Perfect.
Kwa hiyo Chavda wetu alinunua deni kwa 2.5 millioni, jamaa akaenda kuvuna mabilioni toka kwa mdaiwa ambaye ni serikali yetu!
Nimekupata barabara na kila kitu sasa kimefunguka vyema.
Haya tuendelee!
Ndiyo mkuu. Walikuwa wamejipanga kama mafisi waliokamata mzoga.
Kwa Mfano Chavda baada ya kununua hilo deni kwa 2.5m Tzs, alipewa mkopo wa Tzs 661m, ili kuendeleza mashamba ya mkonge ambapo yangeliingizia Taifa pesa za kigeni(deni la Taifa hulipwa kwa fedha za kigeni).
Lakini yeye hizo pesa, akawagawia ama “kuwalipa” Subash na Patel bila hata ya kuonyesha malipo hayo yalikuwa ya minajili gani ama kazi gani!
Wenzake nao walipochukuwa mikopo kutoka kwenye kampuni zao, walifanya hivyo hivyo kugawana, huku vigezo vya kukopa pesa hizo za wavuja jasho vikiwa ni kuanzisha biashara Alan shughuli zitakazolipatia Taifa pesa za kigeni, kutengeneza ajira na kusaidia uchumi wa nchi kwa ujumla.
Hata Kagoda ya RA yenyewe ilichukuwa kwa sababu za kilimo!
Swali ninalojiuliza, hata kama walipewa hizo pesa kifisadi, kwanini hata wasingewekeza kama walivyokubaliana kwenye kupewa hizo pesa? Kwasababu at least tungenufaika kama Taifa na wananchi wangepata ajira nk. Kuna waliodai ni viwanda vya ngozi nk. Ingekuwa kweli uchumi ungeimarika! Na wangewekeza kwa wakulima pia ingewanufaisha wananchi walio wengi ambao ni wakulima wenye vipaji vidogo ama masikini.
Hizo pesa mpango mzima waliamuwa kuziweka kwenye akaunti ya madeni ya nje ama EPA! Nadhani waliona huko hazitakuwa monitored! Maana kama ni za kulipa madeni si ni kama zimeshatoka? Kwahiyo wakazitafuna badala ya kuziwekeza ili kulisaidia taifa kwenye uchumi na ulipaji wa madeni ya nje!
Baada ya zile kelele, JK aliwaambia baadhi yao(hao wa EPA ya pili), kuwa wazirudishe na kwamba wakulima watapewa hizo pesa! Hadi leo hakuna anayejuwa status ya hizo zilizopatikana kwenye hii EPA ya pili. Kumbuka EPA ya kwanza ni hiyo ya miaka ya 90 kabla hawajaanza mpango rasmi wa kuzichota kutoka kwenye akaunti maalum iliyofunguliwa.
Kitendo walichokifanya, ni kutuongezea urefu wa shimo... down deep in a rabbit hole!