Bado wapo wenye imani na CHADEMA?

Bado wapo wenye imani na CHADEMA?

Naona una majeraha ya mtima.

Pole sana.

Ndo matokeo ya kuwekeza hisia kwenye watu wasio na uaminifu,.
Ninachokiona ni mwisho wa CDM. Chama kimeshakosa dira na hakina itikadi inayokisimamia, kwa ujumla nimekosa imani na CDM, tujiandae kwa anguko kuu katika uchaguzi wa 2020
 
Hivi bado kuna mtu bado ana imani na ccm baada ya miaka zaidi ya miaka 50?
Kama wapo basi wenye imani na Chadema pia wapo.
 
Hii ni nchi yenye dola iliyo tayari kujeruhi na kuua raia katika masuala ya kisiasa. Mifano ipo ya kutosha. Ningeshangaa sana kama CHADEMA wangeshikilia msimamo wa kuandamana kesho. Kuna mambo sikubaliani nao LAKINI, hadi sasa, naiona CHADEMA kuwa chama pekee Tanzania chenye watu wenye jeuri dhidi ya utawala wa mabavu wa serikali ya CCM.

Ni dhahiri kuwa Serikali ya CCM imeshindwa kufikia bei ya watu kama Mbowe, Lissu, Mnyika, Lema, Mdee, Sugu, n.k. CHADEMA inajengwa na watu wasiolingana na "stereotype" ya Watanzania wengi; ya kunyenyekea watawala kupita kiasi kwa ajili ya maslahi binafsi. Inavyoonekana serikali na CCM wanatikiswa sana na harakati za CHADEMA kwani hawajui jinsi ya kuwadhibiti zaidi ya kulilia "tishio dhidi ya amani" na kuamrisha polisi na, sasa, jeshi kujiandaa kupiga/kuua yeyote anayeshiriki harakati za CHADEMA. Kwa mazingira tuliyo nayo, nje ya CHADEMA, tunao mbadala upi wa kuiweka sawa serikali angalau iwe na adabu kidogo?
 
Mimi nina imani na CHADEMA.
Nyani Ngabu tengeneza uzi mwingine wenye vitufe vya ku vote ili research yako iwe na Maana
Huu mtego waliowekewa Chadema wangeingia mkenge ndio ungekuwa mwisho wao.

Watanzania tunaongoza kwa unafki, Nyani Ngabu yupo Marekani anataka wenzake wauwawe yeye abaki tu kwenye keyboard.

Nina imani kikao cha msajili kitapata ufumbuzi na mikutano itaruhusiwa kwa vyama vyote.

Malengo ya Chadema kisiasa yamefikiwa hakuna haja ya kutowa sadaka maisha ya watu na kusababishia ulemavu.
 
Hawa CHADEMA ndo basi tena.

Naona wapo kwenye mwendokasi wa kuelekea kaburini.

Hii si mara yao ya kwanza kuwapandisha watu mzuka halafu wanaishia kubadili gia angani na kuwaacha watu wakining'inia.

Nani tena atawaamini hawa jamaa? Manake baada ya kuwaaminisha watu kwa miaka mingi kuwa Lowassa ni fisadi, matokeo yake ndo akaja kuwa mgombea wao. Mamlaka ya kimaadili ya kukemea ufisadi wakayapoteza.

Baada ya kuwapandisha watu mzuka wa UKUTA, leo wameufyata mbele ya Ngosha.

Sasa eti wametangaza hayo maandamano yatafanyika Oktoba mosi.

Watampata nani hiyo Oktoba mosi? Wake, waume, na watoto wao?

Wameishiwa kabisa. Hawana jipya tena. Hawana dira wala mwelekeo wowote ule.

Mtu afadhali unaweza kusema kuwa kabla ya ujio wa Lowassa kwamba watu walijua wanasimamia nini na wanasimama wapi.

Lakini leo hii nani anayejua wanachokisimamia? Nani anajua wanaposimama?

Walishindwa hata kuwashawishi wapinzani wenzao kuwaunga mkono ki hali na ki mali kwenye huo UKUTA wao. Wengine wakadiriki hadi kuwatakia kila la kheri na kuwaahidi kuchangia damu endapo wangehitaji baada ya kupokea kichapo cha vijana wa Ngosha.

Matokeo yake tingatinga limepita na kuusambaratishia mbali.

Wanahitaji uongozi mpya wenye maono mapya la sivyo wataenda bye bye for good.
TINGATINGA linatisha wewe...!!

Hatuwahukumu chadema kwa ulaghai wa UKUTA ...bali ulaghai wao juu ya kuupinga ufisadi ilihali wanampinga mpambanaji wa ufisadi!

Pia tunawahukumu kwa ukigeugeu wao ambao tumeshaushuhudia na tutaendelea kuushuhudia(Mungu atazidi kuwaumbua inshalah)
 
Hivi bado kuna mtu bado ana imani na ccm baada ya miaka zaidi ya miaka 50?
Kama wapo basi wenye imani na Chadema pia wapo.

Ndo maana wengine hatuna vyama na wala hatukuwashabikia Lowassa au Magufuli.
 
Huu mtego waliowekewa Chadema wangeingia mkenge ndio ungekuwa mwisho wao.

Watanzania tunaongoza kwa unafki, Nyani Ngabu yupo Marekani anataka wenzake wauwawe yeye abaki tu kwenye keyboard.

Nina imani kikao cha msajili kitapata ufumbuzi na mikutano itaruhusiwa kwa vyama vyote.

Malengo ya Chadema kisiasa yamefikiwa hakuna haja ya kutowa sadaka maisha ya watu na kusababishia ulemavu.
Halafu anatuita Mashabiki wa CHADEMA wa Mtandaoni wakati kaleta hoja mtandaoni sasa sijui alitaka ajibiwe kwa platform ipi zaidi ya kwenye mtandao
 
Huu mtego waliowekewa Chadema wangeingia mkenge ndio ungekuwa mwisho wao.

Watanzania tunaongoza kwa unafki, Nyani Ngabu yupo Marekani anataka wenzake wauwawe yeye abaki tu kwenye keyboard.

Nina imani kikao cha msajili kitapata ufumbuzi na mikutano itaruhusiwa kwa vyama vyote.

Malengo ya Chadema kisiasa yamefikiwa hakuna haja ya kutowa sadaka maisha ya watu na kusababishia ulemavu.

Uliniona wapi mimi nikichagiza watu waende wakaandamane?
 
Hawa CHADEMA ndo basi tena.

Naona wapo kwenye mwendokasi wa kuelekea kaburini.

Hii si mara yao ya kwanza kuwapandisha watu mzuka halafu wanaishia kubadili gia angani na kuwaacha watu wakining'inia.

Nani tena atawaamini hawa jamaa? Manake baada ya kuwaaminisha watu kwa miaka mingi kuwa Lowassa ni fisadi, matokeo yake ndo akaja kuwa mgombea wao. Mamlaka ya kimaadili ya kukemea ufisadi wakayapoteza.

Baada ya kuwapandisha watu mzuka wa UKUTA, leo wameufyata mbele ya Ngosha.

Sasa eti wametangaza hayo maandamano yatafanyika Oktoba mosi.

Watampata nani hiyo Oktoba mosi? Wake, waume, na watoto wao?

Wameishiwa kabisa. Hawana jipya tena. Hawana dira wala mwelekeo wowote ule.

Mtu afadhali unaweza kusema kuwa kabla ya ujio wa Lowassa kwamba watu walijua wanasimamia nini na wanasimama wapi.

Lakini leo hii nani anayejua wanachokisimamia? Nani anajua wanaposimama?

Walishindwa hata kuwashawishi wapinzani wenzao kuwaunga mkono ki hali na ki mali kwenye huo UKUTA wao. Wengine wakadiriki hadi kuwatakia kila la kheri na kuwaahidi kuchangia damu endapo wangehitaji baada ya kupokea kichapo cha vijana wa Ngosha.

Matokeo yake tingatinga limepita na kuusambaratishia mbali.

Wanahitaji uongozi mpya wenye maono mapya la sivyo wataenda bye bye for good.
1472666259690.jpg
 
Nimekusoma, una hoja lakini, ukumbuke kwamba, viongozi wengi wa chadema wamekamatwa, hayo maandamano yangefanyika vipi? Nadhani alichokosea mbowe ni kutaja tarehe nyingine, vile vile naona alitakiwa kuhairisha maandamano tangu aliposikia kuna zoezi la usafi, maana wananchi walihofu hapo kwenye usafi wa jeshi.
 
Hawa CHADEMA ndo basi tena.

Naona wapo kwenye mwendokasi wa kuelekea kaburini.

Hii si mara yao ya kwanza kuwapandisha watu mzuka halafu wanaishia kubadili gia angani na kuwaacha watu wakining'inia.

Nani tena atawaamini hawa jamaa? Manake baada ya kuwaaminisha watu kwa miaka mingi kuwa Lowassa ni fisadi, matokeo yake ndo akaja kuwa mgombea wao. Mamlaka ya kimaadili ya kukemea ufisadi wakayapoteza.

Baada ya kuwapandisha watu mzuka wa UKUTA, leo wameufyata mbele ya Ngosha.

Sasa eti wametangaza hayo maandamano yatafanyika Oktoba mosi.

Watampata nani hiyo Oktoba mosi? Wake, waume, na watoto wao?

Wameishiwa kabisa. Hawana jipya tena. Hawana dira wala mwelekeo wowote ule.

Mtu afadhali unaweza kusema kuwa kabla ya ujio wa Lowassa kwamba watu walijua wanasimamia nini na wanasimama wapi.

Lakini leo hii nani anayejua wanachokisimamia? Nani anajua wanaposimama?

Walishindwa hata kuwashawishi wapinzani wenzao kuwaunga mkono ki hali na ki mali kwenye huo UKUTA wao. Wengine wakadiriki hadi kuwatakia kila la kheri na kuwaahidi kuchangia damu endapo wangehitaji baada ya kupokea kichapo cha vijana wa Ngosha.

Matokeo yake tingatinga limepita na kuusambaratishia mbali.

Wanahitaji uongozi mpya wenye maono mapya la sivyo wataenda bye bye for good.

Tena tunaoiamini CHADEMA ndo tumeongezeka sasa. Tukutane 101.
 
Huu mtego waliowekewa Chadema wangeingia mkenge ndio ungekuwa mwisho wao.

Watanzania tunaongoza kwa unafki, Nyani Ngabu yupo Marekani anataka wenzake wauwawe yeye abaki tu kwenye keyboard.

Nina imani kikao cha msajili kitapata ufumbuzi na mikutano itaruhusiwa kwa vyama vyote.

Malengo ya Chadema kisiasa yamefikiwa hakuna haja ya kutowa sadaka maisha ya watu na kusababishia ulemavu.
Nakubaliana na wewe kuliko watu waumizwe na vyombo dola vya serikali dhalimu, bora kutafta suluhu am sure wengi hawaelewi yanayoendelea nyuma kuhusu amani ya nchi yetu kuandika na kulaumu ni rahisi, mno ila uhalisia hawaujui.
 
Back
Top Bottom