Baba kususa kuhudhuria harusi ya mwanae

Baba kususa kuhudhuria harusi ya mwanae

Hakuna sababu ya kumlaumu mzazi , lazima kuna sababu ya msingi ambayo yeye hakubaliani nayo kuhusu ndoa hii! Kuwatukana wazazi wenu kuwa wamefullia ni utovu wa maadili mema, mtakuja pata laana bure!!
 
Tatizo ni kwamba wazee wengi hawatimizi majukumu yako (wanakwepa) sasa watoto wakifanikiwa na kuamua kuoa (kuachana na usela) mzee anaona amedharauliwa na kuweka mgomo baridi. Sasa nyie wazee endeleeni na misuso ya kijinga vijana watawaacha hapo na upuuzi wenu. MTASUSA SANA.
 
Kwetu sisi kama familia mchango sio pesa tu. Kuwa pamoja, kushauriana na kufarijiana ni muhimu zaidi. Kuna mtu tunamthamini mno, hajawahi kuchangia mgonjwa, elimu wala harusi kwa pesa bali kwa uwepo wake.

tukisalia kwenye mada. Michango haiwezi kunichosha. Wana dharau na ni wabaguzi. Odcoz hawakuwahi kuwa na jeuri ya kunidharau mimi, lakini dharau kwa wanafamilia wengine ndio ilikuwa kero yangu.
Hukuchanga sababu wenyewe hawatoi ushirikiano/ hawakuchangia kwenye harusiyako au ni kwasababu ulichoka na michango?
 
Mimi huwa naita 'kuweka mguu chini' ili watu wasikuchezee. Ila kuwa muangalifu kaka, usije ukawaadhibu wana kwa uovu wa baba zao. Tafuta mahali pa kuhit umlenge mhusika bila kuumiza wengine.

pole sana, sikiliza mtima wako na uwe na amani
my sister hili la kwangu ni more than that, sijawahi kuishi maisha ya beef ila nafundishwa kwa mara ya kwanza.

kuna vitu havivumiliki ila tu kwa sababu mambo yetu serious wengine huwa tunabaki nayo moyoni hatuyaleti hapa kwa sababu hakuna wa kuelewa chanzo cha haya yote, nasikitika sana nafundishwa roho mbaya ambayo muhusika/wahusika haitawahathiri bali innocent people ndio watakuwa wahanga wa hili.
 
ni upuuzi wa kishamba kususia harusi ya mwanao (wa kumzaa) hata kama angekuwa kafanya nini. Kwa kuitwa Baba alipawa kubeba majukumu halafu kama ana ishu aiseme baada ya tukio (Harusi)
 
Huyo mzee hana akili hata kidogo Baba ndio Mungu wa dunia. Maadam mzazi alitimiza wajibu wake wa kumzaa na kumtunza hadi akawa mtu mzima kama ukimuona mjinga sawa. Lakini mzazi hawajibiki kusapoti jambo ambalo yeye analiona ni la kijinga sababu tu mtoto anatalika. Hivi wangekuwa wako ulaya na mtoto anafunga ndoa ya jinsia moja na baba anapinga bado ungemlaumu? Maana pia kwa wazungu ni kitu cha kawaida kufunga ndoa ya jinsia moja. Kuna tofauti ya kuoa na kuokotana kwa ajili ya kusukuma. Ndoa ngapi zinazofungwa na kuvunjika kabla hata ya miezi sita.
 
Wazazi lazima tujue wajibu wetu kwa wazazi wetu regardless of any situation maana hivi unaposusa harusi ya mwanao unataka nani ndo aende?
 
Pole sana mhusika ila ni lazima kuna tatizo kubwa katika hii familia.
 
hapo watulie hao maharusi wapige kimya kabisa wasiongee na huyo mzee labda kwa ishu ya ugonjwa ama kifo
 
Huyo mzee ana lake jambo si bure aisee yaani bila shaka kafulia sasa anaona anadharauliwa
 
Unafikiri ww utabaki kijana? Utazaa na mwanao uliyemhangaikia kwa kila kitu anakufanyia utumbo sasa akikuita kwenye pari yake utaenda?
Tatizo ni kwamba wazee wengi hawatimizi majukumu yako (wanakwepa) sasa watoto wakifanikiwa na kuamua kuoa (kuachana na usela) mzee anaona amedharauliwa na kuweka mgomo baridi. Sasa nyie wazee endeleeni na misuso ya kijinga vijana watawaacha hapo na upuuzi wenu. MTASUSA SANA.
 
Kamwe baba hawezi kukataa jambo jema kama ndoa ya mwanae! Possibly kuna smth wröng!
 
huyo mzee bazazi kweli kweli hata kama mtoto alikosea adhabu si kususa kwenda kwenye harus yake kama alikualika. mengine mnaweza kumalizana baadae kupitia vikao vya familia. Ona sasa mtoto kaoa je umefaidika nini kwa kutokwenda?
 
hao wazee sometimes wanazingua wengi wao ni wastaafu sasa hana hela kama zamani, so kila kitu anaona amedharauliwa, matokeo yake misuso holela kama hiyo
 
Hii inanikumbusha Harusi ya rafiki yangu ambaye Baba yake hakufika ukumbini kwenye sherehe na wala kanisani hakwenda. Ilibidi tuwadanganye wageni waalikwa kwamba Baba alikuwa safari na wakati wowote ataingia, tukitarajia labda angekuja. Mpaka sherehe inaisha saa 6 usiku hakujitokeza. Angalau tuliijua sababu ya kutokufika kwake, alifungiwa ndani na mkewe kwani baba aliisha achana na Mama wa Bwana Harusi. Mke wa sasa wa mzee alijua hiyo ni nafasi ya mzee kukutana na mkewe wa zamani akaamua kumfungia ndani wakati yeye yuko nje ya nyumba na funguo.

Wivu mwingine mbaya sana.

Tiba
 
Inauma kwa kweli lakini maisha inabidi yaendelee. Hao maharusi washikamane kwa kweli wajue baba hayupo upande wao so wakipambana wajue ni wao peke yao. Lakini ipo siku huyo mzee atakuja kujua kosa alilofanya.
Inawezekana pia kuwa mwenye Kosa ni kijana.
 
Hii inanikumbusha Harusi ya rafiki yangu ambaye Baba yake hakufika ukumbini kwenye sherehe na wala kanisani hakwenda. Ilibidi tuwadanganye wageni waalikwa kwamba Baba alikuwa safari na wakati wowote ataingia, tukitarajia labda angekuja. Mpaka sherehe inaisha saa 6 usiku hakujitokeza. Angalau tuliijua sababu ya kutokufika kwake, alifungiwa ndani na mkewe kwani baba aliisha achana na Mama wa Bwana Harusi. Mke wa sasa wa mzee alijua hiyo ni nafasi ya mzee kukutana na mkewe wa zamani akaamua kumfungia ndani wakati yeye yuko nje ya nyumba na funguo.

Wivu mwingine mbaya sana.

Tiba

Huyo mzee nae mjinga hajitambui au kalogezewa wanasema.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom