Baada ya kumdhibiti Makonda, nisisikie mtu akilalamika juu ya madawa ya kulevya!

Baada ya kumdhibiti Makonda, nisisikie mtu akilalamika juu ya madawa ya kulevya!

Kweli kabisa wakifanikiwa kumdhibiti Makonda tusisikie kelele oooh madawa oooh unga..
Walipokuwa wanataka mapapa walikuwa wanafikiri mapapa hawapo nchini?

au walifikiri hao mapapa sio popular figures??

Go makonda, Go
 
Kweli nimeanza kuamini kuwa adui wa maendeleo ya Africa ni mwafrica mwenyewe.
Makonda alianzisha kampeni ya usafi lkn matokeo yake kila mtu alikuja na kisingizio,wengine walidai wanaenda kazini jumamosi,wengine wakadai ni siku yao ya kupumzika,wengine wakadai hawawezi kufanya usafi wakati mamlaka zipo na wao wanalipa kodi,leo hii zoezi limekufa na jiji bado chafu,wanarudi kumcheka Makonda kuwa kila alianzishalo linafeli.
Maendeleo tutayasikia tu na kubaki kusifia tu mataifa ya wenzetu sababu walishatoka huko kwenye ujinga kama huu.
 
Kipi bora kutaja watu bila ushahidi na kuishia kuwahoji na kuwaachia ama kuchukua list ya kitwanga na kuanza kukamata na kufungua kesi mahakamani???

Kwahiyo list ya kitwanga ndio ilikuwa na ushahidi wa kujitosheleza wa kuwafungulia kesi,nao si walikuwa watuhumiwa tu kama hawa?
 
waTZ wanafiki sana!!! eti kuwakamata drug dealers no kutafuta sifa!!! subiri mwanao awe teja ndo utakuja jua umuhimu wa hii vita.
 
Hii nchi ni aibu mpaka basi! Chombo cha kutunga sheria kinasimama kidete dhidi ya MTU aliyeamua kusimamia sheria ili kulinda usalama wa watanzania!
Kuna MTU anaitwa kwa jina LA kabila Fulani hana kabisa mshipa wa aibu!
Inatia hasira kuona chombo na watu waliopaswa kuunga mkono vita dhidi ya biashara haramu ya madawa ya kulevya wanakuwa mstari wa mbele kumvunja moyo na kumtisha aliyejitoa mhanga kuwa mstari wa mbele kwenye vita hii! Washindwe na walegee!
Musu-****
 
Sitetei utajiri wa Makonda, lakini huyo MTU anayeitwa kwa kabila Fulani mbona yeye hahoji ukwasi wa kutisha alionao? Hivi ni yeye ndiye pekee mwenye hati miliki ya kuwa tajiri nchi hii?
Haya mambo ya kusubiri watu Fulani wametuhumiwa kiasi cha kuguswa maslahi yao binafsi ndio na wao waanze kutuhumu, tuhuma zao zinakuwa na sifa ya majungu? Kama walikuwa na sababu ya kutilia mashaka Mali za MTU Fulani wala tusingewalaumu kama wangemfikisha kwenye vyombo husika vya dola viweze kumchunguza!
Musu-****
 
Acha kukosa uzalendo unahisi watumia Madawa ni masikini tu?hebu tulia serikali ifanye kazi ake being suspected it doesn't mean you under guilty ...let the count of law choose who is guilty who is not
 
Vita ya madawa vita ya siasa? Wa kolomije huyo ana uwezo wa kupambana na madawa au kiki tu kwani dsm ni nchi mapambano yawe hapo tu... hii vita marekani na mataifa makubwa inawasumbua wenye mabajeti ya matirioni ije iwe mtu tu from zero.. kumbukeni soko lake nila kidunia ukitikisa bongo umetikisa dunia pia hii biashara mapapa wengi ni mamafia so mie nadhan mako anamsumbua tu siro... ni lini mapambano yawepo nchemba yupo kimya hebu tuache maigizo na kiki za kijinga.... nadhani kama ni kudandia treni kwa mbele basi huyu kadandia la umeme lile la japani.... So mie naona mbele nikuja kulipa watu sijui io pesa itatoka wapi amuulize meng na ukwasi wake jamaa alimtoa jasho mpk leo kimya akiitwa mdaharo atokei sasa kama ni backup ya akina GSM na ridh ndogo sana.... hii biashara ukishake tz umeshake masalia ya akina escobar na el chapo
Hakuna vita ya madawa ya kulevya hawa majamaa wanalao jambo
 
Acheni utoto kumtangaza mtu kwenye media ndio kupambana? Akipatikana hausiki inakuaje? Jaribuni kufikiri kwa usahihi.
Ujinga mtupu halafu dar tu
Huh ni ujinga tupu...... Nahisi kuna jambo nyuma ya huh mchezo ni mazingira yanatengenezwa I swear
 
"...ni kufikiri hovyo kudhani kuwa jukumu la vita dhidi ya udhibiti madawa ya kulevya Tanzania limeanzishwa na kuishia kwa Makonda,kuna vitengo na watu wanalipwa mishahara kufanya kazi hiyo. Hao wamewezeshwa kwa rasilimali watu, vifaa na nguvu za kisheria. .."

Anonymous
 
"...ni kufikiri hovyo kudhani kuwa jukumu la vita dhidi ya udhibiti madawa ya kulevya Tanzania limeanzishwa na kuishia kwa Makonda,kuna vitengo na watu wanalipwa mishahara kufanya kazi hiyo. Hao wamewezeshwa kwa rasilimali watu, vifaa na nguvu za kisheria. .."

Anonymous
Kiko wapi hicho kitengo? Kinaitwaje? Kimeshafanya nini toka kianzishwe?
 
Nawaonea huruma zaidi vyama vya upinzani. Wanatetea ufisadi na sasa wanatetea madawa ya kulevya. Sipati picha kwenye kampeni wataongea nini!
 
Inaonekana kuna watu wamejipanga kisawasawa kumdhibiti Makonda kwenye hii vita ya madawa.

Sikutegemea kuona baadhi ya Watanzania kumkashifu Makonda kwamba anatafuta sifa! Sifa jwa ajili ya nini? Sikutegemea kuona baadhi ya wabunge kusimama na kuanza kumpinga Makonda.

Sasa kinachofuata, Makonda ataachana na hii operesheni na hapo madawa yatakuwa yameruhusiwa rasmi hapa nchini.

Na kwakuwa tumeshindwa kumasapoti Makonda kwa sababu ya mahaba yetu ya kisiasa, nisisikie mtu akilalamika kuhusu madawa ya kulevya tena.
Sidhani kama watu wanakinzana na upigaji vita wa hili janga, isipokuwa utaratibu ambao Mh. Makonda anautumia si sahihi. Tuna kikosi cha kuzuia madawa ya kulevya, tuna jeshi la polisi ambalo lina maofisa waliosomeshwa na kodi zetu, wangekaa na Bw. Makonda na wangefanya kazi hii kiustaarabu kabisa. Fahamu kuwa hawa ni watuhumiwa tu unawaanika hadharani, ni rahisi sana kumchafua mtu lakini ikithibitika hawa watuhumiwa hawana hatia inakuwa tayari wameshachafuliwa na inachukua muda sana kwa ghalama kubwa kurudisha imani kwa wadau wao. Tunafurahi Bw. Makonda kujikitika katika kupambana na biashara hii haramu ya madawa ya kulevya lakini si kwa utaratibu huu anaotumia!
 
Back
Top Bottom