Baada ya kugundua kuwa niko JF amani imetoweka

Mume wangu ni mwanasiasa mwenye wadhifa wa juu ndani ya CCM.
Maisha yetu kwa ujumla ni ya amani na upendo, ukiachia mbali matatizo madogomadogo.
Usiku wa kuamkia jumamosi iliyopita. nilikuwa na sleepless night, hivyo nikawa busy na JF.
Mida ya saa usiku, mheshimiwa akataka kujua ni nani namuandikia ujumbe (nilikuwa nina reply comment). Akachukua simu na kukuta najibu michango ya JF.
Nilishanhgaa amehamaki, akaninyang'anya simu na kuanza kutukana matusi makubwa huku akinifananisha na nyoka, mara aniite. Shetani nk
Kuanzia siku hiyo hali nyumbani, haitikii salamu, amenuna, yaani amani na upendo vimetoweka.
Jamani, nifanyeje mwenzenu?
Naomba msaada wenu

Sasa huoni unazidi kuiweka ndoa yako matatizoni kwa kuja kuanika matatizo yenu ya ndani ya ndoa jf isitoshe akiona atajua ni wewe.. Tunza ndoa yako JF isije ikawa chanzo cha mtafaruku ndani ya ndoa yako.

Ushauri - achana na JF msikilize mumeo..
 
hivi wanaume wa namna hii mnawatoa wapi???????????????/

Wamejaaaaa teleeee kuliko hao unaowafikiria........borea sie na Asprin wetu hata tukichakachua yeye ndo kwanza anazidisha mapenzi maradufu:A S-heart-2::A S kiss::A S-rose::A S-rose::hug::mwaaah: yani ni kitareheee tu:violin: mtindo mmoja si eti cacico?
 
Last edited by a moderator:
Wamejaaaaa teleeee kuliko hao unaowafikiria........borea sie na Asprin wetu hata tukichakachua yeye ndo kwanza anazidisha mapenzi maradufu:A S-heart-2::A S kiss::A S-rose::A S-rose::hug::mwaaah: yani ni kitareheee tu:violin: mtindo mmoja si eti cacico?
Tena leo nawaruhusu mkacheat wote ili kesho mnijie na maujuzi mapya.... Waambie wenzio cacico na BADILI TABIA.

Ila mjue kabisa kesho naanza na zoezi la kuwakunja tayari kwa kutumia maujuzi nloyapata kwa Kongosho enzi zileee kabla hajanipiga kibuti. Kuwa na wake watatu raha bana!!

attachment.php
 
Last edited by a moderator:
Jaamani Wanaume "Kwanini mnafanya hivyo, yaani wake zenu wajifiche ili waingie JF",? Natamani nifungue darasa muwalete waume zenu niwapige shule ya umuhimu wa ninyi kuwa member wa JF, hawajui kuwa wanafaidika sana kwa ninyi kuwa humu? Ushauri; Tafuta ana tatizo gani mumeo kisha tafuta jibu la tatizo lake-print mpelekee mwambie jibu limetoka hapa JF, km hutamwona anakenua meno akishukuru! Ila yale mabishi litatukana lakini kimoyomoyo lita -appreciate. Haya, kila mmoja wenu aanze mtaona watatulia, ila muwe wavumilivu itachukua muda.
 
Tena leo nawaruhusu mkacheat wote ili kesho mnijie na maujuzi mapya.... Waambie wenzio cacico na BADILI TABIA.

Ila mjue kabisa kesho naanza na zoezi la kuwakunja tayari kwa kutumia maujuzi nloyapata kwa Kongosho enzi zileee kabla hajanipiga kibuti. Kuwa na wake watatu raha bana!!

attachment.php


Na wee unavyopenda kutukunja looh......una bahati umetukuta wote vi portable
 
Pole shosti,kubali au kata ulifanya kosa sababu ingekua wewe ungefikiriaje unamka usiku unamkuta yeye kashika cm busy na sio mida ya kazi? hapo shosti kidogo umechemka,afadhali angekukuta unasoma kitabu angeelewa na usisahau hao watu 24/7 wanaota wanaibiwa wanaogopa mpaka vivuli vyao,sasa basi msubiri ameshapumzika kutoka kazini mwambie unataka kuongea nae na jaribu kumuelewesha na muapie mungu kwa kutumia kitabu cha dini yako takatifu na mwenyezi mungu atakusaidia atakuelewa.....
 
Kwa kweli sina tabia wala mazoea ya kuamka usiku na kuingia JF, imetokea mara moja tu.
Mume wangu anasema JF ni ya wazushgi na inasababisha CCM ichukiwe na kudharauliwa, hivyo basi, mimi sikupaswa kuwa memba wa mtandao unao muharibia maisha mume wangu
Pole sana. Nakubaliana na mawazo ya Bishanga. Ni vema pia tutazame upande wa pili; inawezekana umekuwa unamkera kwa tabia yako ya kuamka usiku na kuwa bize na JF. Unajua tena JF ilivyo, sometime utacheka peke yako, mara utaguna, hii yote inaweza kuwa kero kwa mumeo. Hakuna mume atakayefurahi kuona mkewe anaamka usiku na kuwa bize na sim/comp.

Muombe samahani. Acha tabia ya kushughulika na SHUGHULI NYINGINE YOYOTE USIKU na kumuacha mumeo amelala. Si vibaya ukamuelimisha kuhusu JF.
 
Na wee unavyopenda kutukunja looh......una bahati umetukuta wote vi portable
Nisipowakunja mtakuwa mabonge. Tena cacico itabidi nimbadilishie zoezi, naona anazidi kujinenepea.
 
Last edited by a moderator:
Dah! pole sana ma dearest. ila ukweli ni kwamba sijui kwanini waume zetu huwa hawapend wake zao tuwe memba huku jf ama sijui it was meant for men only sipatagi jibu.

wenzio sisi huwa tunajifichaga akiwa mezani wewe unakwenda kwa b/rum ukiskia stepa zake tu unaficha unafungua yahoo. wengine tunafungaga laptop ghafla. anyway kwakua tayari tatizo limeshaingia fanya hivi tulia wala usimsemeshe chochote yaani omba msamaha mara moja amekubali sawa hajakubali sawa wewe carryon with your duties. jthd sana usionyeshe weak ness yako yaani timiza wajibu wako vyema ili asipate kosa endelevu. pia sali ukimsihi Mungu arejeshe amani hiyo.

mwisho kabisa hivi janmani sisi wanawake tutajikomboa nini? hivi kwanini ndoa zinakuwa kama gereza? wakak na wababa wa jf kwanini hampendi wake zenu kuwa memba wa jf?

na fikiria kwanini wanaume wengi Wanakasirika akisikia dadake yuko na rafikiye wakat wadada akisikia uko na rafikiye atakutafutia na mwingine uwe unakula kokote
 
ah na nyie wanawake mlio olewa ya nini haya mambo ya jamii forums usiku...u start planting seeds of doubt kwa waume zenu. kuwa a sensible woman na achana na mambo ya kupofya jf usiku bana
 
Mume wangu ni mwanasiasa mwenye wadhifa wa juu ndani ya CCM.
Maisha yetu kwa ujumla ni ya amani na upendo, ukiachia mbali matatizo madogomadogo.
Usiku wa kuamkia jumamosi iliyopita. nilikuwa na sleepless night, hivyo nikawa busy na JF.
Mida ya saa usiku, mheshimiwa akataka kujua ni nani namuandikia ujumbe (nilikuwa nina reply comment). Akachukua simu na kukuta najibu michango ya JF.
Nilishanhgaa amehamaki, akaninyang'anya simu na kuanza kutukana matusi makubwa huku akinifananisha na nyoka, mara aniite. Shetani nk
Kuanzia siku hiyo hali nyumbani, haitikii salamu, amenuna, yaani amani na upendo vimetoweka.
Jamani, nifanyeje mwenzenu?
Naomba msaada wenu

Pole sana, jaribu kuwa mpole hasira zake zikishuka apologise but be firm kwamba wewe unaheshimu political affiliations zake nae ajitahidi kukubali na kuheshimu yako, do not be aggrresive and confrontational kwa sababu yeye kutokana na mfumo aliokulia na jinsi walivyo wao ndani ya CCM haWATAKI KUKUBALI KWAMBA NCHI HII LAZIMA ITABADILIKA, hawana tofauti na Gadafi, jitahidi umueleweshe taratibu atakuelewa, mwambie yeye sio focus ya involvement yako na JF bali mfumo ambao kwa bahati mbaya amejikuta akiutumikia na wewe unamuelewa.
 
Mume wangu ni mwanasiasa mwenye wadhifa wa juu ndani ya CCM.
Maisha yetu kwa ujumla ni ya amani na upendo, ukiachia mbali matatizo madogomadogo.
Usiku wa kuamkia jumamosi iliyopita. nilikuwa na sleepless night, hivyo nikawa busy na JF.
Mida ya saa usiku, mheshimiwa akataka kujua ni nani namuandikia ujumbe (nilikuwa nina reply comment). Akachukua simu na kukuta najibu michango ya JF.
Nilishanhgaa amehamaki, akaninyang'anya simu na kuanza kutukana matusi makubwa huku akinifananisha na nyoka, mara aniite. Shetani nk
Kuanzia siku hiyo hali nyumbani, haitikii salamu, amenuna, yaani amani na upendo vimetoweka.
Jamani, nifanyeje mwenzenu?
Naomba msaada wenu

Huu unaonekana kuwa ni uzushi! Kama kweli mbona unaficha-ficha kutaja jina? kama kweli akiiona hii si atajuwa ni wewe tu, kwanini usiweke wazi? Jibu ni dogo tu; huo wako ni uongo.
 
Huu unaonekana kuwa ni uzushi! Kama kweli mbona unaficha-ficha kutaja jina? kama kweli akiiona hii si atajuwa ni wewe tu, kwanini usiweke wazi? Jibu ni dogo tu; huo wako ni uongo.

Zomba ukiona sehemu imeandikwa CCM lazima uje. Nakupendaje basi lol
 
hee, smile kumbe yula jamaa ameshakuoa?maana nakumbuka uliomba ushauri hapa jf kuhusu kuogopa kutendwa tena na huyu wa sasa...many congratulations my dia!
polee mimi wa kwangu tulikutana humuhumu na jf ndo nyumbani kwetu...
 
Back
Top Bottom