Bandiwe
JF-Expert Member
- Oct 19, 2013
- 9,530
- 3,553
Kwa kina manyumbu aka ufipa !Makarai ndio wapi huko?
Kwa kina manyumbu aka ufipa !Makarai ndio wapi huko?
duuh jamani tusipende kila kitu kuihusisha serikali kuna watu wengine wana personal issues..kila kitu siasa..watanzania bhana..!!
duuh jamani tusipende kila kitu kuihusisha serikali kuna watu wengine wana personal issues..kila kitu siasa..watanzania bhana..!!
Jamaa alikuwa kajidunga vipombe vyake tu
Alizimika...kinywaji kilimkata network.Akakutana na mchaka mchaka wa watu wasiojulikana??
Ndoa matatani....*TAARIFA YA MWANDISHI WA GUARDIAN KULEWA BILA KUJITAMBUA*
Mnamo tarehe 08/04/2018 majira ya Saa 1:30 asubuhi eneo la Bunju A Mianzini mwandishi wa habari aitwaye *Finnigan Frazer Simbeye*,47 yrs Mkristo mwandishi wa habari wa gazeti la Guardian Mnyiha,mkazi wa Bahari beach mtaa wa kondo alikutwa amelewa bila kujitambua na kukutwa amelala mtaroni jirani Bagamoyo road.
Taarifa kamili ni kwamba mnamo tarehe 07/04/2018 Majira ya saa 4:00 asubuhi alitoka nyumbani kwake Bahari beach akiwa na gari lake T383 BCU Toyota Mark ll kwenda Tegeta Kibo ambako aliiacha gari pale na kwenda eneo la Mwenge na baadae alirudi Tegeta kibo na kuchukua gari lake hadi Ununio katika bar ya *Bajet* na baadae alirudi Tegeta darajani katika bar ya *B &DG* ambako alikutana na hawala yake aitwaye *Tonto* mkazi wa Salasala na hapo alikunywa bia 8. Ilipofika saa 1:00 hrs usiku alikwenda katika Bar ya *QR* eneo la Azania Tegeta na kukutana na hawala yake mwingine mhudumu wa Bar hiyo anayeitwa *Grace* na kuendelea kunywa pombe!!!.
Ilipofika saa 3:00 usiku alikwenda katika bar ya *Benten* na kuendelea kunywa na pale alikunywa bia chupa 6 na baadae aligundua kuwa amelewa sana,na hapo hawala yake *Grace* alimshauri watafute Guest walale lakini wakati wakienda gari lake liliingia katika dimbwi la maji na kuzimika na alipoomba msaada wa kulitoa ikashindikana hivyo akaliacha hapo hapo na wakati huo huo hawala yake *Grace* alichukua simu yake ya Smart Phone aina ya *LG* na kuondoka huku akimuacha pale.
Majira ya saa 10:00 usiku alichukua bodaboda kwenda nyumbani kwake Bahari beach ambako aligonga lakini hakufunguliwa na baada ya kutofunguliwa aliamua kwenda tena katika Bar ya Kibo ambao alifika saa 11:00 alfajiri na kukuta watu wanatoka na Bar ikiwa imefungwa,hivyo kuchukua bodaboda kurudi nyumbani tena lakini pia hakufunguliwa na kwa kuwa alikuwa amelewa sana aliamua kuondoka na hakukumbuka tena kinachoendelea hadi asubuhi anajikuta yupo Mwananyamala Hospitali.
Katika mahijiano tumegundua kuwa mwandishi huyo amekunywa pombe sana na kulewa kushindwa kujitambua, amekutwa na ufunguo wa gari lake mfukoni mwake akiwa hospitali na hana jeraha,uvimbe wala mikwaruzo yoyote mwilini, amewekewa dripu za maji na anaendelea vizuri japo bado amelazwa Hospitali Mwananyamala .
Tayari polisi amefunguliwa jalada Kosa la *KULEWA BILA KUJITAMBUA WMB /IR/1565/2018* Taarifa za mitandao kuwa ametekwa sio kweli.
Huwa anaandika habari za aina gani? Tuanzie hapo kwanza maana kama anaandikaga habari za michezo basi watafute chanzo kingine cha tatizo!
Wakurupukaji wa kutoa lawama za kijinga kwa mamlaka naona mmeumbuka...Mjipange
Tunako kwenda ni kubaya sana. Kama mkubwa hakemei watu wanaopotea, tutapotezenana wengi sana hata kwa visa ambavyo serikali haihusiki na lawama zote zitaelekezwa kwa serikali.
Mjomba umeongea kwa busara sana na maneno yaliyojaa hekima sanaa. Tunaangamia taratibu, mazuzu wanashangalia..jk nitamlaani mpaka naenda kwa maanani...baharia wa msoga kacheza mbowe sanaaa...tuko pabaya ndugu zangu..tuanze kutembea kwa makundi ndugu zangu.
Lugha ya malkia imekuja kwa bombadie,andika kwa kinyamwezi