GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,553
- 108,888
Taarifa nilizozipata kutoka katika Chanzo changu 'Nyeti' zinasema kwamba kilichogundulika juu ya Sakata zima la Mchezaji Bernard Morrison ni kwamba Klabu ya Yanga 'imedanganya' kuhusu 'Mkataba' wake na kwamba hata 'Sahihi' yake pia 'imefojiwa' kinyume na Sheria. Ukweli kamili wa hili upo njiani kutolewa kwa Watanzania ili 'Wahuni' na 'Matapeli' wa Soka la Tanzania wajulikane na waumbuke rasmi.
Chanzo changu hicho Kimeendelea kusema kwamba sehemu ambayo Yanga SC 'imejikoroga' ni katika Tarehe ya Mkataba wa Mchezaji Bernard Morrison ambapo Yanga SC 'wamedanganya' Umma kuwa 'alisajiliwa' tarehe 15 na Kuuwasilisha TFF wakati Mchezaji aliwasili nchini tarehe 17 na hata Mawasiliano yake ya Email yana Ukweli wote pamoja na Tiketi yake ya Ndege.
Hivyo basi 'Adhabu' ambayo huenda Yanga SC 'ikakumbana' nayo katika 'Hukumu' inayoenda 'Kutolewa' leo ni ama 'Kunyang'anywa' Alama ( Points ), Kupigwa Faini Kubwa, Kuzuiwa Kufanya Usajili, Kushushwa Daraja, Viongozi wake Kukamatwa, Kushtakiwa na Kufungiwa kabisa. Na kama TFF wakisema walipeleke hili 'Suala' huko FIFA kuna uwezekano Klabu ya Yanga 'ikafutwa' katika ramani.
Chanzo hicho kimemalizia kwa kunielezea kuwa kumbe baada ya Uongozi wa Yanga SC hasa kupitia 'Wadhamini' wao GSM kuona kwamba wanaenda 'Kuumbuka' walienda Kutoa 'Rushwa' ya Tsh Milioni 20 TFF ili hili 'Suala' lisiende mbali lakini Uongozi Imara na wenye 'Uweledi' wa TFF ukakataa huo 'Upuuzi' na kuwaambia Yanga SC hili 'Suala' lazima lifike mwisho ili liwe Fundisho nchini.
Baada ya Yanga SC na GSM kujua kuwa 'wameshalikoroga' na Mashabiki wao hawatawaelewa wameamua 'Kuwahadaa' kwa Kufanya 'Usajili' wa aliyekuwa CEO wa Simba SC Senzo Mbatha Mazingisa huku 'wakiwadanganya' kuwa 'wanamsajili' Mchezaji Clatous Chama na akina Deo Kanda. Hii yote Yanga SC wanafanya kama kutafuta 'Huruma' kwa Mashabiki na Wanachama Wao.
Namalizia kwa kusema 'sijakulazimisha' ukubaliane na nilichokiwasilisha hapa ila Yanga SC jana walifurahi lakini leo watalia sana na Moto utawaka.
Chanzo changu hicho Kimeendelea kusema kwamba sehemu ambayo Yanga SC 'imejikoroga' ni katika Tarehe ya Mkataba wa Mchezaji Bernard Morrison ambapo Yanga SC 'wamedanganya' Umma kuwa 'alisajiliwa' tarehe 15 na Kuuwasilisha TFF wakati Mchezaji aliwasili nchini tarehe 17 na hata Mawasiliano yake ya Email yana Ukweli wote pamoja na Tiketi yake ya Ndege.
Hivyo basi 'Adhabu' ambayo huenda Yanga SC 'ikakumbana' nayo katika 'Hukumu' inayoenda 'Kutolewa' leo ni ama 'Kunyang'anywa' Alama ( Points ), Kupigwa Faini Kubwa, Kuzuiwa Kufanya Usajili, Kushushwa Daraja, Viongozi wake Kukamatwa, Kushtakiwa na Kufungiwa kabisa. Na kama TFF wakisema walipeleke hili 'Suala' huko FIFA kuna uwezekano Klabu ya Yanga 'ikafutwa' katika ramani.
Chanzo hicho kimemalizia kwa kunielezea kuwa kumbe baada ya Uongozi wa Yanga SC hasa kupitia 'Wadhamini' wao GSM kuona kwamba wanaenda 'Kuumbuka' walienda Kutoa 'Rushwa' ya Tsh Milioni 20 TFF ili hili 'Suala' lisiende mbali lakini Uongozi Imara na wenye 'Uweledi' wa TFF ukakataa huo 'Upuuzi' na kuwaambia Yanga SC hili 'Suala' lazima lifike mwisho ili liwe Fundisho nchini.
Baada ya Yanga SC na GSM kujua kuwa 'wameshalikoroga' na Mashabiki wao hawatawaelewa wameamua 'Kuwahadaa' kwa Kufanya 'Usajili' wa aliyekuwa CEO wa Simba SC Senzo Mbatha Mazingisa huku 'wakiwadanganya' kuwa 'wanamsajili' Mchezaji Clatous Chama na akina Deo Kanda. Hii yote Yanga SC wanafanya kama kutafuta 'Huruma' kwa Mashabiki na Wanachama Wao.
Namalizia kwa kusema 'sijakulazimisha' ukubaliane na nilichokiwasilisha hapa ila Yanga SC jana walifurahi lakini leo watalia sana na Moto utawaka.