Baada ya kuachana na matumizi ya pombe

Baada ya kuachana na matumizi ya pombe

Adimu:
Huu Ujumbe Print kisha mpelekee mkeo(Shemeji yetu)
Hallo Mrs:Adimu
Ninakupa pongezi sana na mungu akubariki kwa kuvumilia ndoa ya mumeo kwa kipindi kirefu katika hali ya Ulevi.
Mungu akubariki na atakupa njia ya mafanikio na ndoa yenye amani na furaha kati yako na mumeo.
Na pi mungu awajaalie awape kizazi chema chenye kujitambua.Nakushauri kama unawatoto jaribuni kuwa nao pamoja na karibu ili kufuta makosa ambayo Mumeo alikuwa akiyafanya mbele ya watoto ili watoto waweze kujua kwamba baba yao sio yule wa zamani na hii itawajenga kisaikolojia na kuwa na furaha nahat kuweza kufanya vizuri kwenye masomo yao.
Fanyeni sana ibada kumuomba mungu nakumshukuru kwa hili na awalinde na kizazi chenu,maana walevi wengi uzeeni inakuwa ni tatizo,na Pombe inafuata kizazi kama hakitajitambua.Kuna watu wanalewa Babu,bibi hadi wajukuu.Ikifika umri fulani hakuna hata mmoja mwenye kujitambua kimaisha.
Wapo wanaoenda na watoto wao Bar huku wakijua kabisa kwamba ni kutengeneza kizazi kiharibifu na laana mbele ya Mungu.
Ulevi ni chanzo kikuu cha maasi,ikiwemo Uzinifu,magonjwa ya Zinaa hasa Ukimwi ambao wengi walevi umewapeleka na wanao,maradhi ya Sukari,ini,figo nk.Kwa ufupi ulevi ni Laana.
Mungu awabariki katika ndo yenu na kizazi chenu(AMEEN),ibada muhim sana

Ni ujumbe mzuri sana huu hakika mwenzangu ataufuraia! Shukran
 
Ashukuliwe Mwenyezi kwa kutupa pumzi mpaka muda huu! Napenda niwashirikishe katika furaha na maisha mapya tangu nilipotoka kwenye Team gambe!
1: Nawai kuludi kwangu.
2: Pesa ninayoipata naitumia vizuri na kufanya vitu vyenye kuleta maendeleo.
3: Swala la hang over na kuzimua nimeshalisahau.
4: Ugomvi na mavulugu yote kwisha.
5: Maelewano na mama watoto yamekua kwa kiasi kikubwa.
6: Kuchoka choka nikiwa kazini kumekwisha.
na mengineyo meengi!
Wito wangu kwenu; Pombe ni adui wa maendeleo, ukitaka kuishi kwa mafanikio huna budi kuiacha.

Wewe ulikua mlevi siyo mnywaji wa pombe! Tofautisha hivyo vitu viwili.
 
Wapo wenye mafanikio ambao niwanywaji ila kama wasingekua wanywa pombe mafanikio yangekua zaidi yake!
mafaniikio ya mtu ni mipango yako mwenyewe lakini unaendekeza pombe na ukaacha kufuatilia vitu vya msingi utalost tuy, vivo hivyo kwa wasiokunywa kama hawana malengo maishani lazima watakufa maskinini. Ulevi uko mwingi ngd yangu sio pombe tu, hata wanaondekeza sana kusoma bila malengo hawatoki kimaisha. ILA MIMI SINYWI KABISA MKUU
 
Wewe ulikua mlevi siyo mnywaji wa pombe! Tofautisha hivyo vitu viwili.

Hii kauli yenyewe ya kilevi.
Maana walevi wote wnajiita wanywaji,hata kama unakunywa tone moja tu wewe ni mlevi.
Hii kauli wamekuwa nayo hata Wazinifu,mtu ukimuambia wewe mzinifu anakasirika na kukuambia mie sio mzinifu ila yule ni Mpenzi wangu wa siku nyingi na wala sina mwingine zaidi yake na tunaaminiana sana,je mmeoana,hapana

So,hizo kauli za kujifariji,kuimba na kulia zote ni kelele
 
A drunk does not have the capacity to plan
ofisini ninae kunywa pombe pekeyangu na nina maendeleo kuliko hao ambao hawanywi. Hadi wenyewe wanashangaa maendeleo ni mipango sio suala la kutokunywa pombe.
ingekuwa hivyo wale wazee wa uswahilini kariakoo wanaoshinda kwenye majamvi wangekuwa mabilionea
 
Pongezi mkuu kwa uamuzi wako mzuri. Hata mimi nilikuwa bingwa wa mambo hayo lakini niliacha zaidi ya miaka 15 uliyopita. Kila mtu alishangaa na waliniuliza nimepata wapi dawa ya kuacha kilaji!

Mimi naamini akuna cha dawa wala nini ni maamuzi tu!
 
Wewe ulikua mlevi siyo mnywaji wa pombe! Tofautisha hivyo vitu viwili.

Mlevi na mnywaji wote ni kitu kimoja, kwasasa unaweza kujicontrol ila kaa ukijua pombe itakutawala na utaangukia kwenye ulevi!
 
ofisini ninae kunywa pombe pekeyangu na nina maendeleo kuliko hao ambao hawanywi. Hadi wenyewe wanashangaa maendeleo ni mipango sio suala la kutokunywa pombe.
ingekuwa hivyo wale wazee wa uswahilini kariakoo wanaoshinda kwenye majamvi wangekuwa mabilionea

Hao wanaoshinda kwenye majamvi si walishashindwa maisha na wengine wanafaidi walichochuma maana ushasema wazee!
 
Hii kauli yenyewe ya kilevi.
Maana walevi wote wnajiita wanywaji,hata kama unakunywa tone moja tu wewe ni mlevi.
Hii kauli wamekuwa nayo hata Wazinifu,mtu ukimuambia wewe mzinifu anakasirika na kukuambia mie sio mzinifu ila yule ni Mpenzi wangu wa siku nyingi na wala sina mwingine zaidi yake na tunaaminiana sana,je mmeoana,hapana

So,hizo kauli za kujifariji,kuimba na kulia zote ni kelele

Zanzibar spices kuna siku unakuaga na pointi. Ni nini umekula leo ? HONGERA KWA KUTOKUNYWA POMBE
 
Uwa unapiga nini mkuu

Kila siku lazima nipate maji ya kunywa safi si chini ya lita 5 mkuu hiyo ndiyo siri na vitunguu swaumu natafuna sana

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Naisi huu mchepuko ulianzia kwa msukumo wa pombe

sasa naona unataka tuhame kwenye pombe tuhamie kwenye mchepuko hizi ni mada mbili tofauti jamani usichanganye mambo na utamu wake ni tofauti na madhara yake ni tofauti na uzuri wake ni tofauti jamnai ..... mweeee tukutane pale nikupe ofa ya kisichana (konyagi)
 
Ashukuliwe Mwenyezi kwa kutupa pumzi mpaka muda huu! Napenda niwashirikishe katika furaha na maisha mapya tangu nilipotoka kwenye Team gambe!
1: Nawai kuludi kwangu.
2: Pesa ninayoipata naitumia vizuri na kufanya vitu vyenye kuleta maendeleo.
3: Swala la hang over na kuzimua nimeshalisahau.
4: Ugomvi na mavulugu yote kwisha.
5: Maelewano na mama watoto yamekua kwa kiasi kikubwa.
6: Kuchoka choka nikiwa kazini kumekwisha.
na mengineyo meengi!
Wito wangu kwenu; Pombe ni adui wa maendeleo, ukitaka kuishi kwa mafanikio huna budi kuiacha.

Hapo namba 4, kumbe ulikuwa unajijua wakati wa kupigana na watu eeeee? Au zikishakuisha kichwani ndio unahadithiwa kuwa jana ulizikunja?
 
Back
Top Bottom