Baada ya vijana kuoa huwatupa mama zao

Baada ya vijana kuoa huwatupa mama zao

Si ndio hapo. Hata Maza mwenyewe atakushangaa.

mmenikumbusha kisa cha Lot na mabinti zake wawili. (Genesis 19:30-38). Mabinti walipojikuta wamebaki na baba yao tu wakashauriana kuwa hakuna jinsi. tumnyweshe tu huyu mzee kilauri tujigegedeshe walau tupate watoto! Nimekuelewa sana ulivyosema endapo itatokea watu wote wanakufa utamuokoa mkeo au mpenzio.
 
Mwanamke anainfluence kwa mume. Lakini mwanamke Mpumbavu atakuwa na influence kwa mwanaume Mpumbavu pia. Kwa sababu mwanaume anayejitambua hatoyumbishwa na misimamo ya kipumbavu kutoka kwa mke Mpumbavu. Ukiona mwanaume anafanya Vitu vya kipumbavu ujue na yeye ni Mpumbavu pia, sio tu kwa sababu amekuwa influenced. Kwa hiyo wazazi pamoja na majukumu yote, tunapaswa kuwaombea watoto wetu, Mungu awaepushe na wake wasiojitambua.
dada yangu mwanaume hata awe na busara na hekima kiasi gani, akioa mwanamke mpumbavu lazima ile kwake kwa namna moja au nyingine. kamuulize mfalme selemani au mfalme ahab (1Wafalme 21,2wafalme 9:30-10:1-17)) au wanaume wengine tulio nao kwenye jamii yetu. Ila mwanaume akiwa mpumbavu akaoa mwanamke mwenye busara na hekima hakika amepata kitu chema na vinywa vya watoto, wakwe, majirani n.k vitambariki mwanamke huyo. Wale waliosema ukimwelimisha mwanamke umeelimisha taifa hawakukosea. Kule kijijni kwangu wanaume karibu wote wamekuwa mapoyoyo kisa viroba. Kama si wale kina mama nahisi kingeshakuwa kijiji cha makumbusho.
 
Back
Top Bottom