Baada ya kuhitimu chuo uliendeshaje maisha?

Baada ya kuhitimu chuo uliendeshaje maisha?

Dah! Nimekumbuka those days, nilipomaliza chuo nilijichanganya mtaani nikaanza kuosha magari oil com Moro aisee acha tu nashukuru nilikomaa kifikra sana mpk sasahv japo nna ajira ila najichanganya sana na shughuli nyingine hasa kilimo. All the best mkuu
 
Tafuta sehemu ujitolee hata bure ndugu yangu...!! Then kwaajili ya uzoefu utaweza tengeneza connection nyingi Sana'a!! Zitakupa uwezo mzuri na ujenzi mzuri wa mawazo yakinifu
Ni kweli mkuu.
 
Nahusika ktk kufundisha viziwi, vipofu, kwa ujumla kusaidia pamoja na kufundisha wanadamu wenye mahitaji Maalumu ktk jamii, pia kuelimisha jamii kuhusu watu wenye mahitaji maalumu ili kuondoa unyanyapaa ktk jamii yetu mkuu.
Nimekupata mkuu
 

Niliingia ndani ya maisha,nikafunga mkanda vizuri,nikawasha maisha na kuanza kuyaendesha vizuri tu.
 
Dah! Nimekumbuka those days, nilipomaliza chuo nilijichanganya mtaani nikaanza kuosha magari oil com Moro aisee acha tu nashukuru nilikomaa kifikra sana mpk sasahv japo nna ajira ila najichanganya sana na shughuli nyingine hasa kilimo. All the best mkuu
Hongera sana mkuu
 
Tafuta kazi ujishikize usiangalie umesomea nini hata kuuza nguo fanya tu kama hauna kabisa mtaji tafuta hata kazi ya saidia fundi ukijibweteka nyumbani ni hasara
Alafu hii kitu kujishikiza sitaki kusikia neno hili......limtu linakuomba kazi eti naomba pa kujishikiza. Yaani kwenye Nazi zangu ndo ujishikize!!! Ina maana unakuwa hauko serious hivo siyo rahisi kujituma na kua na bidii kazini coz unakua umejishikiza
 
Tafuta kazi ujishikize usiangalie umesomea nini hata kuuza nguo fanya tu kama hauna kabisa mtaji tafuta hata kazi ya saidia fundi ukijibweteka nyumbani ni hasara
duh saidia fundi ni mziki ila ni kukomaa tu
 
Mm nimeshawahi kuwa mpaka konda mbn nilikuwa fresh tu naingiza chapaa
Mh nope acha uongo cis bt its okay kufanya lakini so kazi tu sometimes tuangaalie na ubunifu pia
Kuna kaZi unaeZa Fanya ikakupa stress za maisha tu
 
Hakuna kitu ambacho sikielewi kama unakuta mtu amekaa chuoni miaka 3 au zaidi kapata hicho alichopata let's say ni u-injinia au udaktari au ualimu halafu anakuja mtaani anauza supu au nguo,
Sisemi kua ni vibaya kufanya hivyo ila kinachonishangaza ni kwamba sasa kama dream ilikua ni hiyo kwanini kuhangaika kwenda kusomea kitu ambacho hakina relation na ulichosomea? Haumuoni huko ni kupoteza muda? Mana kama vision ilikua kuja kufanya biashara baada ya kuhitimu sasa si ungesoma business related courses basi (ambazo zingekusaidia unachokuja kutaka kufanya hapo baadae baada ya masomo)

Mi nachokiona wengi wetu tunaenda vyuoni tukiwa hatujui tumeenda kufanya nini. I mean mtu anafanya maamuzi ya kusomea kozi fulani ili hali hajui ataenda kuifanyia nini mtaani!.
Maisha yanafanya utoke nje ya fani uliyosoma. Co engineers wote wanaouza Nguo baada ya kumaliza chuo wanapenda kufnya Biashara hyo
 
Mleta mada, hongera sana kwa kuendea kilimo... Ila kwa uelewa wangu ni kwamba mtu yeyote ategemeae kilimo kuwa ndio biashara yake pasipokuwa na kazi nyingine imleteayo kipato ama kila siku au kila mwezi, mtu huyu atabaki kuwa masikini mpaka kufa kwake. (Kilimo ni biashara ya msimu). Binafsi baada ya kuhitimu chuo nilijiingiza mchanganyikoni mtaani kisha kuendesha bajaji, saizi nafanya ishu zangu tu freely
 
Nilivolunteer 1 year bure ila nilipata uzoefu mkubwa sana wa nilichosomea nikawa navifanyia kazi kuna siku napata pesa siku nyingine kapa nikaacha nikahamia pengine kuvolunteer nikavolunteer kama miezi tisa ndipo ikapatikana nafasi moja nanikawa peke yangu niliefanyiwa interview nikapata kazi hiyo nikapanga nyumba double self fasta coz hakuna kitu kilikua kinaniuma kama unakuta picha kwenye group imeandikwa kama ulitumia let say chupa flani za soda na bado unaishi nyumbani inabidi uhame daa nilikua najisikia vibaya sana au kwenye group wanaulizana vp mshahara ushatoka kwan hapo nilikua nasema lini itakuja kuwa ila kila mtu ana muda wake Mungu amempangia so tusiache kumuomba na kumshukuru kwa kile kidogo alichotujalia
 
Mungu hutenda kwa wakati wake..kikubwa usikate tamaa..nakumbuka nimemaliza coz ya afya 2015..2016 jiwe kapiga ban ajira mpka uhakiki wa watumishi uishe..nikaona isiwe tabu nikajichanganya kitaa nikawa nachukua karanga vijijini naleta mjini nakoboa kisha nauza..nililima dengu nazo zikaniweka mjini..nikapata kazi za tempo shirika fulani nikawa napiga maisha yakasonga..tempo ikazingua nikajitolea mahali flan..kwa kifupi nimegusa kwingi..ila nashuru mh baada ya kuruhusu mambo yakakaa sawa now napambana nakazi.

Never give up in life.
 
Back
Top Bottom