how the knife is going to be put on use this time!
 
Kalamu1, ni kweli wengine tunachombeza tu lakini tupo na tunafuatilia sana ila kuna kitu nakuomba usikisahau, brains behind all this plunder ni Watanzania wenzetu. Majina ya Watanzania hao huwezi kuyakuta katika orodha ama ya wamiliki au ya wenye hisa lakini ni wanufaika wakubwa katika biashara hizi kupitia kivuli cha CCM. Baada ya mfumo wa vyama vingi kuanzishwa rasmi 1992 kama kuna kauli ya viongozi wa CCM ambayo haijabadilika ni hii, CCM itatawala milele! Tuendelee kufuatilia...
Sasa nimegunduwa kwanini mwalimu alikubali vyama vingi. Huu uozo ulianzia wakati mwalimu Nyerere akiwa hai, na ni kuanzia miaka ya mwanzo ya tisini ambapo aliwalazimisha ccm. Kiaina aligunduwa ccm wamegeuka mafisi.
 
hahahahaaaaa hapa ndio utajua kwamba tanzania haina idara ya kitengo...........!


lakn pia tujue kwamba hata nyerere alikua na shida nyingi, mojawapo ni kukumbatia wahindi na kuwafukuza wazungu(europeans)!!!


nchi hii ufisadi unaongozwa na hawa tuliotegemea watulindie mali za taifa...... hawa wanaojiita kitengo!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Upo sahihi...

Sayona is a part of The Motisun Group, a privately-owned diversified business conglomerate based in Tanzania with various manufacturing companies in building materials such as steel, roofing products, cement, plastic tanks, pipes, paints etc. It is also present in sectors such as real estate, logistics, food and beverages and hospitality. Our geographic reach encompasses southern, central and eastern Africa and have our own manufacturing facilities located at Tanzania, Mozambique, Zambia and Uganda.

Under the able leadership, guidance and vision of Mr. Subhash M. Patel – Group CMD, Motisun Group has become one of the most successful business brands in Africa. The group’s investment in Africa while fostering economic growth and development provides ample employment opportunities to the local youth. To date, Motisun Group directly and indirectly provides employment to over 10,000 people.
Halafu wakihojiwa wanasema siri ya mafanikio kufanya kazi kwa bidii kumbe wezi.

Matajiri wengi pesa zao wamezipata kwa njia za ki mafianso.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hahahahaaaaa hapa ndio utajua kwamba tanzania haina idara ya kitengo...........!


lakn pia tujue kwamba hata nyerere alikua na shida nyingi, mojawapo ni kukumbatia wahindi na kuwafukuza wazungu(europeans)!!!


nchi hii ufisadi unaongozwa na hawa tuliotegemea watulindie mali za taifa...... hawa wanaojiita kitengo!

Sent using Jamii Forums mobile app
UPO ila hawawezi kufanya lolote mpaka wampe taarifa SPONSOR (Rais) ndiye aamue nini kifanyike. Katiba ndivyo inavyoelekeza hata ile sheria iliyounda TISS ya mwaka 1996 kipindi cha Mkapa. Marais wenyewe sasa!!!
 
Hili suala la Bank M limedhihirisha udhaifu mkubwa sana wa serikali ya ccm ambao sidhani kama mtu mmoja anaweza kuufuta zaidi ya usanii tu inapotokea wanagombana wenyewe kwa wenyewe!

Hii benki M pamoja na kuhusiana na ufisadi wa EPA, pia imekuwa “ikibebwa” sana na serikali za ccm. Na hivyo kutumia jasho letu sisi walipa kodi! Hata hizo pesa za ufisadi ziliondolewa huko ndo maana! Na mambo mengi sana yamefanyika ili kuificha hiyo connection toka kipindi kile. Kwa mfano Sasa hivi hao jamaa wanaendelea na ma biashara yao makubwa, lakini ukijaribu kutafuta connection yao na EPA au hata bank M, wamefuta! Hata ile mijadala iliyokuwa ikionyesha hizo connections hadi na Mkapa siioni! Hata habari zilizokuwa zikizungumzia hilo! Thread za Jf za namna hiyo, zimegeuka kuwa pdf files zisizo na kitu. Links zimegeuka “a bridge to nowhere”

Like “poof” they disappeared in thin air!
kwamba hata thread za hapa JF wamefuta???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijui wangapi wanakumbuka wakati Ikulu yetu ilipogeuka na kuwa kama pango la walanguzi, naam waliokuwa wanunuzi wa madeni walikuwa kama walanguzi wengine tu.

Ahsante Mag3, kwa video hiyo.

Mjadala huu umetoa fursa kama mfano mzuri kwa yeyote anayetaka kujua hali halisi tuliyoifikia kama taifa.
Ni kiasi cha kusoma tu kwa utulivu na kuelewa yaliyosemwa humu.

Sijaona sehemu yoyote ndani ya mjadala huu hoja yenye utetezi juu ya yaliyofanyika, kwamba yalifanywa kwa manufaa ya taifa.
 
jmushi1, yawezekana wapo wanaokubaliana na mimi kuwa adui mkubwa wa taifa hili ni CCM; niliamini hivyo, naamini hivyo na nitaendelea kuamini hivyo. Sijui tuko wangapi tulioikataa CCM toka kuasisiwa kwake mwaka 1977 lakini mwasisi wa CCM, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere baada ya kutambua kosa lake la kuanzisha hili zimwi alisikitika sana. Bahati mbaya ni kwamba wakati huu ukweli unajiweka wazi kwake, hakupata nafasi ya kuongoza mapambano dhidi ya hilo zimwi; zimwi lilimwahi akaaga dunia akihuzunika na kulia kwa uchungu.

Hakuna muujiza utaweza kufanyika kuliokoa hili taifa ikiwa bado iko mikononi mwa CCM na ili Tanzania ijikwamue kutoka lindi la umasikini wa kujitakia, CCM lazima ipigwe vita na kushindwa. Bila hivyo ni kujidanganya. Nchi hii ilijaaliwa kila aina ya neema na hakuna nchi ndani ya bara hili lililokuwa na utajiri wa asili kama Tanzania lakini hivyo hivyo hakuna nchi barani Afrika linaloongozwa na chama kama CCM. Wana CCM wa leo wamezaliwa humo humo, wakalelewa humo humo, wakakulia humo humo, wakakomaa na kufuzu humo humo;

Ukweli mchungu...kila awamu litakuwa ovu kuliko lililotangulia.
umeongea kwa uchungu sana mkuu Mag3...........


mimi siachi kumlaumu mzee nyerere kwa haya, alikua na uwezo kabisa wa kuua ccm lkn kwann alishindwa??


kwann aliacha katiba ya chama ndio iongoze nchi? maana katiba yetu ni katiba ya ccm ile wala sio ya taifa.........


yule mzee sitaki hata kumkumbuka kwa mazuri yake,,,,, na hii ccm tutakufa tutaiacha!..... nchi haina usalama kabisa kisa ccm

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Amepewa tenda na serikali hii ya jiwe?
Ukishangaa ya Musa, je ya Farao? Juzi tumemuona RA kwenye sherehe ya kumpokea Lowassa siyo? KAGODA, iliyochotewa mabilioni kwenye EPA mwezi Octoba mwaka 2005, iliasisiwa na RA/Manji lakini wanufaika walikuwa ni pamoja na CCM. KAGODA na CCM walikuwa ni kama pete na kidole.

CCM haijawahi kuadhibiwa pamoja na baraka na ushiriki wake katika ufisadi. Ufisadi mkubwa wa CCM kama chama ni ule wa kuwadhulumu Watanzania mali zao kama majengo, makampuni, shule, viwanja vya michezo na mengine mengi tu. Amini usiamini adui nambari wani wa taifa hili ni CCM.
 
Back
Top Bottom