Baba Askofu Munga: Akili na hekima. Corona sio sawa na Wapinzani

saidi kindole

JF-Expert Member
Sep 21, 2012
310
792
Wakati huu dondoo kubwa ya taifa na ambayo serikali yetu inaipa msukumo mkubwa ni mapambano dhidi ya kirusi corona. Mapambano haya hayana mzaha wala kebehi na yanadai umoja na mshikamano wa kitaifa. Usemi wa Ndg. Polepole kwamba corona ni sawa na wapinzani ni lugha ya mtu anayeligawa taifa katika kipindi hiki kigumu.

Malezo yake mengine juu ya corona na madhara yake sina shida nayo. Bali kauli hii ya kebehi na kugawa watu katika makundi ya kisiasa wakati huu inamuonyesha yeye ni mtu wa jinsi gani. Kauli hiyo japo ya maneno machache imechujua hata mambo mengine aliyozungumza.

Wakati mwingine tunatamani kuwa mbali na baadhi ya watu kwa sababu uwepo wao huongeza mahangaiko ya mioyo. Mtu ni utu. Na utu ni kutambua uwepo wako na uwepo wa wengine hali tukitambua kuwa kila mtu anayo nafasi yake ya kuishi na kuitawala himaya yake ya maisha (personal doom).

Haya twaweza kuyatambua ama kwa akili au kwa hekima ambapo vyote viwili ni vipawa tulivyopewa na Mungu. Wakati mwingine akili zetu zaweza kushindwa kuchambua na kufikia maamuzi ya nini cha kusema au kufanya. Katika hatua kama hiyo ndipo huruhusu hekima kuingilia mchakato wa kufikiri kwa akili na kutupa mwongozo. Mara nyingi hekima hutuambia kwamba tutulie kwanza na kuahirisha maamuzi. Hekima hukinga maangamizi yawezayo kusababishwa hata na akili zetu.

Tunapomuomba Mungu atupe vipawa iwe pamoja na kumuomba kwamba vipawa anavyotupa vifanye kazi kwa ushirikiano. Kwa akili na hekima ushirikiano huo huwa wa kwenda sambamba pale tunapoamua mambo mema. Lakini pia wakati mwingine vipawa hivyo hufanya kazi pamoja kwa kutofautiana. Pale akili zinapofanya maamuzi kwa pupa hasa katika mambo ya maangamizi ni vema hekima ipewe nafasi ya kukataa ili kuepusha madhara.

Wakati huu wa kupambana na janga la kirusi corona tutapingana na mtu yeyote anayethubutu kutugawa na kuhangaisha mioyo ya watu kwa maneno yake. Tayari hofu ya corona inaleta mahangaiko mioyoni mwa watu. Taifa halihitaji kuongezewa hofu. Kinachohitajika sasa ni faraja na kuwapa watu matumaini ya kuishi. Sasa tunapambana na janga hili kama Watanzania na wala sio kama CCM na wapinzani. Pale akili zetu zinaposhindwa kufikiri au zinapofikiri vibaya basi tuipishe hekima itupe muongozo wa mambo ya kuzungumza na kufanya.

Mungu ibariki Tanzania!
Mungu tupiganie kama taifa
 
Sijui ni nini kimewapata viongozi wa CCM wa awamu hii. Hivi wamelogwa, wamelaaniwa au vyote kwa pamoja? Walahi kuna damu za watu zinawatesa. Haiwèzekani viongozi wajitoe ufahamu namna hii kama sio laana? Polepole think out my brother, Unalipeleka wapi hili taifa?

Kumbuka wewe ni kiongozi wa chama tawala tena msemaji. Kila unalosema watu wanaamini limesemwa na chama na umetumwa na chama kulisema. Kila neno unalotoa linahifadhiwa kama kumbukumbu kwa vizazi vijavyo.
 
AKILI NA HEKIMA: CORONA SIO SAWA NA WAPINZANI

Wakati huu dondoo kubwa ya taifa na ambayo serikali yetu inaipa msukumo mkubwa ni mapambano dhidi ya kirusi corona. Mapambano haya hayana mzaha wala kebehi na yanadai umoja na mshikamano wa kitaifa. Usemi wa Ndg. Polepole kwamba corona ni sawa na wapinzani ni lugha ya mtu anayeligawa taifa katika kipindi hiki kigumu.

Malezo yake mengine juu ya corona na madhara yake sina shida nayo. Bali kauli hii ya kebehi na kugawa watu katika makundi ya kisiasa wakati huu inamuonyesha yeye ni mtu wa jinsi gani. Kauli hiyo japo ya maneno machache imechujua hata mambo mengine aliyozungumza.

Wakati mwingine tunatamani kuwa mbali na baadhi ya watu kwa sababu uwepo wao huongeza mahangaiko ya mioyo. Mtu ni utu. Na utu ni kutambua uwepo wako na uwepo wa wengine hali tukitambua kuwa kila mtu anayo nafasi yake ya kuishi na kuitawala himaya yake ya maisha ( personal doom).

Haya twaweza kuyatambua ama kwa akili au kwa hekima ambapo vyote viwili ni vipawa tulivyopewa na Mungu. Wakati mwingine akili zetu zaweza kushindwa kuchambua na kufikia maamuzi ya nini cha kusema au kufanya. Katika hatua kama hiyo ndipo huruhusu hekima kuingilia mchakato wa kufikiri kwa akili na kutupa mwongozo. Mara nyingi hekima hutuambia kwamba tutulie kwanza na kuahirisha maamuzi. Hekima hukinga maangamizi yawezayo kusababishwa hata na akili zetu.

Tunapomuomba Mungu atupe vipawa iwe pamoja na kumuomba kwamba vipawa anavyotupa vifanye kazi kwa ushirikiano. Kwa akili na hekima ushirikiano huo huwa wa kwenda sambamba pale tunapoamua mambo mema. Lakini pia wakati mwingine vipawa hivyo hufanya kazi pamoja kwa kutofautiana. Pale akili zinapofanya maamuzi kwa pupa hasa katika mambo ya maangamizi ni vema hekima ipewe nafasi ya kukataa ili kuepusha madhara.

Wakati huu wa kupambana na janga la kirusi corona tutapingana na mtu yeyote anayethubutu kutugawa na kuhangaisha mioyo ya watu kwa maneno yake. Tayari hofu ya corona inaleta mahangaiko mioyoni mwa watu. Taifa halihitaji kuongezewa hofu. Kinachohitajika sasa ni faraja na kuwapa watu matumaini ya kuishi. Sasa tunapambana na janga hili kama Watanzania na wala sio kama CCM na wapinzani. Pale akili zetu zinaposhindwa kufikiri au zinapofikiri vibaya basi tuipishe hekima itupe muongozo wa mambo ya kuzungumza na kufanya.

Mungu ibariki Tanzania!
Mungu tupiganie kama taifa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli Askofu amenena kifalsafa. Polepole tatizo lake hashirokishi hekima ktk kupayuka kwake COVID-19 ni janga la KIDUNIA, unalihisishaje na CHADEMA. CCM haijapata mwenezi ina mlopokaje. Wazee wa CCm kama Mzee Mkapa, Msekwa, Kikwete, Magufuli, Mwandosa, Mwinyi kweli hawamuoni huyu mzee Kijana kuwa kweny hiyo nafasi ya anapwaya? CCM ni chama kikubwa san kinaitaji mwenez wa kuunganisha Taifa sio huyu Mzee Polepole anayehubiri migawanyiko.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Polepole hana itikadi y ccm huyu mtu tangu mwanzoni ni mpambania haki hapo alipo ni njaa imempeleka huko n ss amevimbiwa. Polepole tunae mjua ni yule wa rasimu y katiba y jaji Warioba. Analazimika hivi ss kusema tu lolote linalomjia kinywani ili aendelee kula nakupanda V8.
 
Kuna mengi mazuri Askofu kayaongea lkn mbn wenye taaluma wameshindwa hata kusema wanaishia kusema duh. Mwana CCM anaona neno la kufananishwa chadema na kirusi cha covid19 linafaa.

Matokeo ya kushughulikiwa corona yatawapata chadema na maana yake viongozi wa CCM walioko chini watajitahidi kuwaangamiza chadema kabisa. Na kwa mapenzi na upendo wa MUNGU, CCM wasijidanganye au kutoikemea kauli kama hiyo kwa sababu siyo pekee yao MUNGU yu upande wao.
Wasio haki hujiona kushinda lkn hawana muda MUNGU atawaondoa.

Askofu anaposema kauli hii inaligawa taifa anasema kweli kwamba kuna wenye kupendelewa na muumba kuwatawala wasio pendwa na MUNGU.

NA WENYE KUELEWA WANAPO AMUA KUKAA KIMIA wajinga huinuka na kulisababisha taifa kuugua. Ipo siku.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maaskofu waingie tu kwenye siasa tujue moja
Inasubiriwa tu watu wa ccm wakohoe watoe nyongo zao,kuna watunga sheria wamevamia.gereza na kutaka kufungulia wafungwa,askofu kama hakulisikia hilo,yupo kimyaaa
Mimi nayaheshimu maoni yako lakini sikubaliani nayo.Corona ni kama wapinzani ni kauli ya ajabu saana....Nape wetu kwa vile kesha omba na kasemehewa,arudishwe asap

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom