Baadhi ya njia unazoweza kutumia kupata wazo bora la biashara (Business Idea)

Daah mkuu nimekuelewa, hii inawalenga wengi sana utakuta mtu ana professional nyingine ila kinachokuja kumtoa ni kingine.
Thanks mkuu
 
Bandiko lako zuri Mkuu

Naomba nami niliongezee thamani zaidi katika kuondoa dhana ya "sina mtaji" ndiyo maana siwezi kufanya biashara. Swali la msingi katika biashara ni "Je tunahitaji Mtaji kufanya biashara ili tufanikiwe?" Jawabu sahihi ni kuwa Mtaji ni jambo la mwisho kabisa uhitaji wa kufanya au kuanzisha biashara. Tunahitaji 1. Wazo 2. "Network" 3. Mtaji

1. Wazo
Ili uanze biashara lazima uwe na wazo. Hakuna biashara mpya ambayo haijafanya katika dunia ya leo isipokuwa kuna uwezekano mkubwa wa kuiboresha zaidi na zaid biashara ambayo tayari ipo sokoni. Na wazo la biashar lazima uliandike sio unasema una wazo lakini hata kuliandika katika japo daftari dogo huandiki. Hili wazo kadiri unavyoliandika utapata kutafakari zaidi na kuandaa dondoo ndogo ndogo za namna gani ulifanikiwe. Pili, waweza kujifunza kwa kutumia wazo lako kupitia kwa wajasiriamali waliofanikiwa na vilevile waweza kuliwasilisha wazo lako kwa washauri wa kibiashara ambao watakupa mwongozo mzuri na namna gani ya kuliboresha na hatimaye kuwa wazo linalokopesheka (bankable ideas).

2. Mtandao
Jenga mtandao wa kimahusiano yenye manufaa na hasa yanayohusiana na wazo lako. Mathalani wazo lako umelipanga vema ukaaweza kuandaa au kuandaliwa Mchanganuo wa biashara (Business proposal and Business plan) waweza kupeleka katika taasisi kama vile SIDO, Benki za kibiashara (TIDB),EFTA na taasisi za serikali n.k kutegemeana na nini unachotaka kufanya na upekee wa wazo lako japo sio jipya duniani lakini yawezekana Tanzania likwa jipya au linahusiana na masuala mathalani mazingira, jamii inaguswa au kwa namna fulani lina uzito wake. Vile vile jenga mtandao na unaoona watakupa njia mbadala za kufikia malengo yako ambao kwa namna moja au nyingine wapo tayari kuona ndoto zako zinatimia. Mliosoma vyuo vikuu, andika andiko lipeleke chuoni kwako kwa idara za masuala ya "research" utafanikiwa tu. Serikali ina ruzuku katika mipango ambayo inaweza kuibadilisha jamii, hangaikia fursa hizo

3.Mtaji

Ukifanikiwa hayo mawili utaona kama ni wazo lako la biashara basi limeshakuwa ni wazo linalokopesheka/linalowezekana kuhuisha na kutumika. Najua kuna watu watasema hatuna dhamana. Kuna baadhi ya taasisi na mashirika yanayokopesha vitu/mashine ambazo hizo hizo ndiyo inakuwa dhamana. Watanzania hasa vijana ni wakati wa kuamka na kuzishughulisha akili zetu. Kufanikiwa katika maisha sio mpaka uajiriwe bali unapata elimu ili uwe kupambana na changamoto za kimaisha na kujikwamua kiuchumi
Kwa kifupi ni haya kwa mtazamo wangu naona
 
Mkuu ni kweli kabisa kwamba Mitaji ni Tatizo, Ila si kwa kiwango tunacho taka kuaminishwa, wewe kama Entrepreners ni lazima pamoja na mambo mengine uwe na Mbinu za kupata mitaji, na tatizo lina kuwa mitaji kwa sababu tuna penda kufanya biashara kubwa sana kitu ambacho ni ndoto, mtu anataka aingie kwenye biashara na amfikie Mengi au jamaa wa Azam, sio rahisi,

Nchi kama Kenya wapo watu wanoenda hata Kupiga Debe ilimuradi wapate mitaji, wapo wanao enda kufanya vibarua vya kufyeka ilimuradi wapate mitaji, Je, ulisha wahi jaribu hivyo na kukosa mtaji? AU unataka mtaji wa Milioni 100?

Tatizo tunataka kuanzia juu wakati wenzetu wote waliaznia chini na kufika hapo walipo sasa ingawa iliwachuku miaka mingi,

so ni vizuri kuanza na ulicho nacho, na kusonga mbele kwa sababu maswala ya mitaji yatakukuta mbele ya safari na si kusibiri mtaji ndo safari ianze, kwa sababu hata kama kuna sehemu Mikopo au mitaji inatolwe wanao pewa kipaumbele wa kwanza ni ambao tiyali walisha anza na si ambao wana mawazo.

Asipokuelewa huyo lazima tumpime mkojo.Asante sana.
 
Wakuu me nina mtaji Wa milioni mbili na nusu ila naomba ushauri ni kibiashara gani naweza Fanya nikiwa hapa dar angalau iniingizie kuanzia elfu kumi na kuendelea !?kama kuna mtu yupo mwenye idear ya biashara ya kufanya hapa dar kwa mtaji huo naomba anisaidie na nipo tayari hata kununua ushauri wake ili lengo langu litimie, ila biashara iwe ni ya kumuacha mtu maana me nimfanya kazi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom