Baada ya vijana kuoa huwatupa mama zao

Baada ya vijana kuoa huwatupa mama zao

It's not that easy man... there are lot of hot ladies out there to fill the world with!!! But aren't one to be my mom again

The situation i'm talking about is the one that the whole world has to be wiped out clean, and it's only you + that one person you'd choose who will survive. Would you still choose your mother? Man, i'd choose even one of my exes if i have to, and my Mum would be proud.
 
Apart from the fact kwamba wamama wanashare a very special bond na watoto wao wa kiume ( just like we girls and our darlin pops).... malezi ya mtoto wa kike na wa kiume yanatofautiana pia.

Tangu tunazaliwa na kukua, binti unalelewa ili uje kuwa mke bora huko kwa mumeo, while mvulana analelewa kuja kuwa msaada wa familia ( yeye anahesabika kama ni mtoto wa nyumbani milele). Utamsikia mmama kabisa yani huyu baba angu ndo atakuja kunisaidia.

Kingine nafikiri wanawake tuna kaubinafsi fulani hivi. Vilivyo vyetu vizuri na tunavyovipenda sana hatupendi kushare kabisaa.

Haya kaka na dada mtapelekwa shule vizuri. Mungu amesaidia mmemaliza shule. Familia itashukuru kwa kuwa mmemaliza salama ila itashukuru zaidi kwa kuwa kaka akipata kazi ataanza kuisaidia familia instantly. Wewe dada hata usipopata kazi haina shida, utakuwa unaombewa tu uolewe basi. Haya kaka kapata kazi, anasaidia home vizuri, but siku akisema tu nimepata mchumba.... familia inahisi kama imepoteza baba na mtu wa kuisaidia. Na worse enough mama anahisi kama "mchumba/mke" atakuwa ndo mwanamke wa muhimu zaidi kwenye maisha ya mwanae. Ndo maana mabinti hadi tuolewe tunapitia mengi jamani, mara mama mkwe na mawifi wakukatae (God forbid), na sometimes ni bila hata ya sababu ya msingi.

Usiombe ukute ni single mother na mtoto pekee aliyenaye ndo huyo kaka, au kaka ndo mtoto wa pekee wa kiume kwao... mama anahisi kama binti/mchumba umekuja kuchukua furaha ya maisha yake. Kuna wamama wanafanya hata juu chini watoto wao wasioe kabisa. Wabaki tu kuishi nao wao

Bahati mbaya zaidi ukishaoa sasa, ole wako nyumbani waombe msaada fulani afu uwajibu wasubiri kidogo... itaonekana tu "mkewe ameshaanza kumbadilisha, kamshika akili". Lakini tunasahau kuwa mtoto wetu amekua, now ana familia yake so ana majukumu mapya. Mkewe ndo ubavu wake jamani, ingawa thamani ya mama itabaki palepale milele daima.

I think wamama inabidi tubadilike, tutambue kuwa vijana wetu wameoa, wana familia sasa hivi, majukumu yameongezeka pia so tusiwabane sana jamani, coz lazima kuna Vitu vitabadilika kidogo

.Na nyie vijana wa kiume msijisahau, manake kuna watu wakishaoa tu wanawake type za kina nanhii basi wanasahau kabisa kuwa kuna watu waliwazaa na kuwatunza kwa shida. Saidieni kwenu, mbona mabinti hatusahau kusaidia kwetu. Mtu unatanua tu huku hata mama ako umeshindwa kumjengea kakibanda. Upo na mama ako unaogopa hata kamtambulisha kwa wenzio au unapata hata msiba unaona aibu kwenda kwa wazazi wako maana hata hapaeleweki. Muache tabia hiyo

Na mabinti mnaoolewa msiwafanyie hivyo mama wa wenzenu. Ukishaolewa tu naamini mama mkwe wako ndo anakuwa mama yako. So mtreat kadri ambavyo utapenda wake wa kijana wako waje wakutreat au kadri unavyowish kumtreat mama yako mzazi. Hata kama huna uwezo wa kusaidia still unaweza ukawa unamkumbusha tu mumeo "baba nanhii unajua mama hatujamtumia hela mwezi wa pili huu". Utabarikiwa hadi ushangae ( samahani kwa huu mzalendo khaaa)
 
Kuwatupa sio neno zuri lakini mtiririko uliouweka ni kweli kabisa na yule asiyekubaliana ndio inaanza kuleta shida kwenye ndoa ya huyo kijana
Nafikiri alicho taka kuonesha mtoa mada ni kwamba asilimia kubwa ya wanaume tukishaoa tuna wasahau wazazi na wengine hufikia kuonesha kuwa wazazi wao ni watu wabaya na hawafai......!

Na mara nyingi ili tatizo husababishwa na aina ya wanawake tunao funga nao ndoa...na ukweli ni kwamba wanawake walio wengi huwa hawapendi wanaume zao kuendelea na majukumu ya kuhudumia ndugu zao au wazazi wao lakini cha kushangaza mwanaume akiwahudumia ndugu wa upande wake huwa si tatizo!

Wanaweke hufikia hatua ya kwenda kwa waganga kuwatengeneza waume zao ili waweze kuwaongoza na wasahau kwao kabisa ...ili ni janga kubwa kwenye ndoa nyingi kabisa na kati ya ndoa kumi basi ndoa sita zina tatizo tajwa!

Ukweli ni kwamba wanaume wengi huwatelekeza wazazi wao kwa kuwa wanawake huhakikisha hilo linatokea na jambo ili haliitaji utafiti kujua...!

Wanawake tunao waoa huchangia sana wanaume kuwatelekeza mazima wazazi wao maana kiukweli hakuna mwanaume normal wakufanya haya!
imeandikwa.... utaiacha familia yako na kwenda kuishi na mkeo!!! nathing new hapo sema tu usisahau wazazi ila priority zinabadilika

kama neno la Mungu lisemavyo tatawaacha wazazi wetu na kuambatana na mwenzio .... hapo ndiyo maana ya uambatano hutokea
 
Kama mtu hana msimamo thabiti na kushindwa kuhudumia wazazi wake asilaumiwe mke au mume ni yeye mwenyewe kutojitambua kwake ama hao wawili kupeana ushauri wa kupotoshana. Ndio miungu wa dunia mama na baba.
 
Hapa Kuna Vitu Watu Wanashindwa Kuelewa Na Kushusha Lawama Tu, Maandiko Yanasema Utamwacha Baba Na Mama Mtakuwa Pamoja Hapo Tena Si Wawili Bali Mwili Mmoja, Na Kuna Fadhila Na Wajibu, Ni Wajibu Wa Mwanaume Kuhakikisha Mke Wma Watoto Wanakula Vizuri Wanavaa Vizuri Watoto Wanasoma, Kiujumla Wanakuwa Na Maisha Mazuri Huo Ni Wajibu Wako, Lakini Kwa Wazazi Ni Kulipa Fadhila Kwa Walichokufanyia Hata Usipowasaidia Wataishia Kunung'unika Tu' Lakini Mke Na Watoto Usipotimiza Wajibu Wako Hata Jela Unaenda
 
Heaven Sent mpendwa hiyo paragraph ya mwisho imenibariki sana..Ubarikiwe sana kwa ushauri huu
 
Last edited by a moderator:
Heaven Sent mpendwa hiyo paragraph ya mwisho imenibariki sana..Ubarikiwe sana kwa ushauri huu

Amen barikiwa sana mpendwa. Nazidi kumuombea K naye awe mwanamke wa baraka kwako, kwao na kwa familia yako.
 
Last edited by a moderator:
Nafikiri alicho taka kuonesha mtoa mada ni kwamba asilimia kubwa ya wanaume tukishaoa tuna wasahau wazazi na wengine hufikia kuonesha kuwa wazazi wao ni watu wabaya na hawafai......!

Na mara nyingi ili tatizo husababishwa na aina ya wanawake tunao funga nao ndoa...na ukweli ni kwamba wanawake walio wengi huwa hawapendi wanaume zao kuendelea na majukumu ya kuhudumia ndugu zao au wazazi wao lakini cha kushangaza mwanaume akiwahudumia ndugu wa upande wake huwa si tatizo!

Wanaweke hufikia hatua ya kwenda kwa waganga kuwatengeneza waume zao ili waweze kuwaongoza na wasahau kwao kabisa ...ili ni janga kubwa kwenye ndoa nyingi kabisa na kati ya ndoa kumi basi ndoa sita zina tatizo tajwa!

Ukweli ni kwamba wanaume wengi huwatelekeza wazazi wao kwa kuwa wanawake huhakikisha hilo linatokea na jambo ili haliitaji utafiti kujua...!

Wanawake tunao waoa huchangia sana wanaume kuwatelekeza mazima wazazi wao maana kiukweli hakuna mwanaume normal wakufanya haya!

Lawyer I hear youuuu. Ndo maana mafundisho yanasema "Mke ndiye anayebeba kusudi la mume wake". Yeye ndiye anayebeba kitu ndani yake cha kumsaidia mumewe ( ni Msaidizi wa mumewe) . Mwanamke akijitambua na kusimama katika sehemu yake, tutaona kwa macho jinsi mwanaume na ndoa yao kwa ujumla itakavyokuwa ya baraka, mume atakumbushwa wajibu wake.

Lakini oa mwanamke Mpumbavu, na tutashuhudia maisha yenu yatakavyokuwa ya ajabu
 
kama neno la Mungu lisemavyo tatawaacha wazazi wetu na kuambatana na mwenzio .... hapo ndiyo maana ya uambatano hutokea

Ha ha ha! Madam nilivyokuwa naisoma sentensi nilikuwa nawaza eti ... tutawaacha wazazi wetu kwenda kutafuta pesa...! Kumbe ni kuambatana na mwenzio.
 
Hapa Kuna Vitu Watu Wanashindwa Kuelewa Na Kushusha Lawama Tu, Maandiko Yanasema Utamwacha Baba Na Mama Mtakuwa Pamoja Hapo Tena Si Wawili Bali Mwili Mmoja, Na Kuna Fadhila Na Wajibu, Ni Wajibu Wa Mwanaume Kuhakikisha Mke Wma Watoto Wanakula Vizuri Wanavaa Vizuri Watoto Wanasoma, Kiujumla Wanakuwa Na Maisha Mazuri Huo Ni Wajibu Wako, Lakini Kwa Wazazi Ni Kulipa Fadhila Kwa Walichokufanyia Hata Usipowasaidia Wataishia Kunung'unika Tu' Lakini Mke Na Watoto Usipotimiza Wajibu Wako Hata Jela Unaenda
Teh Teh umenichekesha sana....! Kuwaacha wazazi na kuambatana na mkeo haimaanishi kuwatelekeza na kuacha kuwatunza! Hivi walivyo kulea,kutunza ,kukusomesha haikuwa wajibu? Kwanini kuwatunza wazazi usiwe wajibu wako? Hivi kweli leo hii kuwatunza wazazi wako iwe fadhila na si wajibu ikiwa wao ndio walikufikisha hapo ulipo?

Hakika umepotoka sana.na huwa mnatafsiri vibaya maandiko...! Just imagine ikiwa wewe mwanaume ndio mtoto pekee....!

Mimi naamini swala la mwanaume kutunza wazazi tena walio mzaa ni wajibu na lazima kabisa na wala haliitaji mjadala kutoka kwenye vitabu vya dini!
 
Back
Top Bottom