Baada ya kumzika Mama

Baada ya kumzika Mama

Ok9

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2013
Posts
4,556
Reaction score
4,169
Ndugu zangu wapendwa habari za muda mrefu tena.

Naomba kuambatanisha uzi


Ninajitahidi kuzoea hali ya kutokuwa na mama ila bado siamin kama ndo mazima. Inauma lkn hakuna namna.

Mama tulimzika na matanga tayri.

Kuna kauli nilizokutana nazo kwa kipindi hiki nazikumbuka sana naomba niweke hapa.

Dada mmoja ambaye yeye ni Yatima na amekuwa vizuri mikononi mwa ndugu wengine na sasa yupo JWTZ alinipigia simu na kuniambia: SHUKURU WEWE MZAZI AMEKUKUZA HADI HAPO ILA WENGINE WANAPOTEZA WAZAZI MAPEMA ZAIDI.

hii kauli iliniingia kichwani. Binamu yangu mmoja aliniambia.

Nimekuja msibani sio kwa ajili ya baba yenu(kwake ni mjomba) wala ninyi (sisi sasa) ila ni sababu za mama yenu (marehemu) the way alivyoishi na sisi....ana heshima kubwa. Kuna vitu alitengeneza ambavyo vina msaada mkubwa kwetu na sisi tuendeleze.

Pia SWALA MSIBA LISAHAU MAPEMA MAANA KUNA MAISHA BAADA YA MSIBA. Wa tatu ni broo mmoja ambye hata simjui.

Mama yako yupo sehemu salama zaidi ya hapa duniani hakuna haja ya kusikitika.

Hizi ni chache zinazo run kichwani muda wote ila ni nyingi sana ninazo kumbuka .

Nathamini kila mchango wa mwana JF kwan nimepitia kila comment na zimenifariji sana sana.
 
Pole sana mkuu! Huwa mtu huwezi kuamini tena kama mtakuja kuonana tena katika mazingira haya hasa ukizingatia jinsi mlivyozoeana.
 
Jipe muda.....

Baada ya muda utakuwa OK....

Kama unamwamini Mungu huu ndio wakati wa kusali sana. Polepole maumivu yatapona japo pengo la mama huwa halizibiki kamwe maana hakuna mtu mwingine hapa duniani ambaye atakupenda na kukuelewa kama mama.

Endeleza mema yote aliyokufundisha ili mama aendelee kuishi kupitia kwako. Wa kwangu ni miaka mitano sasa imepita lakini utafikiri ni jana tu hata simu yake bado ninayo nimeitunza japo namba yake ilishachukuliwa na watu wengine.

Mungu Akuongoze 🙏🏿🙏🏿🙏🏿
 
Pole mzee, mama hafananishwi na chochote, maumivu yake ni makubwa saana, ila utafanyaje na ndio kazi ya mola, sote tutakufa...

Kwa mujibu wa mafundisho ya dini yangu.
Pindi mtu anapokufa hukatika amali (matendo) yake yote isipokuwa mambo matatu;-
1. Swadaka inayoendelea mfano ulijenga kisima, nyumba ya ibada ama chochote kile ambacho kitaendelea kuwepo wakati we ushakwenda zako, hata mti wa matunda pia
2. Elimu yenye manufaa
3. Mtoto mwema anayemuombea dua

Hii 3 ndio sisi tuliopo duniani tuwafanyie saana wazazi waliotangulia mbele ya haki, aisee jitahidi saana kuwwa unamuombea dua mama mara kwa mara.

Pole saana mzee, najua unayopitia sababu hata mimi nilishapoteza mzazi wa kiume.
 
Ndugu zangu wapendwa habari za muda mrefu tena.
Naomba kuambatanisha uzi

Ninajitahidi kuzoea hali ya kutokuwa na mama ila bado siamin kama ndo mazima.... Inauma lkn hakuna namna.

Mama tulimzika na matanga tayri.



Kuna kauli nilizokutana nazo kwa kipindi hiki nazikumbuka sana naomba niweke hapa.



Dada mmoja ambaye yeye ni Yatima na amekuwa vizuri mikononi mwa ndugu wengine na sasa yupo JWTZ alinipigia simu na kuniambia: SHUKURU WEWE MZAZI AMEKUKUZA HADI HAPO ILA WENGINE WANAPOTEZA WAZAZI MAPEMA ZAIDI.

hii kauli iliniingia kichwani.



Binamu yangu mmoja aliniambia.

Nimekuja msibani sio kwa ajili ya baba yenu(kwake ni mjomba) wala ninyi (sisi sasa) ila ni sababu za mama yenu (marehemu) the way alivyoishi na sisi....ana heshima kubwa. Kuna vitu alitengeneza ambavyo vina msaada mkubwa kwetu na sisi tuendeleze.

Pia SWALA MSIBA LISAHAU MAPEMA MAANA KUNA MAISHA BAADA YA MSIBA.



Wa tatu ni broo mmoja ambye hata simjui.

Mama yako yupo sehemu salama zaidi ya hapa duniani hakuna haja ya kusikitika.



Hizi ni chache zinazo run kichwani muda wote ila ni nyingi sana ninazo kumbuka .

Nathamini kila mchango wa mwana JF kwan nimepitia kila comment na zimenifariji sana sana.

Somehow it’s a decision to move forward, so do not entertain hizo hisia, zinaweza kukufanya uache kufanya kila kitu, she is gone, she is in a better place! Move forward forward now
 
Somehow it’s a decision to move forward, so do not entertain hizo hisia, zinaweza kukufanya uache kufanya kila kitu, she is gone, she is in a better place! Move forward forward now
Sure
 
Nilipompoteza baba yangu niliteseka kwa miaka takriban 6 mfululizo,, mara nimuote mara niwe km namuona,, maruwe yalikuwa mengi mno,, kuna mtu nikamsimulia akanipa majani nitafune tangu wakati huo nikawa sawa tu,
 
Nilipompoteza baba yangu niliteseka kwa miaka takriban 6 mfululizo,, mara nimuote mara niwe km namuona,, maruwe yalikuwa mengi mno,, kuna mtu nikamsimulia akanipa majani nitafune tangu wakati huo nikawa sawa tu,
Duu
 
Back
Top Bottom