Bandari ya Dar es Salaam yakabidhiwa eneo la Kurasini

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,305
24,200
13 December 2023
Dar es Salaam, Tanzania

SERIKALI YAKABIDHI ENEO LA KURASINI JIJINI DAR ES SALAAM KWA BANDARI YA DAR ES SALAAM BAADA YA MRADI WA EPZA KUFELI


Eneo lililokuwa maalum kwa uwekezaji chini ya Mamlaka ya Ukanda Maalum wa Uwekezaji (EPZA) lakabidhiwa kwa bandari ya Dar es Salaam iliyo chini Mamlaka ya Bandari Tanzania TPA . Eneo hili mwanzo lilitwaliwa na serikali kuwa eneo maalum la uwekezaji wa viwanda

HISTORIA YA ENEO LA EPZA

24 September 2021​

Prof. Kitila akagua eneo la Uwekezaji Kurasini, EPZA yalikabidhi kwa SUMA JKT na BICO kuanza Ujenzi



View: https://m.youtube.com/watch?v=26a9s9_qaog

Waziri Prof. Kitila Mkumbo anaelezea makubwa kama maji, umeme na barabara ili kubadilisha eneo hili kuwa la mfano kimataifa kuwa Kurasini Logistic Centre na Industrial Park kuwa mtaa wa viwanda Business Centre Kurasini.

Bidhaa za kieletroniki zitaunganishwa pia soko maalum la mazao ya Korosho, Chai na mbogamboga ili kuingia katika mfumo wa soko huru la bidhaa Afrika AfCFTA
Mwaka 2009 China na Afrika nchi 4 za kujengwa kituo cha Kimataifa cha Biashara na Logistics, Tanzania ilipochaguliwa ikaamua kutwaa eneo na kuwalipa wananchi kiasi cha bilioni 101 shilingi za kiTanzania kama fidia ya kuhama Kurasini.

2019 18 December

View: https://m.youtube.com/watch?v=7ga5SiU6fPY
WAZIRI INNOCENT BASHUGWA NA EPZA WAJIPANGA KWENDA SAMBAMBA NA RAIS MAGUFULI

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Innocent Bashungwa ameongoza kikao cha bodi ya Wakurugenzi wa Kanda maalumu ya uwekezaji EPZA (Export Processing Zones Authority).Mhe. Innocent Bashungwa ndie Mwenyekiti wa bodi hiyo ya Wakurugenzi.Kikao hicho kimekuwa na malengo ya kuangalia dira na mwelekeo wa EPZA katika kutekeleza mkakati wa Serikali hususani hotuba ya Mheshimiwa Rais Magufuli aliyoitoa tarehe 12/12/2019 kwenye mkutano wa halmashauri kuu ya CCM Taifa ambayo ilieleza mkakati wa nchi wa kujenga uchumi wa kati kupitia serikali ya viwanda kwa mwaka 2020 mpaka 2030.Pia bodi imejadili kuhusu ujenzi wa kituo cha kuchakata mazao katika kata ya Kurasini Dar es saalam. Mradi huo utachukua eneo lenye ukubwa wa ekari 61.87 ambalo litahusisha mitaa ya shimo la udongo, Mvinjeni na KiunganiPia bodi hiyo imeunda timu maalum ya kuandaa mkakati mpya ambao utaleta mabadiliko na sura mpya ya EPZA na kuangalia mikakati ya hotuba za Rais na mikakati ya SADC na Viwanda vidogo, vya kati na vikubwa ili kujenga nchi yenye uchumi wa kati kupitia viwanda

MWAKA 2014
Awali mwaka 2014 serikali ya China kupitia kampuni ya Yiwu Pan-Africa International Investment Corporation na serikali ya Tanzania iliyowakilishwa na EPZA ziliingia mkataba kuanziasha mradi wa eneo maalum la uwekezaji.


Ujenzi wa mradi huo ulitazamiwa utagharimu Dola za Marekani milioni 400 ambazo ni sawa na Sh. bilioni 660 ambazo zitagharimiwa na serikali ya China.

Tanzania kwa upande wake ilitoa ardhi na kulipa fidia kwa wakazi wa maeneo hayo ambayo yana ukubwa wa ekari 60.4 yaliyotengwa katika kata ya Kurasini ikihusisha mitaa ya Shimo la Udongo, Mivinjeni na Kiungani.

“Tunatarajia kituo hicho kuwa kikubwa Afrika ya Mashariki na kati, ninafuraha kuwajulisha kuwa fedha iliyokuwa imeahidiwa kwenye bajeti, tayari imewasilishwa katika mamlaka ya EPZA kwa ajili ya malipo,” alisema Dk. Kigoda mwaka .

Alisema katika mwaka wa fedha uliopita, serikali ililipa fidia kwa awamu mbili jumla ya Sh. bilioni 45, ambapo awamu ya kwanza zililipwa Sh. bilioni 25 na awamu ya pili zililipwa Sh. bilioni 20.

Alisema mradi huo utaleta manufaa katika nchi kwa kupata bidhaa mbalimbali kutoka China, kuongeza pato la nchi kupitia kodi, kupanua miundombinu katika eneo la mradi, pamoja na kujenga viwanda vya kuongeza thamani ya mazao hususan mazao ya kilimo na madini.“Mradi huu utatengeneza ajira za moja kwa moja takriban 25, 000,” alisema.

Waziri Kigoda aliongeza kuwa, kupatikana kwa fedha hizo kumetoa mwanya wa kukamilisha mradi huo utakaofanya eneo hilo kuwa kitovu kikubwa cha viwanda na biashara katika eneo la ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maeneo Huru ya Uwekezaji (EPZA), kwa wakati huo Bw. Adelhelm Meru, alisema tayari taratibu za malipo zimeshaanza na matarajio ni kuwa baada ya wiki mbili au tatu zoezi hilo litaanza.

Alisema ujenzi wa kituo unaweza kuanza baada ya miezi miwili baada ya zoezi la malipo kukamilika na baada ya taratibu muhimu nyingine kukamilika.
Naye Naibu Waziri, Wizara ya Viwanda na Biashara, Janet Mbene, aliwatoa wasiwasi Watanzania na kusema kuwa kituo hicho kitakuwa na manufaa makubwa kwa nchi.Jumla ya wananchi 1020 wanatakiwa kuhama katika eneo hilo la mradi.
Chanzo: NIPASHE.
 
Government transfers Kurasini land to Dar port

GOVERNMENT TRANSFERS KURASINI LAND TO DAR ES SALAAM PORT

2 days ago — 12 December 2023

Dar es Salaam. A vast tract of idle land in Kurasini, Dar es Salaam, will now be used by Dar es Salaam Port as a green channel, the government said on Monday.The land was initially meant for the proposed Kurasini Trade and Logistics Centre.“We will now use that particular area as a green channel,” Transport permanent secretary Godius Kahyarara told The Citizen.A green channel refers to a customs area at an airport or port that has been set aside for arriving passengers who have no goods to declare. It can also be used to house perishable goods meant for export.

A total of 60 hectares in Kurasini and parts of Shimo la Udongo, Mivinjeni and Kiungani areas were originally meant for the proposed Kurasini Trade and Logistics Centre.In line with the Dubai model, the area was to have been used as a storage facility for Chinese manufacturers.The facility would have enabled traders from within Tanzania and neighbouring countries to buy a wide variety of goods manufactured in China at a one-stop centre without having to travel to China.The government compensated those who had to move out to pave the way for the project, but the focus changed as soon as the exercise was completed.

With domestic industrialisation gaining momentum, the project began drawing criticism.Some critics were of the view that promoting imports from China was contrary to Tanzania’s development vision which, among other goals, seeks to promote home-grown industries.The government subsequently cancelled the project and converted the area into an extension of Dar es Salaam Port.Industry and Trade deputy minister Exaud Kigahe told The Citizen on Monday that the area was still government property and had since been transferred to the Transport ministry.

New trade and logistics centres are being set up in Kwala, Coast Region, and Ubungo in Dar es Salaam.And, according to Prof Kahyarara, the government shelved the Kurasini Trade and Logistics Centre project to help reduce congestion at Dar es Salaam Port.“A new project is in the pipeline and its execution will start soon. The goal is to ensure that the area becomes a green channel for agricultural products, especially perishable goods, before they are exported,” he said.

Prof Kyaharara added that the government had received many requests from people who were interested in setting up crop storage facilities. He urged Tanzanian businesspeople to grab the available opportunities and grow their businesses. Several analysts who spoke to The Citizen on Monday said transferring the area to Dar es Salaam Port was the right decision.An economist from the University of Dar es Salaam, Dr Wilhelm Ngasamiaku, said by handing over the area to Dar es Salaam Port, the government had shown its seriousness in efforts to improve the port’s efficiency.

This, he added, was because the port needed more space for warehouses and other storage facilities and the investors who were to have been involved in the Kurasini Trade and Logistics Centre project could be given suitable locations elsewhere.“I can say that the area is suitable for the port, but not for industry. It will help the port to breathe and attract more investors. This will go a long way in further promoting economic growth,” Dr Ngasamiaku said.

Mr Kigahe told The Citizen in January that the Kurasini Trade and Logistics Centre project had not been abandoned, but moved to the Kwala dry port in Kibaha, Coast Region, to give Dar es Salaam Port more breathing space.He said upon its completed, the project, which is now known as Kwala Industrial Parks, will draw more than 300 industrial firms.

Mr Kigahe added that thousands of direct and indirect jobs would be created in the process.Implementation of the Kwala project began last year and the facility is expected to become operational next year. Mr Kigahe said the government was putting in place the relevant infrastructure at Kwala as part of efforts to foster a favourable business environment in the area
 
DP World na wawekezaji wengine kuanzia gati 8 -11 katika bandari ya Dar es Salaam kiulaini wanaanza kuona fursa zaidi

08 December 2023
Arusha, Tanzania

16th Joint Transport Sector Review Meeting

Hayo yamejiri leo katika mkutano wa 16 unaohusisha wadau wa sekta ya Uchukuzi ukiotayarishwa kwa pamoja baina ya Wizara ya Uchukuzi kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais Tawala wa Mikoa na serikali za mitaa ( TAMISEMI / PO-RALG )

PROF. MBARAWA : MWEKEZAJI MPYA KUWEKEZA BANDARI YA DSM, SIO DP WORLD NI KAMPUNI NYINGINE

View: https://m.youtube.com/watch?v=8X9S3V7uREU
Ambapo waziri wa uchukuzi amebainisha kuwa taratibu zinaendelea za kumpata mwekezaji kuendesha shughuli katika gati namba 8 hadi gati 11 bandari ya Dar es Salaam huku akisisitiza gati hizo namba 8 hadi 11, kampuni ya DP World haihusiki katika uwekezaji huo.

Pia viwanja vya ndege kama Arusha airport unaoongoza kwa miruko / flights nyingi za ndege Tanzania unaongezewa urefu wa njia ya kuruka ndege na kuwekewa taa ili ndege ziweze kutua wakati wote usiku na mchana.

1702532325605.png


Pia waziri Prof. Makame Mbarawa amesema Lindi kutajengwa uwanja wa ndege kwa kuwa kuna miradi mingi ya uwekezaji ktk sekta ya gesi n.k hivyo kunahitajika uwanja wa ndege. Vilevile viwanja vya ndege Mtwara jengo la abiria na Mwanza airport jengo la abiria kuendelezwa upya ulingane na hadhi yake.

MKUTANO WA WADAU WA SEKTA YA UCHUKUZI JIJINI ARUSHA

View: https://m.youtube.com/watch?v=xsF-PWh-WSk
Video wizara ya ujenzi
 

APSEZ said to acquire berths at Dar es Salaam Port​

A potential acquisition will mark Gautam Adani’s first major acquisition after the Hindenburg allegations and the third overall globally by his port’s unit in recent years.

MUMBAI: Adani Ports and Special Economic Zone Ltd (APSEZ) is said to be close to winning the rights to develop and run some cargo berths at Tanzania’s main port of Dar es Salaam as billionaire Gautam Adani emerges from the Hindenburg episode to make his first major acquisition and the third overall globally by his port’s unit in recent years, multiple sources said.


ET Infra could not ascertain the value of the deal that will put APSEZ firmly on course to reach its goal of becoming the world’s largest port operator by 2030.

Tanzania Ports Authority (TPA), the state-owned entity that oversees ports in the East African nation, is expected to announce the winner, in the next few days, of a dual tender to privatise Dar es Salaam Port, which handles some 95 percent of that country’s international trade
 
Hawa DP World ni watu wa ma deal kama haya, kupata vitu ambavyo tayari tumegharamia bila wao kutoa hata senti moja kama ule mkataba unavyosema bandari na maeneo yote ya ukanda yaliyo karibu na bandari wapewe.
Mama anaupiga mwingi
 
Waziri Prof. Kitila Mkumbo anaelezea makubwa kama maji, umeme na barabara ili kubadilisha eneo hili kuwa la mfano kimataifa kuwa Kurasini Logistic Centre na Industrial Park kuwa mtaa wa viwanda Business Centre Kurasini.
Huyu ni kama jina lake lilivyo
 
14 APRILI 2022

MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BANDARI TANZANIA, YATUMIA BILIONI ZA SHILINGI


View: https://m.youtube.com/watch?v=5QBcvaHUVD0&
Muonekano la kimkakati la Kurasini jirani na bandari kuu ya DSM kwa kutumia drone yaani ndege isiyo na rubani kutupa hali halisi ya maeneo ya iliyokuwa Kurasini EPZA , Shimo la Udongo na Mivinjeni jijini Dar es Salaam ambapo TPA wajenga barabara na daraja kuondoa msongamano katika bandari na ukanda ulio jirani na bandari jijini Dar es Salaam
 
14 December 2023
MAMLAKA YA USIMAMIZI YA BANDARI TANZANIA - TPA YATETA NA WADAU


View: https://m.youtube.com/watch?v=0R0XhwGDS8s

Mdau wa huduma za bandari, usafiri wa meli na bandari kavu Dr. Judith Mhina Sipendi aliye mwenyekiti mtendaji wa PMM Group, Bandari Kavu ICD na meli kubwa MV Mirembe Judith na wadau wengine kadhaa wa bandari walikutana na mkuu wa mkoa wa DSM na, uongozi wa TPA kujadilana uondoshaji wa mizigo bandari. Timu ya pamoja inayojumuisha uongozi wa mkoa, TPA na wadau imeundwa ili kutayarisha paper itakayosaidia kuboresha sera na hatimaye ufanisi wa bandari na bandari kavu.

Source : Dar es Salaam RS Digital
 
Hawa DP World ni watu wa ma deal kama haya, kupata vitu ambavyo tayari tumegharamia bila wao kutoa hata senti moja kama ule mkataba unavyosema bandari na maeneo yote ya ukanda yaliyo karibu na bandari wapewe.
inaudhi sana.
 
Kufumba na kufungua utasikia DP World kishachukua eneo! Ndivyo mambo zetu zinavyokwenda hivyo.

Kweli kabisa chochote kinawezekana katika kurupushani hii ya mashindano ya kubinafsisha.
 
Back
Top Bottom