BAKWATA wamkemea Makonda

BAKWATA wamkemea Makonda

Ngaliba Dume

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2010
Posts
1,710
Reaction score
3,685
Sheikh mkuu wa mkoa wa Dsm leo amezungumza na waandishi wa habari na kukemea kitendo cha Paul Makonda kutumika na kuwahusisha viongozi wa kiislamu na harakati za Lowassa kwenda Ikulu

Sheikh mkuu amesema wao kama Waislamu hawawezi kuchaguliwa marafiki,wala mtu wa kushiirikiana nae ktk misaada ya kuujenga uislamu na taasisi zake.Amemuonya Makonda kuacha kutumika na kuharibu sifa za viongozzi wa kidini.

Sheikh mkuu ameendelea kusema kuwa Makonda hana amri wala dhamana ya kuwachagulia BAKWATA na Waislamu mtu wa kuwa nae,amesema Makonda aseme ni lini na wapi viongozi wa dini walitumika kwa uislamu wao kupiga kampeni.za Lowassa kwenda Ikulu

My Take
Mzee mamvi jamani anatisha sana,kasi yake ni ya hatari...kakaba kila kona
 
Manvi ni kitu ingine kabisa

Makanisani yupo

Misikitini yupo

kwa bodoboda yupo

jamani manvi anakata mbuga kwa kasi ya ajabu......wapi Membe, sita na mama migiro?
 
Natamani nijue Makonda alisema nini kuhusu Uislamu.
Ila inaonyesha Lowassa ameshajioteshea mizizi kwenye maeneo na taasisi nyingi tayari.
Kama sheikh wa mkoa wa Dar anasema Makonda aache kuwachagulia Waislamu marafiki, hii kauli ni nzito na very positive kwa Lowasa.
Napata kiwewe zaidi kuona jinsi jina la huyu mamvi linavyovuma na kutetewa na watu wasiotegemewa.
 
Soon usishangae pia tamko la wakristo kupitia CCT, PCT, RC au Sabato wakimuonya pia Makonda uache kuropoka!!

Siku zote mgombea urais wa CCM ni lazima atokee kwenye milango ya Kanisa au Misikiti.
Alifanya Kikwete na atafanya pia Lowassa, Membe au Sitta nk.
Huwezi kuitenganisha CCM na Udini.
 
Ni wachache wasiokujua wewe Shekhe wa Dar es Salaam, kwani unadhani watu hawajui kuwa unatumika, wewe ni mpenda madaraka tena sana eti unamuungamkono Lowasa ili uje uwe mufti wa tanzania, waislam sio wajinga tena, siku zako hazigandi, yaani zinasonga mbele, bakwata yaaani nyinyi mmekaa mnasubiri mke na mume wagombane ndio mfanye kazi, toka bakwata iwepo ina vyuo vingapi ilivyojenga tanzania, inanini ilichofanya kama sio kutumika kisiasa na kuwakandamiza waislam, yaani acha waislam waje wakushambulie mimi yangu macho maana msije sema kwasababu si mwenzenu ndio maana nimesema haya...
 
BAKWATA wameanza kampeni,it seem that candidate wao ni LOWASSA.
 
Soon usishangae pia tamko la wakristo kupitia CCT, PCT, RC au Sabato wakimuonya pia Makonda uache kuropoka!!

Siku zote mgombea urais wa CCM ni lazima atokee kwenye milango ya Kanisa au Misikiti.
Alifanya Kikwete na atafanya pia Lowassa, Membe au Sitta nk.
Huwezi kuitenganisha CCM na Udini.
hiyo ni kweli mkuu!
 
Lakini juzi Shekh wangu wa DSM alikuwa na kikwete na pinda kwenye mambo ya gesi who knows what was discussed!!!
 
Natamani nijue Makonda alisema nini kuhusu Uislamu.
Ila inaonyesha Lowassa ameshajioteshea mizizi kwenye maeneo na taasisi nyingi tayari.
Kama sheikh wa mkoa wa Dar anasema Makonda aache kuwachagulia Waislamu marafiki, hii kauli ni nzito na very positive kwa Lowasa.
Napata kiwewe zaidi kuona jinsi jina la huyu mamvi linavyovuma na kutetewa na watu wasiotegemewa.
Ukicheka na Nyani utavuna Mabua.
Walidhani Lowassa anatania na mbio za urais ndani ya CCM, jamaa yuko very serious.

Kwenye taasisi za Kidini ni kama alishamaliza iwe makanisani au misikitini kote ameshapandikiza mbegu nyingi sana, pia taasisi za Kielimu keshamaliza, Taasisi za Kichama/CCM huko alimaliza mwishoni mwa mwaka 2012, kwa sasa ameamua kujikita kwenye taasisi za kijamii na michezo, kufikia June Mwaka huu huenda Lowassa akawa inahitimisha harakati zake rasmi kitaasisi ili ahamie kwa ushawishi wa Mtu mmoja mmoja na hapo mtamwona sana kwenye majukwaa ya Kisiasa.

Kitisho pekee kwa Lowassa na team yake kwa sasa ni CHADEMA na harakati zao, kwani harakati hizo zinafika grassroot, mahali ambapo voters wapo, Lowassa aliliona hili tangu 2012 kule Arumeru Mashariki ambapo CCM iligaragazwa vibaya kabisa na CHADEMA ambapo Lowassa alishiriki Kikamilifu although alionekana jukwaani dakika za mwisho.
 
Sheikh mkuu wa mkoa wa Dsm leo amezungumza na waandishi wa habari na kukemea kitendo cha Paul Makonda kutumika na kuwahusisha viongozi wa kiislamu na harakati za Lowassa kwenda Ikulu
Sheikh mkuu amesema wao kama Waislamu hawawezi kuchaguliwa marafiki,wala mtu wa kushiirikiana nae ktk misaada ya kuujenga uislamu na taasisi zake.Amemuonya Makonda kuacha kutumika na kuharibu sifa za viongozzi wa kidini.
Sheikh mkuu ameendelea kusema kuwa Makonda hana amri wala dhamana ya kuwachagulia BAKWATA na Waislamu mtu wa kuwa nae,amesema Makonda aseme ni lini na wapi viongozi wa dini walitumika kwa uislamu wao kupiga kampeni.za Lowassa kwenda Ikulu
NB;% Mzee mamvi jamani anatisha sana,kasi yake ni ya hatari...kakaba kila kona

Kweli Lowassa kiboko! Kawanunua Hata Bakwata. Jamani Bakwata jitambueni. Hivyo vijisenti visiwavunjie heshima.
tunawategemea sana.
 
Back
Top Bottom