Yeah. Huwa sijidanganyi ktk data.Ila inaniuma watz wengi.Hata wanaojiita consultants wanafanya maigizo na kukopi vitu au kufuata mkumbo tuu. Ndio maana hii thread leo naiibua wenye macho waone. Bahati mbaya niliwapa wasomi wa UDSM challenge. Wote waliangukia ktk ushabiki km yale magazeti ya sport na kudanganya watu.Ulitabiri,imekuwa!
mainstream media zilihadaa ulimwengu...wenye nchi wameamua...Republicans nao wamepata excuse kwamba wamemshindwa Trump. Drama bado mtashangaa atakuwa rais halafu mdanganywe na kura kwamba ni rais sijui asiyependwa.
Kwa vile uongo w amainstream media uliwapendeza waongo wa UDSM na agenda zao zilizofichwa wakaupokea hata baada ya mimi kuiweka hii thread hapa bado hawakuweza jinasua ktk upuuzi wao. Wakaamua fanya fani zao km maigizo ya chaguzi za bongo, au magazeti ya sports bongo, au udaku mwingine. Its a sin km hawa jamaa hawakujiongeza na kuwa wakweli ili wachambue kwa weledi na manufaa ya taifa. Wakajidanganya km vile wamarekani wanawasikiliza ujinga wao waliozoea kuwadanganya watz.mainstream media zilihadaa ulimwengu...wenye nchi wameamua...
Kwa vile tunapenda kuvuna na si kupanda. subiri siku ccm inatolewa utaona wengine waakavyotaka hamia airtel na kutaka ukubwa kwamba niw apigania uhuru. Ukiwa na macho na si mtu w akujidanganya, kuwa watu na tamaduni zao ktk issue za kuendesha nchi utaona mengi. Porojo na kujipigia debe kimaigizo,na kushutumu wengine ila wakishika hakuna kitu kinakwenda, zaidi ya mzigo kwa waliotengwa,kulipishwa kodi ili wavivu na waharibu uchumi wazidi kujaza matumbo na kuchafua kila kitu.Hongera sana mleta uzi. Nilimpenda Trump pindi tu niliposikia mpango wake ni kuishikisha adabu bara jeusi kwa uzembe wao na utawala mbovu...nilimpenda tu kwakuwa alihaidi kuwanyoosha ving'ang'anizi wa madaraka. Walivyowabovu ni kashangaa zaidi ndo wa kwanza ku-tweet. Hivi kwa nini mlitaka amerika isiwe ya waamerika ila iwe yenu na siyo yao kama tanzania ilivyo ya kwetu?
Mkuu you are right! Na naamini kuchaguliwa kwa Trump kutapeleka mwangwi sehemu nyingine hasa Ulaya!Miaka zaidi ya kumi nyuma tulishughudia kipindi cha populists wakichaguliwa kwa fujo duniani.. Hawa jamaa walichaguliwa bila hata kupimwa.Na aliyehoji uwezo wao alipata shutuma na upinzani mkubwa sana toka ktk umma. Ndio kipindi tuliwapata akina JK, Obama, na DJ kule Madagascar, David Cameron kule Uingereza etc. Ufanisi wao wao tuliuona.
Sasa wamekuja radicals ambao walizomewa km watu wenye chuki wachonganishi etc. Ila dunia inachoka unafiki km bahari inavyochoka mizoga. Radicals km Donald Trump, Diurtete kule Philippines, na wengine wengi sasa ndio wanakwenda shika dunia. Pengine dunia itaupa unafiki break kidogo ili mambo yaende kiuhalisia kidogo. Kwa Africa ni kipindi cha Neema, rais mwenye kusema na kutenda kweli inayouma kwa viongozi wetu atasukuma issue mbele kidogo.
Kwa wale walilelewa kwa philosophia za UDSM kaene mkao wa kula. Mtaambiwa mabaya mengi sana na hawa wachambuzi, kwa vile siku zao za kudanganya watu kabla ili kulinda watawala, ila siku zao zinahesabika sana.
Propaganda za kijamaa hazina tena nafasi ktk dunia huru.
Waandishi wapuuzi na wenye hila au uwezo mdogo nafasi yao inaondolewa ktk jamii. Media za magahribi na kasuku wao Africa walishambulia na kuuliza maswali yasio ya haki .Km wanavyofanya kwa wapinzani ktk hizi nchi zetu wakidhani wanaokoa roho za fikra maarufu, fikra za mkumbo, dunia nzima fikra za pamoja,fikra maarufu zimethibitika kwamba ni upuuzi na ujinga.
Hata ktk mabunge yetu, ktk jamii zetu, fikra mgando,fikra za pamoja na kulindana hazina tena mashiko. Sasa wajenga hoja,wenye kujiamini wanapiga bao.Watasema na kuoingwa kushambuliwa, ila kadiri wanashambuliwa ndivyo ukweli wa matukio unavyozidi jidhihirisha. Mwishowe inakuwa ngumu sana kwa wanafiki na wafuata mkumbo kukataa hoja
Ushapata whisk mkuu.Post nzuri sana kk, kiukweli dunia sasa tumechoka unafiki, sasa radicals wanahitajika kuliko msimu wowote, me nasubiri Trump ashinde nipate wisk nzito munoo huku nikiwa na matumaini mapya kwamba sasa nyekundu inaenda kuitwa nyekundu na nyeusi ni nyeusi, tumechoka uchumi wetu uko chini ala tunaambiwa unaimarika. Ila kale kamama Hilary kakishinda ni muendelezo wa unafiki
Brexit ilishaanza. France na italia wapo mbioni. Wajerumani sasa hivi wanapikwa kwa kuruhusu wakimbizi waingie kwa wingi na tamaduni zao zinazochosha. Kisha akija mwanasiasa radical agombaniwe haswa na wazawa. Merkel sasa anahemea drip. Watu wa mataifa wana tabia zinachosa, wakiingia tuu tayari kila kitu kinadadilika. Nyumba soon zinaanza wekwa magrill, watu kulazimishwa vaa kwa namna wanazotaka hao wakimbizi km walivyoacha ktk ukiwa wao na kukimbilia neema. Hata wale raia wanaojifanya wanapenda wageni na wasamaria wema,wakionja joto ya jiwe fasta wanaanza lia waondolewe. Kumpa mamba msosi na kujidanganya siku nampa mkono atauacha inakula kwako tuu.Mkuu you are right! Na naamini kuchaguliwa kwa Trump kutapeleka mwangwi sehemu nyingine hasa Ulaya!
Huwezi penda hii kitu.Ndio maana nashupalia kwa vile ni multiple blow kwa wapuuzi wengi sana. wanaojificha nyuma ya vyeti na propaganda. Pole sana najua inauma ila nikusaidiaje?Unavyoshupalia thread yako utafikiri uumegundua mgodi wa almasi!