Bango la Dr Slaa Lazua Mgogoro UKAWA; CUF Watoa Onyo!

HAMY-D

JF-Expert Member
Sep 18, 2011
7,149
3,817
Wana Ukumbi,

Kurejea kwa Dr Slaa kutoka Marekani lilikuwa ni tukio la furaha kwa wapenzi wa CHADEMA na katika kuonyesha hisia za furaha yao baadhi ya mashabiki wameenda mbali zaidi na kuivuka mipaka!

Imeelezwa na mmoja wa viongozi waandamizi wa CUF kuwa, wameshuhudia mabango yakisomeka "Dr Slaa ndiye rais wa awamu ya 5 wa Watanzania" siku ya mapokezi ya Dr Slaa katika viwanja vya mwalimu JKN!

Mtoa habari aliongeza, "Kwa kuzingatia makubaliano tuliojiwekea UKAWA, mabango yaliyokuwa na maneno hayo ni mkakati wa CHADEMA katika kushinikiza Dr Slaa asimamishwe kwenye nafasi ya mgombea urais kupitia UKAWA, kinyume kabisa na tulichokubaliana kwenye kikao."

Kwa mujibu wa makubaliano ya UKAWA yaliyofanyika Zanzibar ni kwamba, mjadala kuhusu nani atasimama katika nafasi ya urais usogezwe mbele ili kutoa muda kwa vyama washiriki kutathmini nani anafaa kuwa mgombea wa UKAWA.

Viongozi hao wa CUF (Zanzibar) wameandika barua makao makuu ya CUF kumtaka mwenyekiti taifa kuwaonya CHADEMA kuhusu kuheshimu na kulinda makubaliano ya vikao ili kuendeleza umoja wao huo wa UKAWA pasipo migogoro isiyo ya lazima.

Source: Zanzibar leo

Bango lililozua mgogoro ni hili hapa chini:


View attachment 246513
 
Mwska huu mtaweweseka sana, kwani UKAWA, Wana wanyima raha, kila siku ni kutafuta chokochoko za kuwagombanisha, ila wao wameshaligundua hilo. Hamtafanikiwa kuwagombanisha
 
Wenye akili tulishachungulia nakubaini kuwa, hakuna lolote pale UKAWA zaid ya madaraka tu.

Ajenda zao ktk kumkomboa Mtanzania ni ndogo sana (au hakuna kabisa). ni muendelezo wa Ngonjera zilezile.

Tunataka Rais mwenye maadili na Roho safi(ambaye hata kwa macho ya nyama tunasadiki hivyo).

Kwa UKAWA sijaona kimsingi. hata wale niliowadhania, wamepigwa kikumbo(mfano Mbatia).

Kwa CCM, i'm sure, #Pinda deserves it.

Let the movie get on.

Mungu Ibariki Tanzania.
Amen!
 
Wenye akili tulishachungulia nakubaini kuwa, hakuna lolote pale UKAWA zaid ya madaraka tu.

Ajenda zao ktk kumkomboa Mtanzania ni ndogo sana (au hakuna kabisa). ni muendelezo wa Ngonjera zilezile.

Tunataka Rais mwenye maadili na Roho safi(ambaye hata kwa macho ya nyama tunasadiki hivyo).

Kwa UKAWA sijaona kimsingi. hata wale niliowadhania, wamepigwa kikumbo(mfano Mbatia).

Kwa CCM, i'm sure, #Pinda deserves it.

Let the movie get on.

Mungu Ibariki Tanzania.
Amen!

Kama hizi zako pia zinaitwa akili basi sishangai kwa nini ndani ya chama kikubwa kama CCM hamjamteua mgombea Urais takribani miezi 4 kabla ya uchaguzi na wote mnaona ni jambo jema tu mnachekelea!!

Tatizo ni nini?? Mnaogopa kitu gani nyie CCM...?? Mbona kila siku mnajinasibu kuwa nyie ni chama kubwa nchini yenye watu kibao wenye sifa za kukubalika kushika nafasi yoyote nchini...Imekuaje tena??

Si ajabu mnavyovizia vizia hivi kutaja wagombea wenu vile vile midahalo ya wazi pia mtaikacha kama kawaida yenu...

Bora hata UKAWA wanao watu ambao wako tayari... nyie mnasubiri nini...Maboresho ya daftari wapiga kura, ripoti ya ZZK/ACT Wazalendo...au nini??

Mkae mkijua kuwa mwaka 2015 wananchi hawapo tayari kubambikiziwa au kuuziwa Rais kwenye gunia...!!
 
Wenye akili tulishachungulia nakubaini kuwa, hakuna lolote pale UKAWA zaid ya madaraka tu.

Ajenda zao ktk kumkomboa Mtanzania ni ndogo sana (au hakuna kabisa). ni muendelezo wa Ngonjera zilezile.

Tunataka Rais mwenye maadili na Roho safi(ambaye hata kwa macho ya nyama tunasadiki hivyo).

Kwa UKAWA sijaona kimsingi. hata wale niliowadhania, wamepigwa kikumbo(mfano Mbatia).

Kwa CCM, i'm sure, #Pinda deserves it.

Let the movie get on.

Mungu Ibariki Tanzania.
Amen!
Hatutaki rais dhaifu kama pinda ha hatopata kura asilani.
 
Bila ushabiki wowote hakuna uhusiano wa Ukawa na wapenzi wa slaa kwenda na bango uwanja wa ndege kumpokea. Bango hilo hakuna tofauti na watu hao kubeba maua au ishara nyingine yoyote kwanini wako pale. Kufanya kama ni suala kubwa kwenye umoja wa UKAWA na kukubalika kujadiliwa hata na viongozi wake kuna leta shaka kaka ubora wa umoja huo kwa maana inaonekana kukosa uimara. Haya mabango maandiko tutayaona sana, kwa CUF, NCCR, CDM etc na kama tutachukulia kuwa ni kete kwa mwingine basi ni bora kuvunja umoja huo na kila chama kufanya mambo yake au vyama ambavyo vinaamini katika umoja kuendelea na vile vinavyoota URASI kila sekunde kuendelea na ndoto zao. Tafsiri nyingine ni kuwa huenda ikawa tuna wanachama ambao hawakuelewa msingi hasa-philosophy- ya kuanzishwa kwa umoja huo. Vyama vielimisha wanachama wao kujitabua na kuangalia masuala ya msingi yatakayoonyesha ukomavu wao. vinginevyo hata sisi wananchi hatuwezi kuwaamini.
 
Wananchi wakiandika ujumbe kwenye bango ni msimamo wao na sio lazima uwe ni msimamo wa CDM. Na kwa kweli ni vema CUF wakakubali mapema kwamba Slaa ndiye mgombea atakayeweza kushinda Urais. Hilo wanalifahamu. Mara ya mwisho ilibidi kiongozi wa CUF ashirikiane na CCM ili kuhujumu kura za Slaa. Alikiri msikitini kwamba alifanya hivyo.
 
Nimeisoma habari kwa umakini sana,nikaangalia bango kwa makini sana.nikagundua wanaolalamika sio CUF wala ukawa!Tena nashauri kila chama ktk ukawa kionyeshe hisia sana juu ya mgombea wao,halafu badae wanachagua mtu mmoja tu,itakaa vizuri sana.
 
Haa haa hivi kuönyesha hisia ni dhambi? Kwa maoni yangu binafsi, kwa upande wa ukawa, mgombea urais wa muungano ni dr. Slaa na upande wa zanzibar ni maalim seif. Full stop zingine hizo ni mbwembwe.
 
Kwa kuangalia nyuzi zake, aliyeleta mada hii, ndiye pia ripota mkubwa wa mikutano na harakati za ACT-WAZALENDO. Sura halisi ya hawa jamaa, inazidi sasa kujulikana!!!! AIBUUUUUUUU!!!!!!!
 
Wenye akili tulishachungulia nakubaini kuwa, hakuna lolote pale UKAWA zaid ya madaraka tu.

Ajenda zao ktk kumkomboa Mtanzania ni ndogo sana (au hakuna kabisa). ni muendelezo wa Ngonjera zilezile.

Tunataka Rais mwenye maadili na Roho safi(ambaye hata kwa macho ya nyama tunasadiki hivyo).

Kwa UKAWA sijaona kimsingi. hata wale niliowadhania, wamepigwa kikumbo(mfano Mbatia).

Kwa CCM, i'm sure, #Pinda deserves it.

Let the movie get on.

Mungu Ibariki Tanzania.
Amen!

acha ujinga Pinda yupi? Waziri mkuu analia baada ya albino mmoja kukatwa mkono waka anauwezo wa kutoa amri walifanya kitendo wakafahamika,mbona wauaji wa RPC Mwanza tuliambiwa wanematwa,kwa kulia lia huko je tukivamiwa Rwanda itakuwaje? Wanasiasa wenzie wapigwe tu
 
Vile tumia akili kuwaza hao walioandika ni wapenzi wa chadema na sio wasemaji wa chedema, na mabando ya lowassa utasema ni ccm wamesema? Wakati nape kila leo analalama, make more sense than stupidy mistake
 
Slaa Kuitwa Raisi ni Jina la toka la Kawaida tulilombandika toka alipogombea 2010... Tumekuwa tukimuita na Majina mengi yenye vinasaba(Material) ya URAISI ambavyo Mungu amemjaalia.. Mfano Raisi wa Mioyo yetu, Raisi wa watanzania, Raisi ajaye n. k, Sioni la Ajabu Hapo.....

Haya nenda Lumumba na wewe ukachukue Msimbazi Wako, maana nyie Partner wao mnaojiita ACT Wazahendo wa CCM mkiandika kuhusu CHADEMA Posho yenu ni Kubwa "MSIMBAZI"
 
Hujasikia kwamba nccr tayari wameshatoa fomu ya mgombea urais? Huo umbeya wenu Wa kichonganishi uishie huko huko Lumumba pambaff!!
 
Mwisho wa Siku vijana wa Bavicha na CUF wataanza kutukanana hadharani Kwani mwisho wa hii ndoa ni matusi.

Hawa Si wamoja hata kidogo kila mmoja anajiona bora Zaidi Ya mwenzake, na kila mmoja hupanga mbinu chafu Za kuchafuana ndani kwa ndani

Lakini mwisho wa yote haya yakitokea ni CCM, hata mvua isiponyesha ni CCM, hata ugomvi Wako na mkeo ni CCM lakini kwenye amani CCM haipo......
 
Babu kachoka lakini, any way mwache ajaribu bahati yake Ya mwisho ambayo pia ataangukia pua na 2020 atakuwa katimiza miaka 98.
Job K
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom