Baba Diamond Ashinda Njaa

Baba Diamond Ashinda Njaa

Hahahaaa!watu miaka michache ile ilopita walikua wanahustle..Wanaakka asubuhi wanawaza leo tunakula nini?? diamond na mamake wanahangaika japo wapate hela ya unga na dagaa wale wasavaivu hapa mjini..Walikua walikua wanaishi kwenye nyumba ya bibi yao tandale.Cjui kama sio huyo bibi kuwapa makazi wangelala wapi?diamond anaungua na jua kali la dar,Kachafuka mweusii kuuza mitumba wapate hela ya kula na mamake...Huku mzee kakumbatia wanawake wengine ndani ya nyumba yake hana habari..Ni mama diamond alikua na cheni yake ya dhahabu moja aloipebda sana akaenda kuiuza kwa sonara hela akmpa diaomnd aende studio akarekodi wimbo wake wa kwanza..Leo maisha yamebadilika unamuona wa maana!! nenda shamba kalime baba mungu kashakufunza!
Aione mzurimie hii
 
Mkuu, umeandika kwa hekima sana! Huyu Diamond, mimi nimeshamuona kama mpumbavu tu, kuna watoto
wa kiume wengine sisi hatuna baba (tunaumia) na kuna wengine walikosana na baba zao sana tu, na huwa wanawasamehe na kuwasaidia. Na kuna wengine walipoteana na baba zao kitambo huwa wanawatafuta
mpaka wanawapata na kama walishafariki huwa wanaumia
sana! Sasa huyu Diamond anamwacha baba yake bila ya msaada hivi ni kosa gani la mzee huyu ambalo halipaswi kusamehewa? Mzee anaishi maisha magumu, Diamond anajidai kutoa
misaada kwa watu baki bila ya kumjali baba
yake sasa ni huruma gani aliyonayo kwa watu baki kuliko
baba yake mzazi ambaye Diamond
bado anatumia jina lake katika majina yake
matatu. Basi kama Diamond hampendi baba yake, aache kabisa kutumia jina la baba yake, atumie jina la ukoo wa mama yake halafu huyu mama Diamond naye ni mtu wa majungu na huyu Diamond hata aende wapi huyo mzee ndio baba yake ni busara akamkumbuka!
Umenena vema mkuu,hata sisi baba yetu hakutusomesha na pesa alikuwa nayo lakini mama alikomaa tukasoma na baba akafulia akawa home tu tulimjali sana mpaka akafariki akituombea baraka tele
 
Nikubaliane na hoja ya Mshana Jr kuwa huyu mzee sasa ifike hatua aachane na magazeti maana anaidhalilisha familia na yeye pia.

Mambo ya familia yasiwe chanzo cha fedha kwenye magazeti alhali familia ikidhalilika. Afe na tai shingoni kama ambavyo alikula pini hadi kupelekea hali hiyo itokee.

Kwa Diamond pia hii si habari nzuri pia maana kila uchao hawa wana udaku kukuandika kuhusiana na hili jambo la baba yako haipendezi. Wakanye wasiingilie masuala binafsi ya familia yako. Ikikupendeza pia sahau yaliyotokea kati yako na mzee wako.

Inawezekana angekulea yeye usingekuwa tunayekujua leo. Sometimes shida tunazosababishiwa huwa ni elimu tosha ya jitihada na mafanikio yetu. Mchukulie kama wakala wa njia ya MIIBA ili kuifikia NEEMA.

Mungu akupe moyo wa ujasiri wa kusamehe na ikiwezekana uwe ni chanzo cha kusababisha Baba yako na Mama yako warudiane na kuishi pamoja. Hili linawezekana. Inapendeza sana kuwa na familia iishiyo pamoja kwa amani na upendo.

Safari kama hizi za nje zaweza kuwa sehemu nzuri ya kutafuta suluhu kati ya wazazi wako. Hutaamini ukijaribu kwa nguvu zote na maarifa yote kulifanikisha hili.

Kwa Mungu thawabu ni kubwa ukifanikiwa kulitenda hilo.
aya magazeti ya udaku yanampa pesa kdogo huyu mzee ili afunguke, huku ukweli wakiujua kwamba hakumsadia mondi kwa lolote
 
Mama yake anamuongeza sumu azidi kumtenga babaake,kama mama ana mchango mkubwa kuongea na mwanae amsaidie babaake
 
Umenena vema mkuu,hata sisi baba yetu hakutusomesha na pesa alikuwa nayo lakini mama alikomaa tukasoma na baba akafulia akawa home tu tulimjali sana mpaka akafariki akituombea baraka tele
Malipo ya dhambi ni hapahapa duniani alikula ujana wake bila kufikiria ana familia sasa hivi mtoto kapata ananza kujpendekeza na wala sio kwa Diamond pekee mifano iko mingi kama Memphis Depay alikimbiwa na baba yake akiwa mdogo kwanini sasa hivi amsaidie??
 
Huyu mzee Lofa kweli!Hana tofauti na Baba yangu!Baba yangu yupo,ila hakuwahi nilipia hata thumni ktk elimu yangu zaidi ya mjomba angu upande wa mama,halafu kesho niwe mbunge wa iramba kupitia chadema,ndio aje ajifanye ananijua?hatopata hata dala langu kudadadeki!
kaka umetisha
 
Huyu mzee hata hio kuumwa miguu naona kama anaZuga ili apate huruma.
Hii ni mfano kwa wanaume wanaowakimbia watoto wao!!
Mkuu usimlamu huyo Mzee, hafu WW Ni Kidume pia, huwezi kujua nini kilitokea mkuu kwenye mahusiano Yao! Vp Kama Mama alikua Tatizo, vp Kama Mama D aliwasakizia mimba Wanaume wawili?
 
Malipo ya dhambi ni hapahapa duniani alikula ujana wake bila kufikiria ana familia sasa hivi mtoto kapata ananza kujpendekeza na wala sio kwa Diamond pekee mifano iko mingi kama Memphis Depay alikimbiwa na baba yake akiwa mdogo kwanini sasa hivi amsaidie??
Memphis hataki kumsikia baba ake hata kidogo, wengine ni Charles taylor, paul ince , giggs , etc
 
Kinachomuumiza sio shida alizonazo bali ni kuona mama yake diamond anakula bata, tena amepanda ndege kabisa wakati walikuwa wakipigiana tambo nani mjanja baadae, hahaha, acha aisome namba.
 
Ali Kiba okoa jahazi saidia mzee kabla hajavunjika kabisa. Ila huyu mzee hajafanya poa kufuatiliwa na waandishi ni kawaida ila asingetoa ushirikiano wowote kwao ama kuliongelea kama alivyoyafanya Diamond. Na kikubwa hata akisaidiwa hatoridhika kwa tabia hii ataendelea kulalamika tu. Diamond ampe milioni hamsini mbele ya wana Habari kama anavyotaka kisha kila mtu aambae kivyake.
hiyo hela akipewa ndani ya miezi miwili hana kitu
 
Mkuu, umeandika kwa hekima sana! Huyu Diamond, mimi nimeshamuona kama mpumbavu tu, kuna watoto
wa kiume wengine sisi hatuna baba (tunaumia) na kuna wengine walikosana na baba zao sana tu, na huwa wanawasamehe na kuwasaidia. Na kuna wengine walipoteana na baba zao kitambo huwa wanawatafuta
mpaka wanawapata na kama walishafariki huwa wanaumia
sana! Sasa huyu Diamond anamwacha baba yake bila ya msaada hivi ni kosa gani la mzee huyu ambalo halipaswi kusamehewa? Mzee anaishi maisha magumu, Diamond anajidai kutoa
misaada kwa watu baki bila ya kumjali baba
yake sasa ni huruma gani aliyonayo kwa watu baki kuliko
baba yake mzazi ambaye Diamond
bado anatumia jina lake katika majina yake
matatu. Basi kama Diamond hampendi baba yake, aache kabisa kutumia jina la baba yake, atumie jina la ukoo wa mama yake halafu huyu mama Diamond naye ni mtu wa majungu na huyu Diamond hata aende wapi huyo mzee ndio baba yake ni busara akamkumbuka!
Kwenye issue Kama hizo Mama anafurahi Tu, tena anazidi kumwaga sumu za uongo! Huwezi kujua nini kilitokea wakati ule, busara ya kawaida ya Mwanaume, Diamond angemsaidia Baba yake!
 
Diamond amfungulie huyu mzee mashtaka ya kumtelekeza utotoni akale ugali wa bure jela kama shida ni njaa...
 
Kama kuna mzazi juha huyu jamaa anashika namba moja...mzazi mwenye kujitambua hawezi kukubali huu upuuzi wa kuhojiwa kwenye gazeti la udaku mambo binafsi yanayohusu familia yake
Huu ni upuuzi na upumbavu wa kiwango cha juu mno
Hivi kalipwa bei gani?
Hivi anajua jamaa wametengeneza bei gani kupitia hiyo habari
Huyu hajitambui na atafakari alipokosea kuliko kuja kulialia kwenye vyombo hovyo vya habari...huku ni kujidhalilisha
Yeye alitoka nduki sasa watoto nao wamemjibu kiukweli si mtu wa busara kama ni mbinu hii ya global kaisha itumia mara nyingi imemsaidia vp?kisha anaoneka hata anavyoongea ni mtu flan wa kunywesha sana.
 
Nikubaliane na hoja ya Mshana Jr kuwa huyu mzee sasa ifike hatua aachane na magazeti maana anaidhalilisha familia na yeye pia.

Mambo ya familia yasiwe chanzo cha fedha kwenye magazeti alhali familia ikidhalilika. Afe na tai shingoni kama ambavyo alikula pini hadi kupelekea hali hiyo itokee.

Kwa Diamond pia hii si habari nzuri pia maana kila uchao hawa wana udaku kukuandika kuhusiana na hili jambo la baba yako haipendezi. Wakanye wasiingilie masuala binafsi ya familia yako. Ikikupendeza pia sahau yaliyotokea kati yako na mzee wako.

Inawezekana angekulea yeye usingekuwa tunayekujua leo. Sometimes shida tunazosababishiwa huwa ni elimu tosha ya jitihada na mafanikio yetu. Mchukulie kama wakala wa njia ya MIIBA ili kuifikia NEEMA.

Mungu akupe moyo wa ujasiri wa kusamehe na ikiwezekana uwe ni chanzo cha kusababisha Baba yako na Mama yako warudiane na kuishi pamoja. Hili linawezekana. Inapendeza sana kuwa na familia iishiyo pamoja kwa amani na upendo.

Safari kama hizi za nje zaweza kuwa sehemu nzuri ya kutafuta suluhu kati ya wazazi wako. Hutaamini ukijaribu kwa nguvu zote na maarifa yote kulifanikisha hili.

Kwa Mungu thawabu ni kubwa ukifanikiwa kulitenda hilo.
sasa huyu mzee atajifunza nn ? yaani aitekeleze familia halafu aitwe aje kula bata kwa kuitelekeza hiyo family ?
 
Naomba kuuliza, ni jukumu la mtoto kumtunza mzazi wake au ni jukumu la mzazi kumtunza mwanaye aliyemleta hapa duniani kwa raha zake? Tuache fikra mgando, si jukumu la Diamond kumhudumia baba yake ila ni hisani kwa Diamond kumhudumia baba yake. Na hii iwe fundisho kwetu sote, tusiwategemee watoto mwache naye ana vipaumbele vyake.
yes, point
 
Back
Top Bottom