Balaa: Mke wa Mtu Afumwa Akijiuza Usiku na Mtoto Mkononi

Simtetei huyo mama kwa kosa alilolifanya, atalipia kosa lake kadiri ya taratibu za kisheria au za kijamii. Nisichokubaliana nacho ni udhalilishaji wa namna alivyomatwa, karibu kuchaniwa nguo, kupigwa picha na kusambazwa kwa picha zake. kuna watu ambao tayari maisha yamewadhalilisha, tusiwaongezee mzigo zaidi. Ficheni basi hata sura yake, isijetokea kwamba mwisho wa siku, hana makosa lakini sura yake imeshasambazwa kwamba ni kahaba.
Huyo msichana kama likuwa anafanya ukahaba na mtoto mkonono basi ni wa kumhurumia zaidi kuliko kushitaki.
Hali ya maisha mbaya sana kwa watu wa kipato kidogo au wasio na kazi.

Ukiona hivi basi hata ndugu wa karibu hawana msaada kwa kinda huyu.
Msichana anatoka kutafuta hela ya chakula na maziwa bila kujua hatari ziambatanazo na shughuli hiyo, achilia mbali hatari kwa malaika mtoto huyo.

Hii imenisikitisha sana.
 
Mtali kwa namna yoyote iwe huyo mama kakamatwa kwenye hilo suala la kujiuza au kwenye jambo lolote hilo wapiiga picha hawakuwa na right ya kumpiga picha wazi kiasi hicho mapaja yake yako nje hata kama hao waliombeba kweney gari walimkamata kwenye tukio lolote lile
Haki za huyo mmtoto mdogo kiasi hicho ziko wapi au hata za huyo mama ziko wapi
Ni kumdhalilisha mna kudhalilisha utu wake
na hayo magazeti ya udaku yashambadika mama kuwa ni kahaba anajiuza na mtoto


Nikweli Mr Rocky Naona wengi wetu wanashabikia kudhalilishwa kwa huyu mama. Ni mara ngapi watu wanajikuta katika mikasa kama hii wakati anapita tu katika mazingira kama hayo. Tujifunze kuwa rational and fair on our feeling for what we see.
 
Katika hali ya kawaida haiwezekani kabisa mwanamke akafanya hiyo biashara akiwa na mtoto mdogo kama huyo katika eneo la tukio. Believe me huyo aliyepiga hii picha hajui kama watu wanaitumia hivi. Sio vizuri wadau. Kila mmoja amezaliwa na mama. Udhalilishaji huu unadhalilisha hata mama zetu. Hebu fikiria kama mama yako akawa anapita katika eneo hilo halafu ndio kamata kamata inaendelea na mama yako nae akatiwa nyavuni kama mshirika wa hiyo business? Tuwe fair jamani.
 
Hata anayenunua anajisikiaje kumuweka mtoto pembeni afu na kuendelea na shughuli? afu hana mvuto wa kivile
 
Shida na umaskini!! maisha bora kwa kila mtanzania!! Inasikitisha ati.
 
Jamani jamani, mama huyu anatia huruma, lakini huruma zaidi ni kwa huyo mtoto. Mara ngapi tunasikia watoto wanatupwa na hata kuuuwawa baada ya kuzaliwa na hata kabla ya kuzaliwa. Nyote nyie ni mashahidi huyu si muuaji kwani hakudhubutu hata kumwacha mwanae kipenzi nyumbani aende huko mnakomtuhumu pasipo hakika. Haya sasa kama alikuwa changu mbona hamuulizi baba na hata jamaa zake wako wapi angalau kumtunza huyu mtoto. Hana chakula, hana msaada, hamna uhakika wa hizi tuuma mnamhukumu. Ole wako unayemtuhumu ni changu pasipo kuwa na hakika na hata kama ni hivyo ungelipaswa kufikiri zaidi na sio kushabikia. POLE SANA Mama na mwanao.
 
ila wanaume tuna roho ya kinyamaa.napata picha mwanaume unamchukua huyo mwanamke una do nae..mtoto anakuwa wapi saa hiyo,lazima chini?analiaa we una furai kwa raha unampa mamaake 2000 au 3000.dah!!napata uchungu sana.
 
tupeni taarifa kamili!
huyo mama/binti alikutwa katika mazingira gani?
naamini si kila mtu anayekutwa nje usiku (binti) ni changudoa!
na ni vigumu kwa mwanaume kumnunua mwanamke mwenye mtoto wakati wapo wasio na watoto katika mazingira hayohayo! hii habari naafikiri haijakaa sawa!
ni sawa na enzi hizo za kusaka wazururaji hakukwepo na vigezo thabiti vya kubaini mzururaji ni nani/au anasifa zipi!
polisi wanahitaji kujifunza njia na mbinu za kuwatia hatiani waalifu (je uchangudoa ni uhalifu?), mbona wamejaa kwenye makasino na vilabu vikubwa hapa mjini? kwanini wa buguruni, Sinza na si wa Maisha Club, Sunciro etc?
 
uyo msichana nimeweza kumtambua mama yake anakaa washington DC,na mara ya mwisho kumuona ilikuwa naenda kuchukua zawadi kwao nimpelekee mama yake DC,mama yake amejenga kitunda,uyo mtoto inasemekana alianza kujiuza zaman tu yani ameshindikana sababu kipind mama yake yuko tz alitoroka kwao akaenda kuishi buguruni,mara ya mwisho alikuwa na watoto 3,nimeshangaa kuona picha ana mtoto mwingine tena mdogo.
masikin mama yake anapata shida sana DC anafanya kazi za kila aina na anamtumia ela ata ameweza kujenga nyumba kumbe amerudia tena hiyo biashara.
nimesikitika sana kuona picha zake na mama yake tushamjulisha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom