Babu wa Loliondo afungiwa kwa muda kutoa huduma...

Kupima ufanisi wa kitu kuna njia nyngi: mfano, ufanisi wa mkandarasi unaweza kupimwa kwa kupima ubora wa jengo au barabara aliyojenga na si kukagua vyeti vyake au zana alizotumia. Nawashauri wapime wagonjwa kama wamepona au la.
Mkuu nia ya serikali si kujua tu kama hizo dawa zinatibu, je zina usalama gani kwa mtumiaji? unaweza ukanywa leo ukapona ukimwi lakini kumbe baada ya miezi 6 unaanza kupata madhara makubwa yanayotokana na hiyo dawa, mara ngapi tumeletewa madawa yanayo tibu lakini kumbe yana madhara makubwa mbeleni.
Ondoa dhana ya kudhani dawa inapimwa ili kujua tu kama inaponyesha au la ili ipigwe marufuku, tambua wale wote wanao kunywa dawa hizi wakianza kupata madhara mbeleni tutakuwa wa kwanza kuhoji serikali ilikuwa wapi
 
TFDA!!!! ....hawa jamaa tunajua kazi lishaashinda zamani maana bdidhaa zisizofaa na kuisha muda zimejaa hadi supermarkets! Kwanza maabara zao ziko wapi? Mbona profesa mmoja alisema juu ya ubovu wa maji na hawakufanya lolote? ...by the way, babu mwenyewe hajasema alifanya laboratory test kutengeneza dawa yake bali alioteshwa! Labda wamuombe Sheikh Yahaya naye aoteshwe kuipinga
 
pumbafffff kabisa hii serikali badala ya kushugulika na masuala ya msingi wameshaona ajenda ya babu wa loliondo ni ishu, mpeni uyu babu sapoti aendelee kutoa huduma yake, mmeshaambiwa kuwa hii dawa inaenda na suala la imani asa utafiti gani mnaoutaka??? kwenye makanisa kibao waumini wanafanyiwa maombezi na kupewa maji kama ishara ya dawa na kupokea uponyaji, je huwa mnaenda kuwafanyia utafiti??? wajinga sana nyie wote hapo wizara ya afya
 
:A S 13:Ukweli hiyo siyo ndumba wala utapeli wa kujitafutia pesa, kwani kama angekuwa anataka pesa angekamua pesa kibao kwa wagonjwa lakini yeye anachukua sh.200/- tu na sh.300/- kwa wanaomsaidia kazi kama kuchemsha dawa, kuchuma dawa, kuosha vyombo na kupokea pesa. halafu mpaka wakuu wa nchi wamekwenda wewe unasubiri nini?
wahi ndg yangu
 
Tanzanians must shun the supposed influence of superstition in matters of national interest. Recent studies have shown that belief in magic is widespread throughout sub-Sahara African countries and Tanzania is leading in these irrational beliefs. Nimeshangaa kumuona Mwenyekiti wa CCM mkoa wa kilimanjaro front page ya magazeti akibugia kombe la mitishamba. Any way hii ni karne ya 21 na sio stone age au Dark ages.
Jamani mi nimeona vitu lakini hiki cha loliondo kimenishtua sana, kwasababu Mzee huyu ni wa ajabu na ameweza kujipatia njia nzuuurii ya kutafuta Pesa bila kutumia unyang'anyi wala Ndumba, bali kwa kutumia Akili yake.
Hakuna uthibitisho wa kisayanxzi kwamba dawa hiyo inaponesha, na kimachoshangaza Eti Dawa hiyo huponi ukichota mwenyewe mpaka achote kwa mkono wake.
naomba tuwege makini, na naomba uthibitisho ili na mimi niende bana

Eti wadau ni njia ya kutafuta Ela au Dawa kweli?
 
Kufuatia ujumbe uliotumwa na wizara ya afya na ustawi wa jamii kwenda Loliondo kwenda kuangalia uhalali wa matibabu yanayo tolewa na babu inasemekana babu hakuwa tayari kuruhusu wataalam hao kuipima dawa yake. ndugu wanajamii je hiyo imekaaje?

Wamekurupuka hao! Babu ni mjanja hii kitu ni 'Intellectual Property' yake kwa hiyo ni lazima wakubaliane kwanza. Hao wanataka kumuingiza mujini ili wai-patent kazi yake...

Bravo Babu wa Loliondo...:wink2:
 
Sasa huo utafiti watafanyaje wakati babu kagoma kutoa dawa yake au baadae alikubali?, hii ni sinema nyingine tukae mkao wa kutazama!!!!
 
Kati ya mambo ambayo amevuta hisia za watu mwezi huu ni juu ya idadi kubwa ya watu wanaomiminika eneo la Loliondo ili kupata tiba juu ya magonjwa yanayowasumbua. Kitu ambacho kinasikitisha sasa hivi ni kuwa watu wengi wanachukulia tukio hili kama utani au jambo la kufikirika, watu wengi wamekuwa wakitafuta kujua ni nani au kiongozi gani anamekwenda huko kupata tiba, kibaya zaidi sababu za kutaka kujua majina au wadhifa wa viongozi wanokwenda huko ni ili kujaribu kuwadhalilisha au kuwafanya waeleweke kwenye jamii kuwa viongozi hao ni wagojwa.Nafikiri linapokuja swala la ugojwa tuweke mzaha pembeni na tujaribu kuheshimu faragha za watu. Sioni sababu za kupiga picha wagojwa, sioni kwanini magari ya wagojwa yapigwe picha na kufanya udhalilishaji. Kitu cha msingi sasa hivi ni kujaribu kujiridhisha kuwa tiba hiyo inamsaada kwa wagojwa au la! nafikiri hiyo ndiyo habari ambayo watanzania wanaisubiri kwa hamu kubwa "ukweli watiba itolewayo" si vinginevyo. Hawanzania wenye adabu na heshima zao hawahitaji kujua ni nani amekwenda huko. Tulinde jamani faragha za wenzetu
 
Mkuu kwani wewe unadhani serikali inafanya hivyo kujua kama dawa hiyo inacontents za kutibu tu au inaangalia pia kama hizo dawa hazina madhara kwa mtumiaji?
Kuna swala la kutibu na kuna swala la madhara kwa mtumiaji, serikali inaangalia madhara kwa mtumiaji na kama inazo hizo contents si vibaya zikafanyiwa kazi.
Kama serikali itaona ni maji ya kawaida na babu akadai ni mambo ya miujiza serikali haiwezi kufanya kitu, issue ni je hiyo dawa ina usalama gani kwa watumiaji?

Knowledge ndogo ya physiology na biochemistry niliyonayo inaniambia wanaweza kupata blood, urine na hata nywele samples na ku analyse kama kuna traces za vitu ambavyo kiscience zinajulikana kuleta madhara
 
Mi naona aibu kwenda coz ni mtu mzito sana halafu kwenda natamani sasa nifanyeje?
 
dawaaa....dawa....dawaaa....dawa! "kila mwenye mzigo mzito na aje kwangu, nami nitampumzisha" - JESUS! magonjwa sugu ni mzigo mzito sana, mchungaji wa loliondo naye anawapumzisha!
 
Muhimu ni wagonjwa kupona, kuna watu wameteseka na magonjwa for more than 10 years, wanachohitaji ni kupona kama kuna madhara hilo litakuwa ni suala lingine nalo litatuliwa kwa wakati wake
 
Soma tena thread yangu member!
Wao wangekua wastaarabu wangekubali wapokee unga.
Lakini hawakukubali.
Huoni ndio kuibiwa jua la saa sita!.
Hapo hata ukipewa maelekezo haitokusaidia ukikumbuka wao ndio wapo hapo jikoni.
Kesho unasikia Dr fulani amefanya utafiti na amegundua dawa fulani.
Sijui umetaka niwe-serious vipi?

Sasa huo unga watajuaje umechanganya mizizi gani? lazima waone kitu original.
 
Tanzanians must shun the supposed influence of superstition in matters of national interest. Recent studies have shown that belief in magic is widespread throughout sub-Sahara African countries and Tanzania is leading in these irrational beliefs. Nimeshangaa kumuona Mwenyekiti wa CCM mkoa wa kilimanjaro front page ya magazeti akibugia kombe la mitishamba. Any way hii ni karne ya 21 na sio stone age au Dark ages.

Sasa jamani kama imani za Watanzania ndo zilivyo wafanyaje? coz hata kipindi cha uchaguzi watu wapo tayari kuogas hata Barabaranui kuhakikisha wanashinda uchaguzi,
We mwenyewe uliona Mjomba alipo anguka Pale Jangwani akasema Mchawi wangu ameshindwa, ina maanisha Kama Raisi anaye tuongoza ni muaminifu wa Ushirikina what abt us? na ndo mumemchagua nyinyi
 
Nilijua kua hawa majuha watafanya hivyo baada ya wao kupata dawa.
Basi tena tumain limepotea kwa wagonjwa
Kama ni kweli basi angalau, at least kuna watu bado wana akili timamu serikalini.

kuna thread hii na huko members wametoa maoni haya.
https://www.jamiiforums.com/habari-...ya-babu-loliondo-agoma-dawa-yake-kupimwa.html
Kufuatia ujumbe uliotumwa na wizara ya afya na ustawi wa jamii kwenda Loliondo kwenda kuangalia uhalali wa matibabu yanayo tolewa na babu inasemekana babu hakuwa tayari kuruhusu wataalam hao kuipima dawa yake. ndugu wanajamii je hiyo imekaaje?

Wawachukue wagonjwa wa ukimwi, kisukari na kifua kikuu kama "sample" wawapeleke na baada ya kunywa wawapeleke maabara kupima kama bado wanasumbuliwa na magonjwa yao. Hili halihitaji PHD kulithibisha, kupima dawa ni kutaka kuiba formular ya Babu bila idhini yake.

Hii ni sawa, lakini kama serikali inabidi/ni muhimu ijiridhishe pia kwamba dawa hiyo licha ya kuponya kama inavyodaiwa haina madhara mengine makubwa kwa mtumiaji (sasa na baadae). kumbuka ni maelfu ya watu wanapatiwa tiba hii na wengine wanatolewa mahospitalini kwenda huko kwa ajili ya tiba, sasa kama ina madhara ni watu wengi wataathirika na serikali ina jukumu la kulinda afya na maisha ya watu wake.

Kwa haraka mawazo mengi yanayotolewa ni mazuri...serikali haijapiga marufuku kama nimeelewa tamko hilo la serikali na mchango wa SMU unatoa mwanga zaidi katika kushughulikia suala hili. Serikali pia ina wajibu kulinda afya za raia, pia kuhakikisha mazingira salama huko kwa babu ambako sasa kuna mkusanyiko mkubwa wa watu na uhaba wa vyoo na huduma nyengine.

Kama nia ya serikali ni pamoja na kuhakikisha mazingira ya kwa babu yanaboreshwa ili watumiaji wa huduma ya babu wasijekumbwa na maradhi ya mripuko si jambo baya..kusaidia pia katika kuweka utaratibu wa kupunguza mkusanyiko mkubwa wa watu kwa wakati mmoja.
 
Bible ina-instruct ...ya kasali mpe kaisali! So babu anapaswa kama kweli ni wa mungu kuwaruhusu wanasayansi waendelee na kazi/wajibu wao.
Na ikumbukwe mungu ndeye greatest and 1st sceintist. Ndivyo alivyo na hatobadilika!
So mambo yake yote yatabaki kuwa na scientific prove! Amesema tuishike sana elimu sasa huyu anayesema hii dawa haiwezi kuchunguzwa katoka wapi?
 
watibishe basi ili tupate nafasi nzuri ya kuanzia mgomo mama lao. Wamehisi babu ni Cdm sasa wanaanza upupu wao. Tena nawaambieni , huyo aliyempa babu nguvu ana mamlaka kulioko Wakwere wote na majuha yao.
 
ha hahaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!

mkwere nae nasikia ataenda kuzindua jiwe la shule ya msingi huko loliondo!!!

mmhh!! nahisi lbd anataka apate gia ya kumpitia babu apate kikombe kimoja.

Ulikuwa hujui alisha kwenda kuangalia unyayo? bado mtoto wa mkulima tu
 
Ndugu yangu usemayo ni sawa lakini ili huduma yoyote ya kiafya iweze kuwa authorized mahali popote duniani ni lazima ithibitishwe na mamlaka husika ya afya,zipo traditional medicine therapy nyingi duniani kama kule china,india hata ulaya lakini zote hizi zinakuwa zimepata baraka kutoka mamlaka husika,hata hapa nchini kwetu regional hospitals na referral hospitals zina vitengo vya wataalamu wa tiba asilia na wote wana baraka kutoka wizarani,hivyo wizara inafanya hivyo ili kujiweka on the safe side na vile vile ni kuhakikisha kuwa hiyo dawa iko salama isije wadhuru consumers baadae kwa sababu dawa uliyokunywa leo unaweza kuona madhara yake even 5-10 yrs later,mimi nafikiri sio jambo baya ili mradi huo utafiti ufanyike kwa haraka na ikithibitika dawa ni nzuri na haina madhara babu aendelee kutoa huduma.
pumbafffff kabisa hii serikali badala ya kushugulika na masuala ya msingi wameshaona ajenda ya babu wa loliondo ni ishu, mpeni uyu babu sapoti aendelee kutoa huduma yake, mmeshaambiwa kuwa hii dawa inaenda na suala la imani asa utafiti gani mnaoutaka??? kwenye makanisa kibao waumini wanafanyiwa maombezi na kupewa maji kama ishara ya dawa na kupokea uponyaji, je huwa mnaenda kuwafanyia utafiti??? wajinga sana nyie wote hapo wizara ya afya
 
Back
Top Bottom