Bajeti ya mshahara wa sh. 400,000

Bajeti ya mshahara wa sh. 400,000

Kuna mwenzako ameanzisha uzi kuwa waajiriwa wana maisha mazuri kuliko wafanyabiashara.
Sasa wewe muajiriwa kwa mwezi pesa ya kula unatumia elfu 80 sasa hapa c utakuwa unakula mataka taka?
 

Pendekeza mkuu
Kwenye 400k
Ndugu unashauri tuwape sh ngapi
Na kuvaa tuweke bajeti kiasi gani

Tupunguze item gani

Ukiwa kwenye hichi kipindi, unahitaji nguo chache nadhifu ambazo utavaa jwa kipindi kirefu

Hela unayoweka akiba inagawanyika mara mbili
50% Emergency
50% Investment

Kama huna bima, ugonjwa ni dharura
Kwa hiyo pesa bado unapiga hesabu za sadaka tena? yaani hapo hata kula yako itakuwa ni ya kuunga unga tu. Ni vyema kwa hiyo pesa usipie hizo hesabu za kuinvest kwanza, kwani utaishi kwa taabu sana. Hizo hesabu utazianza ukishakuwa stable kwenye kipato chako. Yaani hata wazazi hutokuwa unawatumia hata 50K kwa mwezi, na bado umetenga 40K ya sadaka?. Huna hata bwana wadogo watakupiga hata mizinga ya vocha tu?
 
Ukiwa unalipwa 400k na huna familia, yan home alone
Mchanganuo pendekezi huu hapa
Utanishukuru baadae

100,000 Akiba (weka utt)
40,000 Sadaka
80,000 Kodi ya nyumba
80,000 chakula
50,000 usafiri
50,000 mahitaji mengine

Sadaka,
unamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwapa wahitaji au popote unapoamini

Kodi
Haipaswi kuzidi 20% ya kipato chako

Chakula
Haipaswi kuzidi 20%
Hemea kwa jumla
Weka stock ya vyakula kama dagaa, hulali njaa

Usafiri
Panga karibu na eneo la kazi
Au sehemu ya gari moja

Akiba weka utt
Ukifikisha hata 600,000, weka mpunga stock, ni gunia kumi hizi

Lazima uwe bahili hasa, nidhamu sana

Ongezea kama kuna kitu nimeacha
Au tupe uzoefu zaidi tujifunze
Bajetiii ni kwamba unaish singo mkuu. Subiri uwe na spouce au spouces na watoto au na tegemezi wengine.
 
Kwa hiyo pesa bado unapiga hesabu za sadaka tena? yaani hapo hata kula yako itakuwa ni ya kuunga unga tu. Ni vyema kwa hiyo pesa usipie hizo hesabu za kuinvest kwanza, kwani utaishi kwa taabu sana. Hizo hesabu utazianza ukishakuwa stable kwenye kipato chako. Yaani hata wazazi hutokuwa unawatumia hata 50K kwa mwezi, na bado umetenga 40K ya sadaka?. Huna hata bwana wadogo watakupiga hata mizinga ya vocha tu?
Lete mapendekezo mkuu wote tuna jifunza hapa

Imagine unalipwa 400k for 5 yrs
Kumbuka Baada ya muda, may be ndani ya 3yrs utapata familia
Utasubiri mpaka lini

Trust me, kusave ktk kipato kidogo ni maamuzi magumu sana mwanzoni, lkn utaenjoy baadaye

Sadaka, ni kulingana na unavoamini
Ninaamini ipo baraka katika kusaidia wengine wenye mahitaji hata ukiwa na kipato kidogo

Hata wazazi unaweza kuwapa sadaka, ni shukrani yako kwa Mungu
 
Kuna mwenzako ameanzisha uzi kuwa waajiriwa wana maisha mazuri kuliko wafanyabiashara.
Sasa wewe muajiriwa kwa mwezi pesa ya kula unatumia elfu 80 sasa hapa c utakuwa unakula mataka taka?
Waajiriwa wapo madaraja tofauti
Kuna wanaoanza na mshahara 1.2m huyu hatateseka sana kama wa 400k

Kuna wanaolipwa 6m, 10m+

Kwa hiyo inategemea, alikuwa anaongelea wa ngazi ipi
 
Mkuu naomba maelezo kidogo hapa kwenye utt amis vipi ni segment gani ni nzuri zaidi kuchagua unapoweka?

Vipi wakati unatoa pesa yako hakunaga mashaerti mengi mengi kama kufatilia nccf?
Pitia website yao kupata uelewa mpana
Au nenda kwenye ofisi zao kama upo dar, mwanza arusha

Kwa uwekezaji wa chini
Tumia mfuko wa ukwasi/liquid

Kutoa ni anytime kupitia mawakala wao nchi nzima ambao ni benki ya crdb

Mzigo unatua kwenye akaunti yako ndani ya siku 3 tangu ulipojaza fomu ya kutoa
 
Labda ukapange nje ya mji kama vikindu huko lakini mjini kama Magomeni,Sinza,Ilala n.k hapo hutoboi
Mwenge mataa hapo opposite na efatha unapata chumba cha 50k, mabibo pale unapata kwa chumba 60k, kigogo

Unless kama unataka yenye uzio, madirisha aluminium, chini tiles, gypsum, mlango grill
Utakwama
 
Waajiriwa wapo madaraja tofauti
Kuna wanaoanza na mshahara 1.2m huyu hatateseka sana kama wa 400k

Kuna wanaolipwa 6m, 10m+

Kwa hiyo inategemea, alikuwa anaongelea wa ngazi ipi
Hao wanaolipwa hizo pesa ni wachache sana tofauti na hawa wa madaraja ya chini.
 
Ukisha fungua, kuna baadhi ya mifuko unaweza weka hadi 10k
Yeah nimeona Hapa na details Zake hizi hapa..

Screenshot_20240410_101745.jpg
 
Back
Top Bottom