Bango kubwa la Puttin lawekwa New York' Marekani

Bango kubwa la Puttin lawekwa New York' Marekani

DesertStorm

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2015
Posts
3,315
Reaction score
2,739
BANGO KUBWA LA PUTIN LAWEKWA NEW YORK


_91552522_hi035732960.jpg


Polisi walifika na kuliondoa muda mfupi baada ya picha za bango hilo kuanza kusambazwa sana katika mitandao ya kijamii.

Bango kubwa lenye picha ya Rais wa Urusi Vladimir Putin, lililoandikwa "mweneza amani", limewekwa na watu wasiojulikana katika daraja la Manhattan jijini New York.

Bango hilo lililowekwa Alhamisi linamuonesha kiongozi huyo wa Urusi akiwa mbele ya bendera ya Urusi.

Daraja hilo maruufu huunganisha Manhattan na Brooklyn.
Polisi walifika na kuliondoa muda mfupi baada ya picha za bango hilo kuanza kusambazwa sana katika mitandao ya kijamii.
_91552884_hi035732953.jpg


Kufikia sasa hakuna aliyekamatwa.
Polisi wanafanya uchunguzi.
 
Kwa marekani huu ndio uhaini wenyewe......

Watakamatwa mapema sana Kwa kutumia mfumo wa CCTV.....

Wajiandae kwenda uamishoni kama Edward Sinoden
 
Tatizo anakubalika kwa wale wenye utimamu wa akili kuliko wanaoamini Propaganda za chochoko ya amani ya dunia
MKUU NIPE ELIMU BASI HAYA MA MISSILE YANAVYOKUA CONTOLED!

Unakuta mzee putin kakaa zake pale moscow anabinya button tuu s-300v inafanya maangamizi pentagon.
 
Kwani kuna tatizo gani hilo bango kuwekwa hapo? Au halikulipiwa ushuru.



Hilo bango ni Shule tosha mno kwa mataifa ya magharibi hususan marekani na mwenzake. PiaWapo wamarekani ambao wameshachoshwa na huu utawala wa kibabe unaovuruga amani na kusababisha machafuko makubwa ktk nchi za watu hapa duniani hususan Middle East, haikutosha hiyo wakaunda tena kikundi cha isis na kupelekea amani kutoweka, innocent people kuuawa na wengine kuyakimbia makazi yao.
 
Kwa marekani huu ndio uhaini wenyewe......

Watakamatwa mapema sana Kwa kutumia mfumo wa CCTV.....

Wajiandae kwenda uamishoni kama Edward Sinoden
Halafu wakikamatwa watashitakiwa kwa kosa gani?!,
 
Back
Top Bottom