Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 2,206
- 4,698
Asili yetu ni Kijiji cha Nyamwaga, Tarime Mkoani Mara na ni desturi ya ukoo wetu kufanya vikao kujadili masuala yanayotuhusu
WanaUkoo hupewa taarifa mapema kwani wanaishi maeneo tofauti na baadhi ya maeneo kuna shida ya miundombinu ya usafiri
Hata hivyo kwenye kikao cha karibuni Babu yangu hakuhudhuria na nilipojaribu kudodosa niliambiwa hakupewa taarifa kwa wakati!
Nimeshangazwa na sijui kwanini Babu yangu ambaye ni MwanaUkoo Mwandamizi tena aliyewahi ongoza Vikao vingi vya Ukoo siku za nyuma eti ameshindwa hudhuria kikao kwa kukosa taarifa!
Babu yangu ni Mstaafu wa aliyerejea Kijijini akisimamia miradi yake ya kilimo na ufugaji aliyoianzisha kutokana na pesheni yake.
Pamoja na changamoto hiyo kikao kiliendeshwa vizuri na Mwenyekiti wa Ukoo Mzee Chacha na kufikia maazimio/ maamuzi kadhaa sambamba na kuhimiza upendo na mshikamano
Pamoja na kukosekana kwa Babu yangu nitaheshimu maamuzi au maazimio ya Kikao cha Ukoo
Siku moja nitamtafuta tukae chini anipe mrejesho wa kilichojiri!
Wasalaam
WanaUkoo hupewa taarifa mapema kwani wanaishi maeneo tofauti na baadhi ya maeneo kuna shida ya miundombinu ya usafiri
Hata hivyo kwenye kikao cha karibuni Babu yangu hakuhudhuria na nilipojaribu kudodosa niliambiwa hakupewa taarifa kwa wakati!
Nimeshangazwa na sijui kwanini Babu yangu ambaye ni MwanaUkoo Mwandamizi tena aliyewahi ongoza Vikao vingi vya Ukoo siku za nyuma eti ameshindwa hudhuria kikao kwa kukosa taarifa!
Babu yangu ni Mstaafu wa aliyerejea Kijijini akisimamia miradi yake ya kilimo na ufugaji aliyoianzisha kutokana na pesheni yake.
Pamoja na changamoto hiyo kikao kiliendeshwa vizuri na Mwenyekiti wa Ukoo Mzee Chacha na kufikia maazimio/ maamuzi kadhaa sambamba na kuhimiza upendo na mshikamano
Pamoja na kukosekana kwa Babu yangu nitaheshimu maamuzi au maazimio ya Kikao cha Ukoo
Siku moja nitamtafuta tukae chini anipe mrejesho wa kilichojiri!
Wasalaam