Baba yangu aliniambia hanikumbuki, niliumia sana

Baba yangu aliniambia hanikumbuki, niliumia sana

Huyo aliekupeleka kwake nae alikuwa hajakusaidia kikamilifu yeye kama mtu mzima.

Alijua kabisa baba yako huyo ana mke na wewe umemwambia hujawahi kuonana na baba yako, hivi hakujiongeza kufaham kwamba wewe sie mtoto wa mke anaeishi nae na kwamba wake za watu wengi hawapemdi habari za watoto wa nje ya ndoa?

Ilibidi tu akupeleke hata karibu na ofisini kwake huko amwite wakati wewe upo kasehem flan hivi (wafanyalazi wenzake wasikuone huemda wakasafirisha maneno kwa mkewe), hapo hali ingekuwa na afadhali, na wala asingekupeleka nyumbani bali angekulipia hata hoteli ukae hapo siku 2 mjuane zaidi na hata kukupeleka kwa ndugu zako ujuane nao.

Kumbuka mtoto wa nje ya ndoa ni siri kama ilivyo kwa michepuko, ni hatari kuigonganisha na wake wa ndoa.

Pole sana lakini kosa lipo kwa aliekupeleka, Ila hata mama yako pia yeye kama mtu mzima ilibidi akupe kidogo muongozo kwamba ufanye juu chini uonane na baba yako yeye kama yeye anapokuwa peke yake, sio kupitia nyumbani kwake ambako ana mke.

Ulipoenda huko ni kwamba kwa ufupi tu ulikuwa umetia mchanga kwenye kitumbua, ndoa ya huyo baba yako ilikuwa hatarini, Ilibidi tu wewe uondoke, hakukuwa na namna hapo, ila labda tu kosa kubwa ni baba yako kuto kukutafuta baada ya hapo ila hatuwezi jua huendwa alipigwa biti zito mno angefanya hivyo.

Yote kwa yote ulienda kuzua kizaa zaa tu huko, ilibidi upewe muongozo ama kusaidiwa kukutana na huyo baba yako kwa usiri na ninakuhakikishia mambo yangekua yamenyooka.
 
Mkuu, katika maisha na mahusiano kuna Mengi sana. Kwa sababu wewe ni mwanaume kuna siku utafahamu Mengi sana.Ukweli ni kwamba baba yako anakukumbuka sana ila namna ulivofika kwake ndo tatizo.Utaratibu uko hivi. Ulitakiwa Upelekwe na Mtu Mzima, Mjomba au yeyote tena afahamu hasa uhusiano wa baba yako na mama yako ulikuaje.

Kablya ya wewe kumuona alitakiwa aelezwe in details kisha aridhie ndo muonane.Sasa umetokea kama baharia tena ukute we ni mdogo kuliko watoto wake wakubwa unafikiri kesi uliyoacha hapo nyumbani ni ndogo? Anakukumbuka hata leo. Ipo siku mtakutana hata kama ni wakati wa mazishi yake.
 
Very touching, mkuu pambana na baraka za Mungu ziwe juu yako, ukifanikiwa mbona huyo Anayesema hakukumbuki atakutafuta mwenyewe. Shida ni kwamba sasa hivi haoni faida yoyote atapata kutoka kwako zaidi ya yeye kukugharamia na pengine kuongeza migogoro kwenye familia yake.
 
Kaka ndugu zako watakukubali ukiwa kwenye status nzuri ya maisha. Haya maisha sometimes hayapo fair. Ww tafuta pesa ipo siku watakutafuta wao. Haupo pekeako unaepitia haya kwahio usichukue mrengo wa kuliona kama tatizo kubwa ama kizingiti. Mimi najua watu wengi ambao wametafutwa na Baba zao tayari wakiwa na zaidi ya miaka 30 ama 40. Tayari wakiwa na maisha mazuri sana.
 
Pole sana, ninachojua wazazi hata mkosane kiasi gani ugomvi hauwahusu watoto. Cha muhimu ulishafanya juhudi za kumtafuta, kama mzazi hata kama approach ulotumia haikuwa nzuri alipaswa kutafuta namna ya kukutafuta pia.

Hivyo kwakuwa alikukana basi tulia tu endelea na maisha yako na kama wewe ni mwanaume uichukue kama fundisho, usije ukarudia huo ukatili tena.
 
Kufupisha tena bila kuficha baba ni mpumbavu sasa yaani anamtosa mtoto wake kisa kuogopa mke. Sisi wanaume wa Afrika huwa tunaoa sio kuolewa.

Huenda kuna sababu nyingine iliyo mfanya huyo mzee amkatae mtoto ambayo ni kubwa kuliko ya kumuogopa mke wa sasa.

Ninampa pole tu kijana kwa yalio mtokea tena wakati wa kipindi anahitaji msaada.
 
Kaka ndugu zako watakukubali ukiwa kwenye status nzuri ya maisha. Haya maisha sometimes hayapo fair. Ww tafuta pesa ipo siku watakutafuta wao. Haupo pekeako unaepitia haya kwahio usichukue mrengo wa kuliona kama tatizo kubwa ama kizingiti. Mm najua watu wengi ambao wametafutwa na Baba zao tayari wakiwa na zaidi ya miaka 30 ama 40. Tayari wakiwa na maisha mazuri sana..
Tayari nipo katika umri huo mkuu na ninashukuru maisha yanaenda vizuri.
 
Pole mkuu, ila wanaume mngekua na nyinyi mnabeba mimba na kuusikia uchungu mimi nahisi haya maswala yangekua yanapungua.
Ungeishia kwa hayo maneno wawili ya kwanza (Pole mkuu) ingetosha sana kumfariji. Hayo yaliyofuata hayana msingi wowote na wala hayamsaidii katika uzi huu. Umeangalia mno upande mmoja. Mara nyingine chanzo kinaweza kuwa wabeba mimba; usilifumbie macho hilo. Nina ushahidi juu ya hilo.
 
Asante kiongozi, sasa nimeshakuwa mtu nipo na family na family yangu ipo na furaha. Sema mama alishafariki
Pole Sana Kwa Mama Kufariki
Nina Jamaa Yangu Yupo Dar es Salaam
Baba Yake Alioa Mke Mwingine
Jamaa Alipokwenda Kumtafuta Hakupata Msaada Wowote
Nikamshauri Ukiwa Na Family Usifanye Aliyoyafanya Baba Yako
 
Back
Top Bottom