Nami naomba nichangie kidogo...
Mi nafikiri alichoandika mdau Chasha ni cha kweli. Tusianze kulalamikia mitaji kama excuse. Cha msingi ni kuwa na nia thabiti, ambayo kwayo inatoa nguvu kubwa sana. Ukiwa na nia, unaweza kutafuta mtaji through kupiga debe, kufanya vibarua and the like.
Nilijaribu kuongea na rafiki zangu pale Kariakoo, ambao wanauza maji, ambao walinieleza kuwa ukiondoa mtaji, wanaweza kutengeneza ziada ya Tsh. 12,000-13,000, na siku ya biashara mbaya wanatengeneza ziada ya Tsh. 4000 at minimal.
Aidha, wale akina mama wanaouza matunda nao wana make ziada ya kiasi kama hicho,ambapo wao wanachukua matunda kule Temeke Stereo kwa Tsh.50-70 kwa embe moja,lakini kariakoo wanauza kwa Tsh. 250-300, na kwa juhudi zao matunda haya yanaisha.
Niliozungumza nao wananieleza tayari wameshanunua plots (walianza biashara hiyo miaka mi3 iliyopita). Hawa waliongozwa na nia iliyowapa nguvu ya kusonga mbele, japo vipo vikwazo walivyokutana navyo, nawanavyokutana navyo, lakini wanasonga mbele.
Hivyo,nafikiri mtaji mkubwa aliokuwa nao mtu ni mind set,na mtaji mwingine ni kuwa na mahusiano mema na jamii, ambayo kwayo unaweza pata mawazo mengi mazuri, na inawezekana ukaaminika na mtu/watu w/akakupesha mtaji.
Nawasilisha mchango wangu