Samahani unaishi maisha ya kawaida? mfano kuoa, kufanya kazi na kutegemewa na ndugu au jamii inayokuzunguka?
Bila ya samahani, yaani kiroho safi.
Ndio, naishi Maisha ya kawaida na nina shughuli zangu binafsi ninazoziendesha, au kwa lugha nyingine naweza sema nimejiajiri.
Kabisa wala hujakosea, Majukumu yapo/ninayo na nategemewa kama ujuavyo Familia zetu za kuunga unga, Maisha yetu ya Kibongo, hayo ni mambo ya kawaida au naweza sema ya Ulazima. Nisingeweza kufunguka kiundani hapa kwenye Masuala ya Kifamilia, ila kwasababu umeniuliza, basi sioni sababu ya kutokufunguka pengine labda unataka kujua upande wa Pili wa Shilingi kwa kuwa wengi msioijua Bangi mnaamini/mnadhani Mtu anaevuta Bangi ni kama Mtu ambae amepoteza kimaisha, au ni yule Mtu ambae hana nyuma wala mbele, au ni yule aliepoteza mwelekeo ni tofauti sana mnavyoichukulia Bangi na uhalisia wake.
Naendelea hapa kwenye Familia, ambayo ni masuala binafsi nisingefunguka kwa undani ila kwa kunyoosha mistari inabidi niweke mambo sawa.
Mimi sitokei Familia ya Kitajiri, natokea Familia ya kawaida sana ila nashukuru Mungu kwa Neema zake hatujawahi kutia huruma, wala hatujawahi kulala njaa. Nashukuru Wazazi wangu wote wawili wapo hai na nawaonea sana wivu kwa jinsi wanavyoyaendesha Maisha yao, yaani tokea walipofunga Pingu za Maisha kabla ya Mimi HARUFU kuzaliwa, mpaka mie HARUFU namwagika hapa Ulimwenguni, mpaka napata akili, hawa Viumbe wako pamoja mpaka hivi sasa tunapoongea, pamoja ya kuwa Mshua wangu Kitambo hiyo alikuwa Mtu wa kutoka Nje (Majuu) mara kwa mara tofauti na hivi sasa Mshua amekuwa Mtu wa Kulikita Bongo, pamoja na safari za Nje za Mshua mara kwa mara lakini hiyo haikuwa sababu ya wale Waja kutengana. Ni raha ilioje.
Naendelea, Mimi ningekuwa Mtu wa kujibweteka kwa jinsi wale Wazazi wangu walivyo, nna hakika mpaka hii leo ningekuwa naegemea egemea kwao. Kama ujuavyo sisi Wabongo Nyumbani kuwepo japo na unafuu kidogo tu basi kinachofuata ni kuridhika, Lakini kwa upande wangu Mimi sikutaka Maisha ya kutia huruma na kuanza kuegemea Wazazi.
Sasa hapa ndio nataka nifanye hitimisho la kutegemewa, ni hivi:-
Nimejitolea kumlea Mdogo wangu wa mwisho, pamoja ya kuwa Wazazi wangu wasingeshindwa kumlea. Lakini niliwaomba wanipe Jukumu hilo, na lengo langu ni kwa ajili ya Changamoto tu. Na nikaawaambia iwapo nitashindwa basi Mtaendelea nae, tukakubaliana.
Basi huwezi amini tokea nichukue hilo Jukumu, hakuna kilichowahi kuharibika. Haina maana naishi nae mimi, hapana. Anaishi Nyumbani na Wazazi wetu, ila mambo yote kuhusu yeye ni juu yangu mimi, kuanzia Mavazi yake, Masomo, N.K. Gharama ni juu yangu mimi.
Nimejitahidi niandike kiufupi lakini imeshindikana, na kila nilivyojaribu kufupisha imeshindikana hali kadhalika, pamoja nimejitahidi kufanya utulivu na kuutumia Muda ipasavyo lakini imeshindikana.
Nadhani sitokuchosha.
Na kwa kumalizia sasa hivi simo kwenye Maisha ya Ndoa, Niliwahi kuwemo kwenye Maisha ya Ndoa kwa kipindi cha Miaka Minne tu, yaani 2008-2012. Kwa bahati mbaya haikuwa Zali