Bado wapo wenye imani na CHADEMA?

Bado wapo wenye imani na CHADEMA?

Nilitoa shilingi yangu mwaka jana baada ya "landing gears" kurudishwa ndani na 'pipa' kutua kwa kutumia 'tumbo'.

Mbowe must step down, hana maono tena, aliniudhi sana last year, awaachie wengine wenye fikra mpya kuongoza chama. Matamko yasiyo na tija yanaipeleka chadema kuzimu.
 
ACT Wazalendo wajanja sana wao mapema tu walisema watachangia damu.

Ahahahahahaha!!!
 
ACT Wazalendo wajanja sana wao mapema tu walisema watachangia damu.

Ahahahahahaha!!!

Aisee nilicheka sana kuhusu hiyo ya kuchangia damu.

Wao hawakutaka maumivu ya virungu na maji ya upupu.

Wakajitolea kuchangia damu...dizaini sindano haiumi kama virungu.
 
UKUTA wamehairisha hawajaufuta...wacha hii mihemko ya wafanya usafi ipite
 
Sijui kwa nini tu watu huwa hawajibu maswali.

Unamuuliza hiki yeye halafu yeye anakuja na ngonjera nyingine kabisa!

Ndo maana tuna mambo kama hayo ya UKUTA.
Mtu hawezi kujibu swali ambalo halina jibu. tatizo ulilo nalo ni kubwa kidogo zaidi hata ya Mfalme Magufuli. Unachoamini wewe si kila mtu anaamini hivyo.
 
Mm niwape pongezi walio piga ngoma ikanoga na kuwapa hamasa na midadi yenye hari ya juu kabisa upande ule wa pili kuicheza ngoma hio japo ilikua ya mda mrefu lkni hata hawakuchoka kuicheza kwakweli mtoto wa mjini ni wa mjini
 
Mbona nyie mlikuwa mnapiga kelele kwenye Instagram huko na siku moja kabla ya siku ya siku ujumbe umepenyeza.

Ona hawa wenzio....hivi kweli wamekaa hata mkao wa ku rumble hawa?


Big up grinders,Prof umenikumbusha zali la mentali,Sugu umenikumbusha lile neno mzuka,haswa mzuka wa Ukuta.
 
Walau CHadema wameonyesha uthubutu kutetea katiba.
 
Dah.... viongozi wa cdm upeo wao wa kufikiri hauzidi jioni ya leo....ndiyo maana wakaokota mizoga .....wakaharibu muvi yote iliyopangwa kwa zaidi ya miaka 10.... walaaniwe Mbowe & co kwa kuvuruga demokrasia yetu..
 
Ila nadhani tuache.siasa kwenye siasa. Yani kweli watu walitarajia kuwa kungekuwana maandamao? Ukweli ni kuwa hata kama kusingekuwa na mikwara ya serikali bado waandamanaji hawakuwepo wengi.

Hivyo nadhani chadema wameona hali ilivo na wakakubaliana nayo kwani hawakuwa na namna( I belive they did not want to but they had to) kwahiyo kuwalaumu kwanini hawakutekeleza maandamano ni kuwaonea ila wanaweza kulaumiwa kuanzia namna walivoweka hilo lengo na ushirikishwaji wa wadau mbalimbali.

Binafsi nilitegemea kuwa wasingetekeleza.kitu hivyo sijashangazwa na.chochote. Ila chadema wanamengi ya kujifunza hapa. Waache dhana ya kutaka kuwa juu ya wengine always na wakubali kuwa kunapokuwa na ishu wanazoamini ni za kitaifa washirikiane na vyama vingine.
 
Back
Top Bottom