Baada ya vijana kuoa huwatupa mama zao

Baada ya vijana kuoa huwatupa mama zao

Lawyer I hear youuuu. Ndo maana mafundisho yanasema "Mke ndiye anayebeba kusudi la mume wake". Yeye ndiye anayebeba kitu ndani yake cha kumsaidia mumewe ( ni Msaidizi wa mumewe) . Mwanamke akijitambua na kusimama katika sehemu yake, tutaona kwa macho jinsi mwanaume na ndoa yao kwa ujumla itakavyokuwa ya baraka, mume atakumbushwa wajibu wake.

Lakini oa mwanamke Mpumbavu, na tutashuhudia maisha yenu yatakavyokuwa ya ajabu
Asante! Hivi na wewe unakubaliana na wanao sema swala la mwanaume kutunza wazazi wake ni fadhila tuu na si wajibu wake?

Ukitaka kugundu muda mwingine tunawasingizia wanawake kuwa ndio chanzo cha wanaume kutelekeza wazazi wao kabisa fatilia huu mjadala!

Leo hii ni nadra kusikia mwanamke kawatelekeza wazazi wake lakini hili tatizo liko kwa wanaume asilimia 90%,,,,,

Kuna rafiki yangu ana mkewe ana mimba kila leo jamaa anaomba mkewe azae mtoto wa kike na sababu zake anasema watoto wake wana upendo wa kudumu si kwa watu baki tuu bali hasa kwa wazazi wao!

Kila anae soma hapa anaweza kuja na takwimu zake hadi ya wanawake anao wajua walio telekeza wazazi wao na bila shaka tunaweza kosa kabisa.......!

Bahati mbaya hizi lawama tumekuwa tukiwatupia wanawake lakini mjadala unavyo endelea ndivyo utaelewa hata sisi wanaume ni tatizo kabisa halafu mtu anatumia vitabu vya dini kujitetea.....!
 
Ha ha ha! Madam nilivyokuwa naisoma sentensi nilikuwa nawaza eti ... tutawaacha wazazi wetu kwenda kutafuta pesa...! Kumbe ni kuambatana na mwenzio.
Bahati mbaya kwenye huu mjadala watu wanatumia maandiko kuhalalisha makosa yao ya kukimbia m ajukumu ya kuwatunza wazazi wa
 
Mwanamke anaonekana anapasaidia kwao mana kwa lugha nyepesi wanawake wengi ni FISADI. Mme utatafta hela ya kuwakimu na mke ataibajeti na kinachobaki atawapa wa kwao na sio kuigawa sawa kwa sawa pande zote. Pia ikumbukwe mke kipato chake hakihojiwi kinatumikaje ktk familia, hvo kama hana utu ndio hupeleka chote kwao na bado atakunyonya na mme.

Cha muhimu ni kufanya yafuatayo.. Jua kipato cha mkeo, mjulishe na ww kipato chako. Kaeni mpange matumizi ya kujikimu, akiba na kiasi cha kusaidia makwenu. Tena iwe kwa usawa ili isionekane mmoja ana vuta kwake.

Likitokea tatzo upande mmoja wa ukweni ndio ruksa kupeleka fungu la upand wa pili kwa mda flani kusaidia utatuzi. #ila ikumbukwe mkeo ana haki ya jasho lako na sio ndugu wala wazaz, ndugu hana mamlaka ya kudai msaada ila mzaz peke ake ndio ana weza kudai msaada kama alitumia jasho lake lote kukufikisha ulipo.
 
Asante! Hivi na wewe unakubaliana na wanao sema swala la mwanaume kutunza wazazi wake ni fadhila tuu na si wajibu wake?

Ukitaka kugundu muda mwingine tunawasingizia wanawake kuwa ndio chanzo cha wanaume kutelekeza wazazi wao kabisa fatilia huu mjadala!

Leo hii ni nadra kusikia mwanamke kawatelekeza wazazi wake lakini hili tatizo liko kwa wanaume asilimia 90%,,,,,

Kuna rafiki yangu ana mkewe ana mimba kila leo jamaa anaomba mkewe azae mtoto wa kike na sababu zake anasema watoto wake wana upendo wa kudumu si kwa watu baki tuu bali hasa kwa wazazi wao!

Kila anae soma hapa anaweza kuja na takwimu zake hadi ya wanawake anao wajua walio telekeza wazazi wao na bila shaka tunaweza kosa kabisa.......!

Bahati mbaya hizi lawama tumekuwa tukiwatupia wanawake lakini mjadala unavyo endelea ndivyo utaelewa hata sisi wanaume ni tatizo kabisa halafu mtu anatumia vitabu vya dini kujitetea.....!
Kwa nature ya maisha yetu waafrika/ watanzania utegemezi ni suala ambalo lipo na litaendelea kuwepo kwa muda kidogo. As long as bado tunaishi kwa kutegemeana " kuwasaidia wazazi ni inevitable". How on earth utawaacha wazazi wako wahangaike while mtoto wao upo na una uwezo wa kuwasaidia? Sio wajibu wako? Ni wajibu wa nani sasa?

kwa maisha yetu yaliyotawaliwa na umaskini wetu, unakuta wazazi wetu maisha yao karibu yote wametumia kuinvest kwenye elimu zetu. Walisacrifice some luxuries ili tu sisi tusome. Kwa hiyo unakuja kukuta hadi wanaanza uzee wao hawana kitu kikubwa walichojitengenezea kwa ajili ya kuwasaidia uzeeni. Matumaini yao yote yanabaki mikononi mwa watoto zao. Ndo maana unakuta mzigo wote wa kuwatunza uzeeni mwao unatuangukia watoto na Yes inakuwa ni wajibu wote. Kuna watu wa kuwafanyia fadhila but sio wazazi. Vitu walivyotufanyia ni priceless, hatuwezi kuwalipa.

Mwanamke anainfluence kwa mume. Lakini mwanamke Mpumbavu atakuwa na influence kwa mwanaume Mpumbavu pia. Kwa sababu mwanaume anayejitambua hatoyumbishwa na misimamo ya kipumbavu kutoka kwa mke Mpumbavu. Ukiona mwanaume anafanya Vitu vya kipumbavu ujue na yeye ni Mpumbavu pia, sio tu kwa sababu amekuwa influenced. Kwa hiyo wazazi pamoja na majukumu yote, tunapaswa kuwaombea watoto wetu, Mungu awaepushe na wake wasiojitambua.
 
Ha ha ha! Madam nilivyokuwa naisoma sentensi nilikuwa nawaza eti ... tutawaacha wazazi wetu kwenda kutafuta pesa...! Kumbe ni kuambatana na mwenzio.
ha ha ha ha na unaambatana na mwanaume wa aina gani ni mwanaume mwenye pesa ha hahaha... Mungu amekupa only option ya kuchagua mwenza ukimess up shauri yako
 
Sio wote wanawasahau mama zao.... ila maranyingi wanakua wametingwa nashughuli za hapa na pale za ubava...
 
imeandikwa.... utaiacha familia yako na kwenda kuishi na mkeo!!! nathing new hapo sema tu usisahau wazazi ila priority zinabadilika

Sawa kabisa pia biblia haimaanishi utapunguza upendo wa wazazi, its change of location ya kuishi japo priority itakuwa kwa mmeo au mkeo kwa kutegemea issue yenyewe sio mke wangu amtukane mama yangu mimi afu nimpe priority mke la hasha.
 
ndio atakuzingua zaidi si anajua huna pakwenda tena mko wenyewe tu,point yako ya kwamba mtajaza dunia tena ndio naikubali

Uzuri wa kuzinguliwa mkiwa wawili tu, ni kuwa utajipa moyo ni mambo ya wanawake tu na sio kuna jamaa anayempa kiburi.
 
Teh Teh umenichekesha sana....! Kuwaacha wazazi na kuambatana na mkeo haimaanishi kuwatelekeza na kuacha kuwatunza! Hivi walivyo kulea,kutunza ,kukusomesha haikuwa wajibu? Kwanini kuwatunza wazazi usiwe wajibu wako? Hivi kweli leo hii kuwatunza wazazi wako iwe fadhila na si wajibu ikiwa wao ndio walikufikisha hapo ulipo?

Hakika umepotoka sana.na huwa mnatafsiri vibaya maandiko...! Just imagine ikiwa wewe mwanaume ndio mtoto pekee....!

Mimi naamini swala la mwanaume kutunza wazazi tena walio mzaa ni wajibu na lazima kabisa na wala haliitaji mjadala kutoka kwenye vitabu vya dini!

ua ryt mdau, na vitabu vya dini vimesisitiza juu ya kuwajali wazaz.Hata mzazi akifariki MTOTO MWEMA ANA WAJUBU WA KUMUOMBEA KATIKA MAISHA YAKE YOTE YA UHAI WAKE,KUMTOLEA SWADAKA NI WAJIBU PIA
 
Back
Top Bottom