Kamanda wa Polisi wilaya ya Kinondoni afande Jumanne afunguka kuhusiana na tukio la mwandishi wa gazeti la the Guardian kuokotwa maeneo ya Bunju akiwa hajitambui
"Mwandishi wa habari wa gazeti la the Guardian bwana Finnigan alfajiri ya leo amekutwa akiwa amelala maeneo ya Bunju A, Bunju A ni mkoa wa kipolisi wa Kinondoni kwahiyo taarifa zile tulivyozipata tulituma askari na askari walikwenda wakakuta mtu huyo wakamkagua, ukaguzi wa awali ukienda sehemu ya tukio ikaonekana mtu yule hajitambui taarifa za awali za maafisa waliofika pale walimuona katika hali na mazingira ya ulevi kwa maana ya harufu ya pombe -Jumanne murilo mkuu wa Polisi wa Kinondoni
Kwahiyo moja ya majukumu tunayoyafanya sisi tukikutana na hali ya namna hiyo bila kujali yeye ni nani kwasababu tumeshakutana na watu wa namna hiyo mara kadhaa hasa siku za mwisho wa wiki kwahiyo tulimchukua na kumpeleka kwenye hospitali ya Mwananyamala kwaajili ya uchunguzi zaidi.
Uchunguzi wa awali wa Polisi waliofika eneo la tukio wamethibitisha kwangu kuwa mtu yule hakuwa na jeraha lolote lile hata michirizi ya damu hakuna bali amekuwa amelewa kwa kiwango kikubwa
Mimi kama afisa wa Polisi kazi yangu ni kuchunguza ni kwanini mtu yule amelewa kwa kiasi kikubwa kitu gani kilimfanya alewe vile, sisi kama Polisi hatupendi kufanya kazi kwa hisia.-Jumanne Muliro
"Mwandishi wa habari wa gazeti la the Guardian bwana Finnigan alfajiri ya leo amekutwa akiwa amelala maeneo ya Bunju A, Bunju A ni mkoa wa kipolisi wa Kinondoni kwahiyo taarifa zile tulivyozipata tulituma askari na askari walikwenda wakakuta mtu huyo wakamkagua, ukaguzi wa awali ukienda sehemu ya tukio ikaonekana mtu yule hajitambui taarifa za awali za maafisa waliofika pale walimuona katika hali na mazingira ya ulevi kwa maana ya harufu ya pombe -Jumanne murilo mkuu wa Polisi wa Kinondoni
Kwahiyo moja ya majukumu tunayoyafanya sisi tukikutana na hali ya namna hiyo bila kujali yeye ni nani kwasababu tumeshakutana na watu wa namna hiyo mara kadhaa hasa siku za mwisho wa wiki kwahiyo tulimchukua na kumpeleka kwenye hospitali ya Mwananyamala kwaajili ya uchunguzi zaidi.
Uchunguzi wa awali wa Polisi waliofika eneo la tukio wamethibitisha kwangu kuwa mtu yule hakuwa na jeraha lolote lile hata michirizi ya damu hakuna bali amekuwa amelewa kwa kiwango kikubwa
Mimi kama afisa wa Polisi kazi yangu ni kuchunguza ni kwanini mtu yule amelewa kwa kiasi kikubwa kitu gani kilimfanya alewe vile, sisi kama Polisi hatupendi kufanya kazi kwa hisia.-Jumanne Muliro