Babu wa Loliondo afungiwa kwa muda kutoa huduma...

Huyu Mzee Mungu ambariki, kazi yake inaonyesha alivyo mtiifu kwa Mungu.....
Wanaomlaani, Mwenyezi Mungu awaadhibu.
...


Amen! mimi ndugu zangu wawili wamepona yani nakosa maneno ya kusema, Mungu ni Mwingi wa Rehema na kupitia Babu wengi watapona. Wanoamini waendelee kuamini na wasio amini wakae kama walivyo!
 
waanagalie tu wasije wakasababisha babu akakosa nguvu ya kuendelea kutoa dawa tena
 
Aisee ndo yamekuwa hayo tena? Kwa kweli hizi ni taarifa mbaya kwa watu ambao walikuwa wamejiandaa kwenda kule. Haf Mambo ya Mungu hayawezi kuthibitishwa na sayansi, hapo ndo shetani sasa anaanza kuingilia. Nina imani atashindwa na kulegea.
 
Sasa dawa ambayo imeshapikwa na Babu aimwage au? nini kuhusu hao wanachi waliokopa laki na nusu za kufika hadi huko halafu warudi watupu na magonjwa?

Serikali inaleta masihara kama hii habari ni ya ukweli.
 
Utafiti huo utachukua miaka mingi, na huenda matokeo yasitolewe hadharani..
 
Sasa dawa ambayo imeshapikwa na Babu aimwage au? nini kuhusu hao wanachi waliokopa laki na nusu za kufika hadi huko halafu warudi watupu na magonjwa?

Serikali inaleta masihara kama hii habari ni ya ukweli.
Wanataka machafuko yatokee........
 
utafiti wa nini wakati watu wamepona? Au utafiti utazuia asitoe huduma? Upuuzi mtupu . Wenye biashara za dawa wameanza upuuzi wao. Waashindwe na walegee
 
Hivi hii serikali iliyoshindwa majukumu yake inahusikaje na shughuli za babu wa Loliondo? Jamani ama kweli tunashida sana nchi hii serikali ya marufuku imetoka wapi? yaana baada ya kusaidia kuboresha mazingira watu wapate huduma wao wanapiga marufuku? hivi wananchi ni mabwege kiasi hicho mbona hawapigi marufuku hospitali yao ya ocean road inayoendelea kuua watu wasio na hatia kila siku hebu tuamkeni watanzania wenzangu hawa majuha kalulu tukiwaachia tutaigia nao msikitini
 
Wakati utafiti ukiendelea viongozi watakuwa wakienda kwa siri kutibiwa , wengine watakuwa hawaruhusiwi kufika huko.
 
Yule babu wa Loliondo aliyepata umaarufu kwa muda mfupi kutokana na dawa yake kutibu magongwa sugu amefungiwa kuendelea ma kutoa dawa kwa wagonjwa na wizara ya afya,wizara imesema inataka kuifanyia utafiti dawa hiyo pia wamemsauli mchungaji huyo mstaafu kuisajili dawa yake mamlaka ya chakula na dawa(TFDA). Source.Channel ten habari ya saa 7 mchana.

Siamini habari hii....kama ni kweli litakuwa jambo la ajabu kabisa itabidi huduma hata za maombezi pia zifungwe ili hadi zije kuthibitishwa.....
 
Kama ni kweli basi angalau, at least kuna watu bado wana akili timamu serikalini.
 
Alafu amesha sema hiyo dawa ukichemsha mwenyewe haitibu, yeye akitoka hapo kwenda kuwapelekea kwingine haitibu, mgonjwa asipoenda na kuipokea hapo yeye mwenyewe na kupewa na mikono ya babu haitibu so hiyo science itapima kitu gani hapo? But kiroho tunaweza ipima kwamba imani itakufanya wewe unyanyue mguu wako uende kule, unyenyekevu utakufanya wewe ukubali kuacha nyumba yako nzuri na magari na chakula huku ukiweka elimu yako pembeni umfuate babu asiye na jina wala elimu kwenye nyumba yake hiyo ndogo ya matope akakupe dawa inayoponya kwa neno alilopewa kwenye ndoto (Mungu mjanja maana alijua watamhonga babu awape upendeleo wachache wenye uwezo kwanza), but babu ni mtii huyu haongezi wala hapunguzi alichoambiwa (another character of a child of God)...so whats the healing power in that 'MUTI'...the word ofcourse which was given to babu by His God; who then is this God this is a spiritual question...Ukishahakikishiwa ndani ya dhamira yako na ukaipima kwa neno la Mungu tulilopewa (Biblia) ukaona halijapungua then umekiri uponyaji wahuyo mtoa ndoto and according to Babu ni Yesu maana yeye ni mchungaji...Kama kweli imo ndani yake basi ni neno ndilo linaponya hapo huo mti ni media ya kupitisha huo uponyaji kwani Mungu pia anajua cultural setting ya watanzania ni rahisi kuamini mti shamba/physical matter kuliko neno lakuambiwa...Hii ni based na analysis yangu mwenyewe na wala si ukristo nilionao lisije likatukanwa jina la Bwana yesu kwaajili yangu...

Then neno linasema kwa matendo yao mtawajua...kama kweli babu hapokei hata senti tano then yuko biblically correct kwamba umepewa bure na utoe bure..hapo anawaacha wenye dini kwa mbali sana...Tena neno la Mungu linasema God is not respector of person kila mwenye roho iliyotayari hupokea this is proved to both..babu aliyetamani kutibu hayo magonjwa (according to what is said in JF) na wale wote wanaoenda kunywa dawa ya babu huku wakiweka dini zao pembeni na kupokea uponyaji; this is also biblically proved kwamba Bwana Mungu wa majeshi ameleta wokovu kwa wote kwa myunani kwanza na kwa mataifa pia, again babu ni mtii hapunguzi wala haongezi neo sisi je tumeambiwa kila mwenye kulitaja jina la bwana na aache uovu je is this what we do?...niajabu sana wenye dini wameingia kwenye mtego wa kupeleka habari njema kwa wateja wao tu na kuiacha dunia ikiwaya waya kama machele...God promised if you wont take this good news to all nations then I will raise stones to do it on your behalf...so watumishi wajiulize mbona ukimwi bado unatesa dunia wakati wao wamebeba anointing kwenye makanisa huku watu wakiendelea kupukutika? Je yesu alikuwa mwongo aliposema mtapokea nguvu nanyi mtakuwa mashahidi wangu Galilea, Samaria na kwa mataifa yote? Ushuhuda wetu uko wapi? Je ni kipi hatukifanyi sawa? Babu is a challenge to the gospel we are preaching!

Felister,

1. Wagonjwa wenye shida ambao hawana nauli watafikaje kwa babu kama yeye peke yake
ndie anayetoa hiyo dawa na si mwingine?

2. Southern countries ndio zilizoathirika sana kwa ugonjwa wa UKIMWI, are you telling me all
those people should come to TZ to get this treatment from him ONLY?

3. Kama kweli hii dawa Mungu ndiye aliyemfunulia, vipi kuhusu wagonjwa ambao wanafia
njiani wakielekea huko Loliondo? Hawakustahili kupata hii dawa ili wapone?

4. How come we only hearing story from people but we havent actually see someone who got
healed, utasikia tu mtoto wa rafiki yangu, mama yake rafiki yangu, mjomba wangu
anayekaa mbeya etc?
 
Yule babu wa Loliondo aliyepata umaarufu kwa muda mfupi kutokana na dawa yake kutibu magongwa sugu amefungiwa kuendelea ma kutoa dawa kwa wagonjwa na wizara ya afya,wizara imesema inataka kuifanyia utafiti dawa hiyo pia wamemsauli mchungaji huyo mstaafu kuisajili dawa yake mamlaka ya chakula na dawa(TFDA). Source.Channel ten habari ya saa 7 mchana.
Nchi hii ina matatizo mbona za Shekh Yahya alipoamua kumwongezea ulinzi mkuu wa kaya wizara ya afya haikumuomba kuzifanyia utafiti kuona kama zitamdhuru. pia mabango ya waganga yamejaa jiji la Dar hakuna anayefuatilia au kwa kuwa kwenda Loliondo kuna allowance ...
 
huo mti kama unajulikana si wachukue sample waifanyie utafiti ina kitu gani? tatizo kuna nguvu za maombi ndio dawa ifanye kazi sasa hapo sijui wizara ya afya ina role gani.. kwa kua wanatumia kodi zetu kwa ajili ya hiyo safari cha maana waweke vizuri mazingira ili kujiandaa kwa ajili ya magonjwa ya mlipuko ambayo yanaweza kulipuka huko kutokana na uwingi na mikusanyiko wa watu
 
hivi hawa wizara ya afya wana nini, mbona siwaelewi, kama wagonjwa si wao, wao wanataka kufanya utafiti, halafu iweje, lini watamailza utafiti...???? jamani wawaache watu watibiwe, KILA MTU ANAENDA KWA BABU KWA HIARI YAKE, kama vile anavyokwenda kweny zahanaTi au kituo cha afya kingine, , ni hari ya mtu, WAACHENe WANANCHI KWATIBIWEEEE, grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr
 
Mkuu kuchukua wagonjwa eg wa HIV na kuwatumia kwenye majaribio kama wameponywa na hiyo dawa ni kinyume na medical ethics,utakuwa unaingilia haki ya privacy sharti hiyo dawa ipatikane ifanyiwe majaribio kwanza,hapo imekaaje?


kwani watawalazimisha? Si watafute ambao wako tayari kufanyiwa vipimo? Kama wanaweza kushuhudia wamepona kwenye vyombo vya habari wataacha ku colaborate na serikali?
 
Jamani mi nimeona vitu lakini hiki cha loliondo kimenishtua sana, kwasababu Mzee huyu ni wa ajabu na ameweza kujipatia njia nzuuurii ya kutafuta Pesa bila kutumia unyang'anyi wala Ndumba, bali kwa kutumia Akili yake.
Hakuna uthibitisho wa kisayanxzi kwamba dawa hiyo inaponesha, na kimachoshangaza Eti Dawa hiyo huponi ukichota mwenyewe mpaka achote kwa mkono wake.
naomba tuwege makini, na naomba uthibitisho ili na mimi niende bana

Eti wadau ni njia ya kutafuta Ela au Dawa kweli?
 
Hivi hii serikali iliyoshindwa majukumu yake inahusikaje na shughuli za babu wa Loliondo? Jamani ama kweli tunashida sana nchi hii serikali ya marufuku imetoka wapi? yaana baada ya kusaidia kuboresha mazingira watu wapate huduma wao wanapiga marufuku? hivi wananchi ni mabwege kiasi hicho mbona hawapigi marufuku hospitali yao ya ocean road inayoendelea kuua watu wasio na hatia kila siku hebu tuamkeni watanzania wenzangu hawa majuha kalulu tukiwaachia tutaigia nao msikitini

Mkuu.
mchango wako poa tu lakini umeutia kasoro hapo penye rangi ya buluu. Katika hao wanaokwenda kwa babu wamo wanaokwenda msikitiki. Pia ni wananchi na watanzania wenzako.

Naelewa kuwa maamuzi mengi ya serikali iliyopo hivi sasa yanaudhi na yanaumiza wananchi lakini huwatendei haki hao wanaoingia msikitini kwa kauli yako. Wao pia wanaumia na maamuzi ya "hawa majuha". Na kauli yako hiyo ni kiashiria cha ubaguzi au unahubiri mgawanyiko wa wananchi wenzako?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom