Bado wapo wenye imani na CHADEMA?

Bado wapo wenye imani na CHADEMA?

Wadau,

Nimehamasika kuweka hii kura baada ya Mdau mmoja Nyani Ngabu kuweka Uzi kua Imani yake (pengine na wengine) kwa CHADEMA imepotea baada ya CHADEMA Kuhairisha maandamno yao yaliyokua yafanyike tarehe 01/09/2016.

Post hiyo ipo humu Bado wapo wenye imani na CHADEMA?

Binafsi bado nina imani na CHADEMA, na hata pale baada ya kuhairishwa nahesabia kama CHADEMA imepata ushindi mkubwa sana kwa jinsi upande wa pili ulivyolichukulia hili swala serious na kujiandaa kukabiliana nalo. Nguvu iliyotumika kujaribu kuizima ni dhahiri kua dhamira ya UKUTA ilifanikiwa, ila kwa namna ingine.
Teh teh! Makujifariji
 
Ukitaka kujua angalia kama mazoezi ya majeshi yataendelea au la. Na jiulize operesheni ya Makonda na vikosi anavypita vyake ilihali ni vya Watanzania kwa nini imekuwa extended.
 
Anachokera zaidi ni ule uwezo wake wa kujenga spirit ya kiburi miongoni mwa watu wanaomuamini. Hana kabisa humility, hawezi kujishusha akawa katika level ya mtu wa kawaida. EL pamoja na kukejeliwa sana na viongozi wa juu wa chama tawala lakini bado alikwenda kwenye sherehe ya mzee BWM, that is what we call humility, that can only be found in a true leader, it comes from heart not mind.
FAM anakosa sifa za asili za kuwa kiongozi, kwani kuongoza ni zaidi ya kuendesha vikao vya chama na kuhutubia jukwaani, mtindo wako wa maisha pia ni sehemu muhimu wa sifa za uongozi.
Ulitaka ajenge 'spirit' ya uoga na kujipendekeza kama huko kwenu lumumba. Poleni.
 
Mimi naammini hasira dhidi ya ccm na serikali yake inazidi kuongozeka, hii ni kwa mujibu wa vijiwe ninavyotembelea tu. Sijasikia watu wakikata tamaa na CHADEMA.
 
Huo ndiyo ukweli ulio wazi.



Sina uhakika kama uko sawa kwa kutukuza English, lugha ambayo nina uhakika ni tatizo kwako. kumbe hujui lugha ya ya Taifa si 'English' au! Umesomea "english medium school"! Hongera kwa ujuha huo. Aibu.

Mbowe kweli ni mwiba mchungu kwenye mioyo ya wapenda amani na maendeleo, nchini. Alijidhirisha kama Kiongozi mwanamapinduzi kwa kauli zake za kuchukia maouvu katika jamii (rushwa, ufisadi, ubadhirifu) na utendaji mbovu (uzembe) wa watumishi wa serikali. Laiti angesimama kama mgombea Urais wakati huo, badala ya Slaa, naamini angeshinda.

Kwa sasa Mbowe kakosa mwelekeo, ila imedhihirika wazi kwamba kumbe ni mjasiriamali kisiasa. Amemkaribisha mtu ambaye chama chake kilimtuhumu ni fisadi papa, kwa sababu ya umaarufu wake kisiasa, ili apate majimbo mengi ya uchaguzi (ruzuku). Angalau hiyo ruzuku basi itumike kama mtaji wa kuweka vitega uchumi vya chama, ioi kiinuke kiuchumi na kuweza kujijenga zaidi, badala ya kuendesha operesheni za kujinufaisha binafsi na kikundi cha watu wachache kwenye chama.
Ni sawa na Lucifer kujifanya anamshauri malaika wa Mungu namna ya kumpenda Mungu
 
Nisipokuwa na imani na CDM niwe na imani na chma gani sasa?

CDM IS DA ONLY HOPE LEFT
 
Kwa wanaojua sayansi ya siasa, hiki walichokifanya chadema ni mafanikio makubwa sana kwao, kwa jinsi tulivyoona hadi mwanasheria mkuu akiwa kwenye press, inamaanisha kwa sasa serikali itabidi ijiridhishe sheria zinasemaje kabla ya kufanya jambo. Siamini kwamba hawajui na ndio maana wametumia kila njia kushambulia hii operation.
 
Tukose imani kwa sababu ya kuahirisha maandamano, akili gani hizi!!?
 
Ulitaka ajenge 'spirit' ya uoga na kujipendekeza kama huko kwenu lumumba. Poleni.
Angalau atumie akili na kutambua kuwa greda au tingatinga linaweza kuvunja ukuta ndani ya muda wowote ule.
Unapowajengea watu spirit ya kuwa na kiburi, kumbuka kwamba unapambana na mamlaka ambayo inaweza kukudhuru anytime.
Kosa la huyo ambaye akipiga chafya watu kama nyinyi mnapatwa na mafua ya muda mrefu, ni kwamba hajui kwamba tactics za mapambano huenda zikibadilika, hazipaswi kubakia ni zile zile.
 
Angalau atumie akili na kutambua kuwa greda au tingatinga linaweza kuvunja ukuta ndani ya muda wowote ule.
Unapowajengea watu spirit ya kuwa na kiburi, kumbuka kwamba unapambana na mamlaka ambayo inaweza kukudhuru anytime.
Kosa la huyo ambaye akipiga chafya watu kama nyinyi mnapatwa na mafua ya muda mrefu, ni kwamba hajui kwamba tactics za mapambano huenda zikibadilika, hazipaswi kubakia ni zile zile.
Nchi inaongozwa kwa katiba, na sio matamko. Mengine hayo hatuyahitaji.
 
Nchi inaongozwa kwa katiba, na sio matamko. Mengine hayo hatuyahitaji.
Kuongozwa na katiba sio kigezo cha watu kuendelea kuishi maisha ya kukariri.
Wakati masikini anapoishi kwa shida wakati uhalisia wa mambo ni kwamba anayemuibia haki yake ni msomi aliyesomeshwa kwa kodi ya masikini huyo huyo tena anayoilipa kwa shida, katiba inakuwa kazini kama kawaida.
Wakati mkurugenzi analifisi shirika la ndege mpaka nchi inazidiwa na kina Ethiopia, Kenya na Rwanda, katiba inakuwa kazini kama kawaida.
Punguzeni kuishi kwa kukariri kama vile mwanafunzi anavyokariri ili aweze kufaulu mitihani ya darasani.
 
Kuongozwa na katiba sio kigezo cha watu kuendelea kuishi maisha ya kukariri.
Wakati masikini anapoishi kwa shida wakati uhalisia wa mambo ni kwamba anayemuibia haki yake ni msomi aliyesomeshwa kwa kodi ya masikini huyo huyo tena anayoilipa kwa shida, katiba inakuwa kazini kama kawaida.
Wakati mkurugenzi analifisi shirika la ndege mpaka nchi inazidiwa na kina Ethiopia, Kenya na Rwanda, katiba inakuwa kazini kama kawaida.
Punguzeni kuishi kwa kukariri kama vile mwanafunzi anavyokariri ili aweze kufaulu mitihani ya darasani.
Hizo hadithi za kutunga. Wakati wa kuapa hakutumia hizo hadithi, alitumia katiba. Kitaeleweka tu bado kitambo kidogo tu na nyie mtafumbuka macho. Mungu awabariki. AMEN.
 
Hizo hadithi za kutunga. Wakati wa kuapa hakutumia hizo hadithi, alitumia katiba. Kitaeleweka tu bado kitambo kidogo tu na nyie mtafumbuka macho. Mungu awabariki. AMEN.
Katiba aliyoapa kuitumia ndio hiyo ambayo imeuvunja UKUTA. huwezi kuishi kwa kutegemea kificho cha demokrasia, ukawa na uwezo wa kupambana kiuchumi na wanaokuzunguka. JK aliwapa uhuru mkubwa sana wa kuongea, matokeo yake mkaishia kumtusi na kumdhalilisha.
Mnapozimwa tangu mapema maana yake imeshagundulika kwamba hamna shukrani hata kidogo.
Na mtu asiye na shukrani siku zote huishi kwa kutegemea fadhila inayotokana na uvumilivu wa mtu.
Mmekariri maisha, ufike wakati wa kubadilika, na muwe tayari kuyapokea mabadiliko. Vinginevyo mtaishia kulalama na kulialia bila ya kuwa na nguvu zozote za maana za kubadilisha chochote kile.
 
Katiba aliyoapa kuitumia ndio hiyo ambayo imeuvunja UKUTA. huwezi kuishi kwa kutegemea kificho cha demokrasia, ukawa na uwezo wa kupambana kiuchumi na wanaokuzunguka. JK aliwapa uhuru mkubwa sana wa kuongea, matokeo yake mkaishia kumtusi na kumdhalilisha.
Mnapozimwa tangu mapema maana yake imeshagundulika kwamba hamna shukrani hata kidogo.
Na mtu asiye na shukrani siku zote huishi kwa kutegemea fadhila inayotokana na uvumilivu wa mtu.
Mmekariri maisha, ufike wakati wa kubadilika, na muwe tayari kuyapokea mabadiliko. Vinginevyo mtaishia kulalama na kulialia bila ya kuwa na nguvu zozote za maana za kubadilisha chochote kile.
Nadhani umeanza kuota.Nenda kaisome, hakuna popote panapozuia siasa kwa wengine isipokuwa yeye tu. Kapumzike.
 
Nadhani umeanza kuota.Nenda kaisome, hakuna popote panapozuia siasa kwa wengine isipokuwa yeye tu. Kapumzike.
Wewe ndiye uliye ndotoni. Sijakataa juu ya uhuru wa katiba. Naongelea umasikini unaotuzunguka na juuya utatuzi wake licha ya uhuru mkubwa ulio ndani ya katiba.
Uhuru wa kuwakilisha hisia zako ulio ndani ya katiba unakuwa na faida zipi ikiwa hauwezi kuongeza pato lako na langu?.
Sifa za nchi kuitwa ya kidemokrasia zina faida gani, ikiwa hakuna ubunifu wa kutafuta maisha yenye neema miongoni mwa raia wake?. Ambao bila ya hata wanatembea na nguo zenye viraka lakini wapo huru?.
 
Wewe ndiye uliye ndotoni. Sijakataa juu ya uhuru wa katiba. Naongelea umasikini unaotuzunguka na juuya utatuzi wake licha ya uhuru mkubwa ulio ndani ya katiba.
Uhuru wa kuwakilisha hisia zako ulio ndani ya katiba unakuwa na faida zipi ikiwa hauwezi kuongeza pato lako na langu?.
Sifa za nchi kuitwa ya kidemokrasia zina faida gani, ikiwa hakuna ubunifu wa kutafuta maisha yenye neema miongoni mwa raia wake?. Ambao bila ya hata wanatembea na nguo zenye viraka lakini wapo huru?.
Katiba iko wazi, hayo mnayochomeka ndio tatizo lenyewe, kwa malengo yenu maovu. Over and out
 
Katiba iko wazi, hayo mnayochomeka ndio tatizo lenyewe, kwa malengo yenu maovu. Over and out
Katiba kuruhusu siasa haimaanishi nchi iwe na anarchy. JK aliwapa uhuru mkubwa sana, bahati mbaya miaka yake kumi mkashindwa kuuthamini. This time around you will be dancing according to the song that is played by our current leadership.
Nchi sio mahali ambapo kila mtu awe na sauti kwa kisingizio cha demokrasia. Uhuru unayo mipaka yake, na kote duniani sio hapa tu.
 
Back
Top Bottom