Baba Askofu Dr. Bagonza: Mapenzi ya Mungu na Mapenzi yetu

Baba Askofu Dr. Bagonza: Mapenzi ya Mungu na Mapenzi yetu

Dah.. Chadema ni wajinga sana walahi!

Kila andiko wao huona kwa upande wa siasa basi! Tena likiwa limetolewa na mkosoaji wa Magufuli.

Kwa akili za wana chadema wanaona askofu kasema tusijenge mabwawa, tusinunue meli wala ndege kwa sababu zina majanga!

Ni heli unyimwe kipato kuliko akili za kutafakari!
Duh mkuu, kumbe hawa wanaoshambulia na kushutumu hicho alichoandika huyo Askofu ni CHADEMA?!
 
Baba askofu umeongea point,ambaye hajaelewa ana matatizo ya akili.
 
kwa nilivyomuelewa baba Askofu hoja yake ipo hapa, "hatua zote za maendeleo zina majanga hivyo uwezo wetu upimwe kwa kushughulikia majanga".
hatua za maendeleo ni zipi kazitaja tumenunua ndege, meli mpya ya abiria 2000, na tunajenga strigglers gorge. vitu vyote hivo sio vigeni hapa duniani na vyote vimeshaleta majanga makubwa yaliopelekea vifo vya watu na uharibifu wa mali na miundombinu mbalimbali.
sasa sisi kama watanzania tujiulize; kwasababu vitu hivo vinamajanga tusinunue ndege?,tusinunue meli? tusijenge mabwawa? jibu ni hapana, ila tunapaswa kujiuliza tunajiandaa vipi kushughulikia kuzuia majanga yasitokee na tunakabiliana nayo vipi pindi yanapotokea majanga. tumenunua kivuko je tunazingatia sheria na taratibu za kuendesha kivuko?, idadi ya watu na mizigo tunayopakia ina endana na uwezo wa kivuko?, tunazingatia sheria za usalama wa anga?, tuna vifaa vya uwokozi vya kutosha?.
iyo ndio hoja ya Baba Askofu na sio mihemuko unayosema wewe.
Ufafanuzi mzuri kabisa.
 
Mwanasiasa aliyejificha kwenye dini.Afanye moja aeleweke.
Kwahiyo na wanasiasa wanaoongelea mambo ya dini nao ni wachungaji waliojoficha kwenye siasa??Jipe akili sawa sawa Siasa ni maisha ya kila siku hakuna mtu mwenye hati miliki nayo ,so mtu yeyote anaweza kuizungumza na kutoa maoni yake
 
Anaandika Baba Askofu Dr.Benson Bagonza (PhD), daktari wa Falsafa na Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe.
_____________________________
MAPENZI YA MUNGU na MAPENZI YETU.

Siyo kila kifo ni mapenzi ya Mungu hata kama Mungu anajua kila kifo. Siyo kila ajali ni Mapenzi ya Mungu hata kama Mungu anaiijua kila ajali.

Tukumbuke alimuacha Mwana wake kuuawa hata kama alikuwa na uwezo wa kuzuia. Alimwacha Mwana wake kusalitiwa hata kama alikuwa na uwezo wa kumkomesha msaliti wake.

Hatua zote za maendeleo zina ukurasa wa majanga. *Dreamliner na Bombadier usiote janga lake. SGR janga lake ni kiama. Stiggler's Gorge ina janga la kuangamiza mamilioni kwa siku moja kingo za bwawa zikipasuka. Meli mpya ya abiria 2000 ni kaburi la halaiki linaloelea majini.*

Uwezo wetu upimwe kwa kushughulikia majanga, si kwa kuchochea majanga. Poleni wafiwa, Ugua pole majeruhi, Tufarijiane Watanzania.

#MyTake:
Falsafa ni somo gumu, halijawahi kueleweka kwa wote. Lakini pamoja na ugumu wake, tuzitafakari falsafa za baba Askofu Bagonza, na tujitahidi kuzielewa. Zina mengi ya msingi.!
Mhh sidhani kama wamemwelewa huyu baba askofu??subiri postings
 
Nina uhakika uelewi ata king kidogo kuhusu dini. Hakuna sehemu ata moja dini iliwahi kutengwa na siasa.

Soma story zote za mitume na manabii hawakuwahi kuficha nyuso zao kwa kuogopa watawala.
[emoji818][emoji818]nimeipenda sana hiyo.Tatizo hulka ya kusoma Tz imeshuka sana. most us read for exam and not for knowledge gain.Wengi wetu huamini tuambiwacho na watu bila kutafakari na kuutafuta ukweli.
 
Aliekudanganya kuwa kwenye ndege kunamiamvuli ya kujiokoa kakuweza kwelikweli. Panda ndege hata sikumoja uone kama kunakitu kama hicho. Kitu ambacho kipo ni life jacket kama za kwenye meli hakuna parachute ndugu yangu.
miavuli kwenye ndege????jukwaa limeingiliwa
 
kwa nilivyomuelewa baba Askofu hoja yake ipo hapa, "hatua zote za maendeleo zina majanga hivyo uwezo wetu upimwe kwa kushughulikia majanga".
hatua za maendeleo ni zipi kazitaja tumenunua ndege, meli mpya ya abiria 2000, na tunajenga strigglers gorge. vitu vyote hivo sio vigeni hapa duniani na vyote vimeshaleta majanga makubwa yaliopelekea vifo vya watu na uharibifu wa mali na miundombinu mbalimbali.
sasa sisi kama watanzania tujiulize; kwasababu vitu hivo vinamajanga tusinunue ndege?,tusinunue meli? tusijenge mabwawa? jibu ni hapana, ila tunapaswa kujiuliza tunajiandaa vipi kushughulikia kuzuia majanga yasitokee na tunakabiliana nayo vipi pindi yanapotokea majanga. tumenunua kivuko je tunazingatia sheria na taratibu za kuendesha kivuko?, idadi ya watu na mizigo tunayopakia ina endana na uwezo wa kivuko?, tunazingatia sheria za usalama wa anga?, tuna vifaa vya uwokozi vya kutosha?.
iyo ndio hoja ya Baba Askofu na sio mihemuko unayosema wewe.
[emoji818][emoji818][emoji818][emoji818][emoji818][emoji818][emoji818][emoji818][emoji818][emoji818][emoji818][emoji818][emoji818]
 
Watu wajinga tu ndio wataona Baba Askofu anafanya siasa. Hapa Askofu katahadharisha umuhimu wa kuzingatia usalama katika masuala yanayohusu uhai wetu. Ununuzi wa ndege ambao umefanyika kwa nia njema, uendane na uendeshaji wenye uzingatiaji wa kanuni za usalama. Treni ya mwendo kasi iendane na uzingatiaji wa kanuni za usalama wa watumiaji wake. Miradi aliyoitaja Baba Askofu yote inaweza kuangamiza mamia ya watu ikiwa kutafanyika uzembe kama wa Mv Nyerere. Hakuna ubishi kwamba ajali ya MV Nyerere imetokana na uzembe wa wasimamizi wa chombo husika. Idadi ya miili iliyopatikana hadi sasa inaonyesha kile kinachosemwa hapa na Askofu Bagonza.
Ni mjinga pekee, mvivu wa kufikiri na mtu asiye na hekima ndiye anaweza kuona siasa katika tamko la Askofu..!
 
Aliekudanganya kuwa kwenye ndege kunamiamvuli ya kujiokoa kakuweza kwelikweli. Panda ndege hata sikumoja uone kama kunakitu kama hicho. Kitu ambacho kipo ni life jacket kama za kwenye meli hakuna parachute ndugu yangu.
Mr Slow ndo huwa anawapiga fiksi hawa vijana.
Awamu hii kiongozi wa dini akikosoa jambo lolote anaambiwa anachanganya dini na siasa.
Toka karne na karne dini huwezi tenganisha na siasa.
 
Huyo anafanya siasa tu..kwa nini agusie miradi ya maendeleo ambayo chadema wanaipinga..?mbona mabasi yanapata ajali..boda boda na vingine..hata magari binafsi..mwanadamu huwa akikaa hafikirii mabaya..kwenye ndege kuna miamvuli ya kujiokoa lakini hata siku moja husikii ndege imepata ajali na kuna watu wawili walijiokoa kama ambavyo tunaagizwa kufanya tukiingia kwenye ndege ( hii ni kwa waliowahi kupanda)..inapotokea ajali watu hughafirika na unaweza usione hata hilo boya hususani kwa ajali ya mara moja na haraka...lakini ukiangalia hii ajali ilikuwa inaepukika..ni suala la uzembe na rushwa kwa wasimamizi wa kivuko..
Hii falsafa ya baba askofu is not for average minds!
 
Anaandika Baba Askofu Dr.Benson Bagonza (PhD), daktari wa Falsafa na Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe.
_____________________________
MAPENZI YA MUNGU na MAPENZI YETU.

Siyo kila kifo ni mapenzi ya Mungu hata kama Mungu anajua kila kifo. Siyo kila ajali ni Mapenzi ya Mungu hata kama Mungu anaiijua kila ajali.

Tukumbuke alimuacha Mwana wake kuuawa hata kama alikuwa na uwezo wa kuzuia. Alimwacha Mwana wake kusalitiwa hata kama alikuwa na uwezo wa kumkomesha msaliti wake.

Hatua zote za maendeleo zina ukurasa wa majanga. *Dreamliner na Bombadier usiote janga lake. SGR janga lake ni kiama. Stiggler's Gorge ina janga la kuangamiza mamilioni kwa siku moja kingo za bwawa zikipasuka. Meli mpya ya abiria 2000 ni kaburi la halaiki linaloelea majini.*

Uwezo wetu upimwe kwa kushughulikia majanga, si kwa kuchochea majanga. Poleni wafiwa, Ugua pole majeruhi, Tufarijiane Watanzania.

#MyTake:
Falsafa ni somo gumu, halijawahi kueleweka kwa wote. Lakini pamoja na ugumu wake, tuzitafakari falsafa za baba Askofu Bagonza, na tujitahidi kuzielewa. Zina mengi ya msingi.!
Sioni Falsafa yoyote hapa zaidi ya unafki wa kisiasa tu.
 
Hawa miungu watu wa Afrika lazima wakemewe tuu, na manabii na mitume wa Mungu.

Haya ni maneno ya Yesu mwenyewe akimwambia Herode.

Luka 13:32
Akawaambia, Nendeni, mkamwambie yule mbweha, Tazama, leo na kesho natoa pepo na kuponya wagonjwa, siku ya tatu nakamilika.
Halafu kwa Yesu kumuita mbweha maana yake ndani ya Herode kulikuwa na roho ya shetani iliyovaa sura ya mbweha
 
Back
Top Bottom