Babu Seya kuachiwa huru na Kikwete?

Babu Seya kuachiwa huru na Kikwete?

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
27,195
Reaction score
27,810
CHOZI LA BABU SEYA BADO LAITESA SERIKALI YA CCM; BABU SEYA AMWAGIZA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI KWENDA KUMUOMBEA MSAMAHA KWA JK.

Kwa mujibu wa KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA MWAKA 1977, SURA YA PILI, SEHEMU YA KWANZA, IBARA YA 45, inampa Rais wa Jamhuri ya Muungano mamlaka ya kutoa msamaha kwa mtu yeyote aliyepatikana na hatia mbele ya mahakama kwa kosa lolote, ama bila ya masharti au kwa masharti, au kumwachilia kabisa mtu huyo asitimize kabisa adhabu hiyo au kuibadilisha adhabu yoyote aliyopewa mtu yeyote kwa kosa lolote au kufuta adhabu yote au sehemu ya adhabu yoyote.

Nguza na mwanaye Papii walitoa ombi la kusamehewa na kuachiwa huru kupitia wimbo wakati wakitumbuiza katika maadhimisho ya Siku ya Magereza yaliyofanyika Chuo cha Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam tar 20/06/2014.

Ombi hilo waliliwasilisha kupitia kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe aliyekuwa mgeni rasmi kwenye sherehe hizo ambapo Babu Seya na mwanawe, Johnson Nguza (Papii Kocha), walitumbuiza wakiwa na Bendi ya Wafungwa. Walimwomba Waziri Chikawe kufikisha ombi lao kwa Rais Kikwete. Chikawe akijibu ombi hilo alisema “Mtu akishatumikia kifungo kwa miaka saba au 10 gerezani nina hakika kama ana moyo na nafasi ya kuacha, atakuwa amebadilika hivyo anaweza kupewa msamaha.”

Maswali ya kujiuliza ni:
1.Je, kwa nini jambo hili linamlenga sana JK badala ya mahakama iliyotoa hukumu hiyo??
2.Je, kwani Babu Seya ndiye mfungwa pekee wa maisha katika magereza ya Tanzania? Kama wapo wengine, je, wao wameridhika na adhabu hiyo au hawana pa kusemea?
3.Je, rais ataweza kweli kutumia mamlaka aliyopewa na katiba kuwaachia huru watu hawa? Sheria nyinginezo na historia ya Tanzania zinasemaje kuhusu mfungwa wa maisha kuachiwa huru kwa msamaha wa rais?
4.Ikumbukwe katika kampeni za uchaguzi za mwaka 2005 JK aliahidi kuwa kama atashinda kiti cha urais basi suala hili la Babu Seya atalipa kipaumbele zaidi, je, alifanya ivyo? Na kwa nini Babu Seya pekee ndio apewe kipaumbele na sio wafungwa wengine?

Mimi binafsi nimekosa majibu ya maswali hayo, naomba mwenye majibu ya uhakika tushirikishane.
:yield:
 
Mimi huwa naamini kila jambo hutokea kutokana name sababu Fulani,ni mipango ya mungu, mungu hakumuumba mwanadamu aje anyanyasike ktk ulimwengu,so neema inakaribia kwa Babu Seya, eee mungu mnusuru na Mapito ya dunia hii
 
Kuna kitu kimefichika katika suala hili sio mambo ya sheria tuu. Hata wakati wa kesi ya uhaini hatukusikia jamii ikimtaja sana Rais kuhusu kuwasamehe wahusika waliokuwa wanatumikia adhabu kama hii. Kuna siku ukweli utakuwa wazi
 
Mjepo rekebisha lugha yako lasivyo na wewe utaenda huko jela... Hakuna kiswahili kisemacho "ulaiyani" sema uraiani.. Au keyboard yako aina R!!


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mjepo rekebisha lugha yako lasivyo na wewe utaenda huko jela... Hakuna kiswahili kisemacho "ulaiyani" sema uraiani.. Au keyboard yako aina R!!


Sent from my iPhone using JamiiForums
Mkuu mbona iko poa tu ntakuchapa kwa uchokozi wako.
 
Ningekua mimi nisingetumbuiza ningekataa,narudia tena kama ningekua mimi binafsi

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
hivi wale watoto waliobakwa wako wapi sasa hivi?

Wameshazaa Kama Siyo Kujifungua Na Namkumbuka Mmoja Wao Alikuwa Anaishi Karibu Na Kwa Marehemu Mama Yangu Mdogo Pale Sinza Jirani Kabisa Na Maeda Sijui Meeda Bar Jina Lake Nalihifadhi Kimaadili Ila Mimi Binafsi Nilimfanyia Mahojiano Ya Kiaina na Alikuwa Ananiheshimu Mno Na Alinizoea Pia Na Alichoniambia Ni Kwamba Si Yeye Wala Wale Wenzie ILA Kilichotokea tu Ni Kwamba Suala Lote Lilitengenezwa Na Wazazi Wao Walipewa Chochote Kitu Pamoja Na Vitisho Juu Na Hata Hadi Sasa Wanafuatiliwa Na Wanachungwa Mno. Alichoniambia Ni Kuwa Zile Alama Nyekundu ktk Vyupi Zao Wala Hazikuwa Damu za Kuingiliwa Bali Ilikuwa Ni Mchanganyiko wa Tomato Source na Kemikali Nyingine Kwa Maadili Ya Kijasusi Siwezi Nikaitaja Hapa. Habari Ndiyo Hiyo ILA Hili Suala Limekaa KISIRI na KIHATARI Sana Kushinda Hata Ile Ajali Ya Jana Pale Lugalo ( Supa ). Ushauri tu au Ombi Haswa Kwa Wanaume Wenzangu Hebu TUACHE BIFU ZA KISHAMBA, KIJINGA na Za KITOTO ZA KUMKOMOA MWANAUME MWENZAKO KISA TU " AMEKUKANYAGIA " AMA DEMU WAKO tu au MKEO. INASIKITISHA na INAUMA Sana. Mademu au Wanawake Wenyewe Wa Kibongo Hawana Dhamana.
 
Back
Top Bottom