Baada ya kuwauliza Matajiri wakubwa kuhusiana na tuhuma za kutokuhudhuria nyumba za Ibada walinijibu kama ifuatavyo

Baada ya kuwauliza Matajiri wakubwa kuhusiana na tuhuma za kutokuhudhuria nyumba za Ibada walinijibu kama ifuatavyo

Pakome

JF-Expert Member
Joined
Dec 8, 2024
Posts
1,541
Reaction score
916
Mimi kwa muda mrefu nimekuwa nikifanya kazi za matajiri wengi sana ikafikia mahali Matajiri wale wakawa wananialika kwenye shuhuli zao

Sasa kawaida binadamu kuna wakati tunazungumza mambo mengi

Siku moja nikachomeka swala la Ibada

Nikawauliza kuwa kuna shutuma kuhusiana na matajiri kuwa hawaendi nyumba za Ibada nikama wavivu hivi

Wakanijibu kuwa wanapenda sana na wanatamani sana kuhudhuria nyumba za Ibada lakini tatizo ni moja tu

Wakadai kuwa tatizo hilo linatokana na mafundisho mengi kujaa umbea badala ya mafundisho yakusaidia binadamu kwa maisha haya halisi

Nikawauliza umbea upi huo? Wakanambia idadi kubwa ya viongozi wa dini hawana habari nyingine za kuelezea Waumini zaidi ya umbea wa Shetani wa mamilioni ya miaka iliyopita, umbea ambao ulishatupwa kwenye dampo na maisha mengine yakaendelea, kwamba alifanya haya akafanya yale mara akagombana na Malaika

Wakanambia habari hizo kwao ni umbea wa kijinga ambao ulishatupwa kwenye dampo mabilioni ya miaka iliyopita na wala Shetani haukumbuki tena ni sisi binadamu wajinga na tunaopenda umbea na chokochoko ndio tunahangaika na mambo ya kipuuzi ya kimbea mbea kama wajinga wasiokuwa na akili

Wakanambia wanachotaka kusikia viongozi wakifundisha watu ni namna ya kutafuta maisha na kutoa mbinu za kukabiliana na maisha haya halisi

Mfano wanataka viongozi wawafundishe mambo tunayoyaishi mfano Kilimo, kwamba mvua ya mwaka huu ni ya kiwango gani ili wapande mazao ambayo mwisho wake yatawapa chakula

Wakanambia wanataka kusikia viongozi wakifundisha maswala ya Uchumi kwamba ni biashara zipi watu wakifanya kwa hali ya sasa watapata faida nzuri

Wakanambia wanataka kusikia ni mifugo ipi yenye faida nzuri ili hata kama watafuga wapate fedha za kuendesha maisha yao na familia zao

Wakanambia wakifahamu nyumba ya Ibada inayotoa mafunzo ya maisha haya halisi tunayoishi basi watafurika kwasababu wanachotaka kufundishwa ni reality na sio kujazwa mafundisho ya kimbea mbea ambayo hayawezi kuwapa chakula wala ada za kulipa shuleni

Wakanambia habari za Shetani alifanya hivi mara akafanya vile kwao ni upumbavu na habari za kimbea mbea kwasababu haziwezi kuwasaidia wanachotaka nikusikia viongozi wanaowafunulia biashara nzuri za kufanya, mbinu za kuwekeza na mambo ya kubadilisha maisha yao

Wakanambia hizo habari hata huyo Shetani mwenyewe anaziona takataka kwasababu zilishatupwa mabilioni ya miaka iliyopita na kwanza alishasahau ni sisi binadamu wajinga tunahangaika nazo badala ya kuhangaika na mambo yatakayotusaidia kwenye maisha haya halisi kama kilimo, ufugaji, biashara, uwekezaji, na mambo kede kede

Wakanambia kama hakuna mafundisho hayo hawana muda wa kwenda kusikiliza takataka

Wakanambia kama ni kuhusu Mafundisho ya vitabu vya dini hawana tatizo nayo kwasababu yanaongelea mambo mazuri mfano upendo amani, huruma, msamaha lakini haya ya migogoro huwa hawapendi kwasababu hata kwenye vitabu vya dini hayajaandikwa sana
 
Kama waligusia kuhusu UMBEA basi umbea wenyewe ndiyo huu uliouleta hapa,eti wanataka mchungaji aongee kuhusu uchumi, na wachumi waongelee nini sasa? Kwani hawawajui maafisa kilimo wakaongee nao kuhusu kilimo? Watumishi wa Mungu wana mipaka yao,kama tu walivyo wahasibu nk, hao matajiri wako ni maskini wa elimu, au ni wale matajiri wa ndele!
 
Kama waligusia kuhusu UMBEA basi umbea wenyewe ndiyo huu uliouleta hapa,eti wanataka mchungaji aongee kuhusu uchumi, na wachumi waongelee nini sasa? Kwani hawawajui maafisa kilimo wakaongee nao kuhusu kilimo? Watumishi wa Mungu wana mipaka yao,kama tu walivyo wahasibu nk, hao matajiri wako ni maskini wa elimu, au ni wale matajiri wa ndele!
Walisema kwamba mafundisho yaliyoandikwa kwenye vitabu vya dini ni mazuri hata wao wanayakubali mfano amani, upendo, huruma, msamaha lakini wakadai viongozi wa dini wameongeza ya kwao waliotunga na hasa yamekaa kimgogoro mgogoro mara sijui vita sasa hawana muda na vita hizo
 
Kama waligusia kuhusu UMBEA basi umbea wenyewe ndiyo huu uliouleta hapa,eti wanataka mchungaji aongee kuhusu uchumi, na wachumi waongelee nini sasa? Kwani hawawajui maafisa kilimo wakaongee nao kuhusu kilimo? Watumishi wa Mungu wana mipaka yao,kama tu walivyo wahasibu nk, hao matajiri wako ni maskini wa elimu, au ni wale matajiri wa ndele!
Kwenye wahasibu ndiko wanakokimbilia ndo mana hawaonekani
 
Kwahyo kanisa imekuwa chuo cha kilimo au ujasirimali?KILA KITU IPO KWA MPANGO MAALUM.
Tulibishana sana kuhusiana na hili wakanambia basi hawataonekana, wakasema hata waendesha Ibada wameacha kufundisha mambo mazuri kama upendo, amani, msamaha wapo kimgogoro sana
 
Hao hawana nia tu ya kwenda nyumba za ibada..
Elimu za ujasiriamali wachungaji wakifundisha na wanaofundisha ujasiriamali wafanye kitu gani?

Viongozi wa dini wanapaswa kufundisha kuhusu maadili na tabia njema, masuala ya kifamilia, amani n.k yaani kama ni maadili wanafundisha uaminifu, tabia njema n.k masuala ya ndoa pia kuna upana wake ikiwemo malezi ya watoto n.k

Kuhusu kwenye utafutaji labda wanaweza kufundisha kuhusu nidhamu ya fedha mfano kuweka akiba n.k, pia kufundisha bidii katika kazi.. lakini kuto elimu za ujasiriamali hilo mnawaonea bure..

Hayo mafundisho yote wanakuwa wanarejea kutoka kwenye maandiko, naamini itapelekea kuwa na jamii imara kuanzia ngazi za familia... na viongozi wa dini wengi tu wanafundisha kuhusu hayo...
 
Hao hawana nia tu ya kwenda nyumba za ibada..
Elimu za ujasiriamali wachungaji wakifundisha na wanaofundisha ujasiriamali wafanye kitu gani?

Viongozi wa dini wanapaswa kufundisha kuhusu maadili na tabia njema, masuala ya kifamilia, amani n.k yaani kama ni maadili wanafundisha uaminifu, tabia njema n.k masuala ya ndoa pia kuna upana wake ikiwemo malezi ya watoto n.k

Kuhusu kwenye utafutaji labda wanaweza kufundisha kuhusu nidhamu ya fedha mfano kuweka akiba n.k, pia kufundisha bidii katika kazi.. lakini kuto elimu za ujasiriamali hilo mnawaonea bure..

Hayo mafundisho yote wanakuwa wanarejea kutoka kwenye maandiko, naamini itapelekea kuwa na jamii imara kuanzia ngazi za familia... na viongozi wa dini wengi tu wanafundisha kuhusu hayo...
Wanadai idadi kubwa wameacha kufundisha mafundisho mazuri kama haya uliyoyasemea
 
Back
Top Bottom