Baada ya kuoa, maisha yaliendeleaje mwanangu?

Ilikuwa inaniuma sana aisee kuna muda nilikuwa sirudi nyumbani nakula huko huko kazini ili tu asile jasho langu ,kumbe na wewe yalikukuta mshikaji wangu ?
Kwangu ilikuwa mshituko wa kuona bajeti imekuwa kubwa, lakini muda mfupi baadaye nilikubali tu kuwa maisha yamebadilika.Ilikuwa ni vita ya kimya kimya kichwani mwangu,wife hakuwahi kujua.Mimi sikuwahi kula peke yangu nje ya nyumbani
 
Inashangaza wanaume wengi wapo too much concerned with rising expenditure baada ya ndoa. Nadhani inawezekana hiyo ikawa ni sababu ya ndoa nyingi kuvunjika.

Mimi sikuwahi kuwaza kabisa kuhusu matumizi. Japo yaliongezeka sana kwasababu wife hakuwa na kazi. So, haikunisumbua akili kabisa. Goal yangu ilikuwa ni kumlisha chochote anachotaka yeye na mtoto.
 
Sio ajabu hata kidogo, na sababu kubwa ni yale mabadiliko ni ya ghafla japo tuliyajua kabla.
Gradually watu wanaelewa na kuyaishi majukumu yao.
 
Usijali huu uzi nitaufuta we nambie tu ulivyooa maisha yaliendeleaje? Huenda ukaniponya mwanangu, ilikuaje baada ya hapo, nasubiri comment yako!
Maisha yalikuja na Sura mbili, maisha magumu sana, kukosa hela Kabisa na msoto Makali wa muda mrefu, ila alivumilia sana na mimi.
Sasa Kama tunateremka kilima, maisha nafuu tunakula na kusasa
 
😁 kuswampa hili neno sijalisikia muda mrefu sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…