Baada ya vijana kuoa huwatupa mama zao

Baada ya vijana kuoa huwatupa mama zao

Old Member (Retired)

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2012
Posts
3,401
Reaction score
1,618
KIJANA AMBAYE HAJAOA
(I) Huwa anampenda sana mama yake, mama yake ndio anakuwa first class, endapo mama yake anaumwa na mchumba wake anaumwa basi atampeleka mama yake hospitali kwanza kabla ya mchumba wake.

BAADA YA HUYO KIJANA KUOA
(II) Mke wake anakuwa firsr class, yaani mama yake mzazi akiwa na shida na mke wake akiwa na shida basi kijana huyo ataanza na mke wake kisha mama atakuwa wa mwisho na hapa ndio unaona kijana anamnunulia gari mke wake lakini mama yake hana hata baiskeli.

BAADA YA HUYO KIJANA KUPATA MTOTO
(III) Watoto wanakuwa ndio first class, mke ni second class na mama anakuwa third class. Hapo ndipo unakuta kijana yupo tayari kupeleka mtoto wake kutibiwa India lakini mama yake mzazi atampeleka kutibiwa Mwananyamala.

Posted by: MCHUNGUZI HURU (Associate Professor)
 
Last edited by a moderator:
Kuwatupa sio neno zuri lakini mtiririko uliouweka ni kweli kabisa na yule asiyekubaliana ndio inaanza kuleta shida kwenye ndoa ya huyo kijana
 
Mke siku zote huchukua nafasi ya mama,hata wanawake wanajua, akiolewa tu anataka amreplace mama wa mwanaume moyoni mwa mwanaume. Ukimpendelea mama analaumu humpendi unampenda mama, akifanikiwa hilo hata mama anawekwa kando.

Maisha ndivyo yalivyo,kwa kujua hilo ndio maana ugomvi wa mama na mke wa kijana wake hua ni kawaida wote wakishindania upendo wa kijana, mama hataki kutoka,binti anataka aingie.
 
MCHUNGUZI HURU

unataka dunia ibaki static things changes,sioni kama kuna tatizo hapo juu unatka kijana ampende mama yake mpaka kufa ndio aoe? kwa mtu mwenye akili huwa tunawapunguzia mawasiliano ila upendo wao unabaki pale pale ,
"UKUMBUKE PIA MAMA YAKO NI MKE WA BABA YAKO" ANAPENDWA NA BABA YAKO SASA NA WEWE UMPENDE KAMA BABA YAKO UPENDO UTAMZIDIA .
 
Last edited by a moderator:
unataka dunia ibaki static things changes,sioni kama kuna tatizo hapo juu unatka kijana ampende mama yake mpaka kufa ndio aoe? kwa mtu mwenye akili huwa tunawapunguzia mawasiliano ila upendo wao unabaki pale pale ,
"UKUMBUKE PIA MAMA YAKO NI MKE WA BABA YAKO" ANAPENDWA NA BABA YAKO SASA NA WEWE UMPENDE KAMA BABA YAKO UPENDO UTAMZIDIA .

kama BABA KAFARIKI????
 
ulichokieleza ndio inatakiwa iwe hivyohivyo... si kwamba tunawatupa hapana...ila ndio system ya maisha ilivyo
 
Kweli aisee, nimeshuhudia mke ananunuliwa gari mbili za kutembelea mama mzazi anasugua gaga na daladala
 
Inategemea na mama yako,je anajiweza?je bado baba yako yupo?anajiweza?kama majibu ni ndio kote mwanaume unakua na jukumu la kuanzisha na kuendeleza familia yako mwenyewe hayo ya mama mwache yuko na mumewe watamalizana.huwezi ukawa na nyumba mbili za kuzihudumia kwa 100%.Ndio maana mnaambiwa muoe wanawake walio na mapenzi na familia zenu ili wawe wanawakumbusha ya kwenu la sivyo nyumbani utakusahau na kuhudumia ukweni tu na mkeo na familia yako mpya.
 
kama baba kafariki????
huwezi replace huo upendo wa mumewe.mama dada kaka wanapendwa upendo wa kawaida tu.hiyo kujifanya unampenda sana mama jirani yangu kavunja ndoa juzi mke anahangaika.wanawake ni viumbe wakuishi nao kwa makini sana tuna udhaifu mkubwa sana .akijua tu unampenda kuliko wife wako,utaona vimbweka vyake utamchukia mkeo bure.
Wanawake tuna asili moja tunapenda kupendwa sisi ,mke apendwe yeye,mama apendwe yy,na dada zako uwapende wao tu.haya kama mwanaume hauko matured enough to hide some,ule upendo wa mama na dada zako unauficha kidogo unashow up wa mkeo .that the facts
 
kweli aisee, nimeshuhudia mke ananunuliwa gari mbili za kutembelea mama mzazi anasugua gaga na daladala
mama mzazi alipaswa anunuliwe gari na mumewe kama wewe ulivyoweza mnunulia mke wako.
Na gari sio kitu muhimu sana katika maisha unaweza saidia wazazi wako kwa namna nyingine ,nawauliza wote hapa mama zenu wakinunuliwa gari watapeleka wapi?kama sio majidai ya bure?
 
Kabla hujaoa, kijana hakikisha unawafanyia mazuri yote familia yako unayoiacha na kuhamia kwa mkeo.
Unaweza kuanzisha biashara za familia wazazi wako wakawepo huko ikawa ni njia nyingine ya kuwaweka karibu.
 
Siku chache kabla kuoa nilienda kumsalimia jirani yangu Mama Hambiliki..Huyu mama alikuwa mshkaji wangu sana..Watt wake tumekua pamoja na tulikuwa marafiki sana..Kwa kipindi hicho watt wake wote walikuwa wameoa/olewa tayari(wanaume 2,wanawake 2)

Basi ktk maongezi akanambia naona mambo yameiva,soon wazazi wako wanakupoteza(huku anacheka).Nikamuuliza kivipi..Akanambia mtt wa kiume akishaoa anakuwa sio wako tena..Nikamwambia sio kweli,Nikamuuliza Mbona we unamaisha mazuri tu hapa..watt wako wanakupa back up ya kutosha wala hawajakutupa(coz kwa kipindi hicho alikuwa ameshastafu kazi..Akanambia nwei we nenda..Tusiandikie mate wakati matope yapo

Sikuchukulia maanani yale maneno mana mama Hambiliki ni mwingi wa utani..Nikajua ni ktk sehemu yake ya utani

Basi nikaingia ndani ya ndoa na kimwana wangu matata(special order kutoka mbinguni).. Ndoa ikanibeba msobemsobe huku ile kauli ya mwanaume ndo kichwa cha familia ikiwa imetamalaki kichwani kwangu..Kila show nilisimamia mm..Japo kimwana alikuwa na kazi nzuri lakini mshahara wake sikuwahi kuuona ukitumika..Sikuhoji na niliona sawa tu..
Mimi Home kwetu nilikuwa sionekani mpaka kuwe na matatizo serious..

Ilipita miaka kama miwili hivi nilikuwa sijakanyaga kijijini kwa wife..Na ilitokana na kwamba wazazi wake walikuwa wanakuja sana huku town kutusamilia..So sikuona umuhimu wa kwenda..Japo wife mara kwa mara alikuwa anaenda

Ikaja kutokea msiba kijijini kwao..Safari hii ilibidi nimsindikize wife..Ebwana mbadiliko niliyokutana nayo pale kwao yalinishangaza sana aisee..Sikuona umuhimu wa kuhoji mana nilijua ni dhahiri kuwa wife ndo kafanya yote hayo coz kwenye familia yao yy ndo alikuwa tegemezi...

Hapo ndo nilipoamua kujiongeza na mm..Nikaona ile kauli ya mwanaume ndo kichwa cha familia uenda sikuielewa vizuri..

Baada ya kupita muda kidogo siku nimeenda kusalimia home nikakutana na Mama Hambiliki..Katika stori za hapa na pale ndo nikakumbuka ile kauli yake..Ikabidi nimuulize hivi ulikuwa unamaanisha nn ulivyonambia vile..Akanambia mwanangu haya maisha unayoniona naenjoy ni matunda ya dada zako..Wao wananikumbuka karibu deile..Wale rafiki zako(watt wake wa kiume) kuonana nao mpaka kuwa na shida kubwa..unless inaweza kupita miaka sijawaona..Alinieleza mambo mengi sana

Safari hii nilimuelewa vizuri zaidi..Ndipo nilipoamua kuanza kuishi kwa akili na wife
 
Back
Top Bottom