Baada ya kimya kingi nami nitie neno DP World, Mtazamo wangu ni Tofauti kidogo

britanicca

JF-Expert Member
May 20, 2015
15,636
30,004
Habari za siku nyingi, nimekuwa kimya kidogo tokea sakata la bandari limeanza.

Uwekezaji ni mzuri sana, hasa unapofuata misingi sahihi. Hasa kwa bandari zetu, hizi zinataka mapinduzi makubwa sana kutoa au kuondoa ukiritimba uliopo. Hivyo siwezi kupingana na aliyeleta hoja ya kuwakaribisha wawekezaji, japo naweza pingana naye kwa namna sakata linavyopelekwa au lilivyobebwa.

A. Kwanini naunga mkono hoja?

Bandari yetu imekuwa ni ya hovyo sana kwa miaka mingi mno. Kupotea kwa mali za wateja, kuchelewa kwa huduma, kutozwa tozo zisizo sahihi, kuharibu mali wakati wa utoaji. Kwenye suala la mwekezaji bandarini, isiishie kwenye kuleta mikono ya kupakua mizigo au kuweka tehama tu. Bali hata usimamizi wa mapato na mchakato mzima wa kumtoza mteja uwe wazi na makusanyo yaelekee sehemu husika.

B. Mapungufu katika mchakato mzima

Natambua fika kwamba wenye bandari, sisi ndio ilibidi tuande draft ya jinsi gani tunataka bandari iendeshwe, alafu tumpe anayekuja kuwekeza. Najua hilo litakuwa limefanyika, ila kama yamefanyika, basi zitakuwa zimepitiwa hatua hizi.

Mwenye bandari, sisi ndio ilibidi kuandaa proposal na tena kuna hatua:

1. Unaandaa hadidu za rejea, yaani terms of reference (TOR).
2. Unaandaa tangazo ili wazabuni waombe kufuatana na vigezo vyako kwenye Hadidu za rejea.
3. Unatangaza tenda ili watoa huduma waombe kufuatana na vigezo vya kwenye Hadidu za rejea.
4. Mnafungua tenda mbele ya wazabuni.
5. Mnachuja wazabuni kufuatana na vigezo.
6. Mkimpata anayewafaa, mnamfahamisha kupitia offer letter.
7. Anajibu offer letter.
8. Wewe mwenye zabuni, ambaye ndiye unahitaji huduma, unaandaa mkataba. Unawapa draft upande wa pili, nao wanaupitia. Wakikubaliana, mnasaini.

Nadhani huu utaratibu au unaofanana na huu ulifuatwa. Tunasubiri CAG akija kwenye ukaguzi, asije kusema trilioni kadhaa zilipotea kwa sababu ya kutofuata taratibu za mkataba.

C. Udini na ukanda

Ukiwasikiliza vijana wengi mtandaoni kwa sasa, hawajibu hoja bali hisia zimejengeka tayari ndani yetu au yao. Kwamba Wazanzibar wanauza Tanganyika, wakati huo huo Wazanzibar wanatetea hata kila lisilotetewa kisa watekelezaji wanatoka upande wao. Hapa ningeshauri kwanza vijana wazichambue hoja zote za msingi, tuweke ukanda na udini pembeni ili sasa tuongee points. Juzi kuna sheikh mmoja nimemuona anamparua Prof Issa Shivji, kama mtoto mdogo bila kujua mzee Shivji ni miongoni mwa wanazuoni 7 waliopewa direct approach Ikulu na kutoa maoni. Na katika maoni ambayo huwa yanazingatiwa sana ni ya Issa. Anatokea mtu anajiita Sheikh, bila kujibu hoja, anambagua kwa rangi yake. Hilo suala halikuwa sahihi kabisa. Masheikh na Maaskofu, umakini katika kuyaongelea masuala ya msingi kama haya, hasa nisifiche mme-pwaya.

D. CCM inatumia watu wa hovyo kufikisha ujumbe

Chama changu pendwa cha CCM, mmetumia watu wa hovyo sana kufikisha ujumbe au kuelimisha jamii. Nina mifano:

- Hili suala la uwekezaji au ubinafsishaji kwenye bandari, wapinzani wametupiga bao kwenye kutumia watu wajanja na wajuzi wa mambo kudadavua undani. Na ndio maana kila mwananchi wa kawaida anadhani au anajua bandari imeuzwa tayari, kwakuwa wamejadili masuala ya msingi. Na hata wasio wapinzani wamejadili mambo ya msingi haswa.

Mfano, Mama Anna Tibaijuka alieleza kwa kina juu ya usalama wa anga (airspace). Kwamba mkataba, kwa kipengele alichosoma, kuna sehemu inasema kwamba bandarini pale, sehemu kadhaa ft kadhaa kwenda juu, hatutakuwa na mamlaka nayo. Hili suala halijajibiwa zaidi ya kusema na kushambuliwa kwamba ESCROW ni ya Tibaijuka. Mara anamtetea Karamagi wa TCTS. Je, hoja yake imejibiwa?

Lissu yeye kazungumzia suala la watakapokuwa na bandari kavu, hatutaruhusu kujenga feeder roads. Kashambuliwa kwa matusi. Je, hoja hii imejibiwa?

Mkataba hauna ukomo, ni hoja ya kila mtu. Mbona nayo haijajibiwa?

Mgawanyo wa jinsi gani tutapata share haikuwekwa wazi. Basi inabidi CCM watumie wataalamu kueleza kwamba uwenda itasemwa hapo baadaye au kuna sababu kadhaa kadhaa kutosemwa.

Chakushangaza, watetezi wa CCM ni Steve Nyerere, ambaye hata wasanii wenzake hawamkubali popote, hata kwenye sekta ya usemeji walimkataa. Ndo CCM inampa airtime kusemea mambo mazito.

Mtu kama Manara, huyo ndo karibu kabisa kwa maelezo yake yamejaa na ubaguzi ndani yake, kwamba watu wa mikoani hawaruhusiwi kuhoji bandari. Are we serious?

CCM au Serikali ina watu wengi wa kuweza kueleza jambo likaeleweka. Wapo kama Mzee Adam Simbeye wa "This Week in Perspective" na wazee wa namna hiyo, wengi wasomi wanaoelewa masuala haya ya mikataba.

Linapokuja suala la mambo ya msingi ya nchi, tafadhali, akina Mwijaku, sijui Baba Levo, wakae kwenye miziki na media huko. Mambo ya msingi wataalamu wawaeleze wananchi kinaga ubaga, kuliko kuwatumia watu watakao watibua watu au kuwa misled na serikali ikaeleweka visivyo, kumbe si lengo la serikali waseme hivyo.

Ushauri wangu:

1. Kama tumekaa na TICTS miaka zaidi ya 20, aongezewe mwaka mmoja. Huku serikali na wadau waanze kuufanya mchakato upya kwa kutangaza magazeti ya serikali na kwenye televisheni ya Taifa. Kiwepo kipindi maalumu cha kuuelezea mkataba kwa Kiswahili tu na kidadavuliwe na wataalamu. Ifanyike hivyo kila wiki mara tatu kwa muda maalumu ndani ya wiki 52.

2. Mwekezaji naye aelezwe kwamba kuna ABCD tunataka wananchi waelezwe, ili kuzuia baadae asije kuwa raisi wa kariba ya wale wasiofuata sheria kama fulani, akaufutilia mbali.

Mwisho, Tanzania ni zaidi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Chama Cha Mapinduzi (CCM), Zanzibar, Tanganyika, ACT, Uislamu, Ukristo, au Upagani.
 
Habari za siku nyingi, nimekuwa kimya kidogo tokea sakata laBandari limeanza,

Uwekezaji ni mzuri sana na hasa unapofuata misingi sahihi, hasa kwa bandari zetu hizi zinataka mapinduzi makubwa sana kuto au kuondoa ukiritimba uliopo,

hivo siwezi kupingana na aliyeleta hoja ya kuwakaribisha wawekezaji, japo naweza pingana naye kwa namna sakata linavyopelekwa au lilivyobebwa,

A. KWANINI NAUNGA MKONO HOJA
Bandari yetu imekuwa ni ya hovyo sana kwa miaka mingi mno, kupotea kwa mali za wateja, kuchelewa kwa huduma, kutozwa tozo zisizo sahihi, kuharibu mali wakati wa utoaji,
kwenye suala la mwekezaji bandarini isiishie kwenye kuleta mikono ya kupakua mizigo au kuweka tehama tu, bali hata usimamizi wa mapato na mchakato mzima wa kumtoza mteja uwe wazi na makusanyo yaelekee sehemu husika,


B.MAPUNGUFU KATIKA MCHAKATO MZIMA
Natambua fika kwamba wenye bandari sisi ndo ilibidi tuande draft ya jinsi gani tunataka bandari iendeshwe alafu tumpe anayekuja kuwekeza, najua hilo litakuwa limefanyika ila kama yamefanyika basi zitakuwa zimepitiwa hatua hizi

Mwenye bandari sisi ndo ilibidi kuandaa proposal na tena kuna hatua.
1. Unaandaa hadidu za rejea yaani terms of reference (TOR).

2. Unaandaa tangazo ili wazabuni waombe kufuatana na vigezo vyako vya kwenye Hadidu za rejea yaani terms of reference (TOR)

3. Unatangaza tenda ili watoa huduma waombe kufuatana na vigezo vya kwenye Hadidu za rejea.

4. mnafungua tenda mbele ya wazabuni.

5. Mnachuja wazabuni kufuatana na vigezo.

6. Mkimpata anayewafaa mnamfahamisha kupitia offer letter.

7. Anajibu offer letter

8. Wewe mwenye zabuni ambaye ndiye unahitaji huduma unaandaa MKATABA. Unawapa draft Upande wa pili nao wanaupitia wakikubaliana mnasaini.

Nadhani huu utaratibu au unaofanana na huu ulifuatwa. Tunasubiri CAG akija kwenye ukaguzi asije kusema trillion kadhaa zilipotea kwa sababu ya kutofuata taratibu za MKATABA.

C.UDINI NA UKANDA
Ukiwasikiliza vijana wengi mtandaoni kwa sasa hawajibu hoja bali hisia zimejengeka tayari ndani yetu au yao kwamba wenda Wazanzibar wanauza Tanganyika, wakati huo huo Wazanzibar wanatetea hata kila lisilotetewa kisa watekelezaji wanatoka upande wao, hapa ningeshauri kwanza vijana wazichambue hoja zote za msingi, tuweke ukanda na udini pembeni ili sasa tuongee points, juzi kuna sheik mmoja nimemuona anamparua Prof Issa Shivji, kama mtoto mdogo bila kujua mzee shivji ni Miongoni mwa wanazuoni 7 waliopewa direct approach ikulu na kutoa maoni na katika maoni ambayo uwa yanazingatiwa sana ni ya Issa, anatokea mtu anajiita Sheik bila kujibu hoja anambagua kwa rangi yake, hilo suala halikuwa sahihi kabisa, Masheik na Ma Askofu Umakini katika kuyaongelea masuala ya msingi kama haya, hasa nisifiche MMEPWAYA

D. CCM INATUMIA WATU WA HOVYO KUFIKISHA UJUMBE
Chama changu pendwa cha CCM mmetumia watu wa hovyo sana kufikisha ujumbe au kuelimisha jamii nina mifano

--Hili suala la uwekezaji au ubinafsishaji kwenye bandari wapinzani wametupiga bao kwenye kutumia watu wajanja na wajuzi wa mambo kudadavua undani, na ndo maana kila mwananchi wa kawaida anadhani au anajua bandari imeuzwa tayari kwakuwa wamejadili masuala ya msingi, na hata wasio wapinzani wamejadili mambo ya msingi haswa
Mfano Mama Anna Tibaijuka alieleza kwa kina juu ya usalama wa anga (air space) kwamba mkataba kwa kipengele alichosoma kuna sehemu inasema kwamba bandarini pale sehemu kadhaa ft kadhaa kwenda juu hatutakuwa na mamlaka nayo, hili suala halijajibiwa zaidi ya kusema na kushambuliwa kwamba ESCROW ni ya Tibaijuka, mara anamtetea Karamagi wa TCTS, Je hoja yake imejibiwa?

lissu yeye kazungumzia suala la watakapokuwa na bandari kavu hatutaruhusuwa kujenga feeder roads, kashambuliwa kwa matusi je hii hoja imejibiwa?

mkataba hauna ukomo ni hoja ya kila mtu, mbona nayo haijibiwi?
Mgawanyo wa jinsi gani tutapata share haikuwekwa wazi, basi inabidi CCM watumie wataalamu kueleza kwamba uwenda itasemwa hapo baadae au kuna sababu kadha wa kadha kutosemwa,

Chakushangaza Watetezi wa CCM ni Steve Nyerere ambaye hata wasanii wenzake hawamkubali popote hata kwenye sekta ya usemeji walimkataa, ndo CCM inampa airtime kusemea mambo mazito,
Mtu kama Manara huyo ndo kaaribu kabisa kwa maelezo yake yamejaa na ubaguzi ndani yake kwamba watu wa mikoani hawaruhusiwi kuhoji bandari, are we serious?

CCM au Serikali ina watu wengi wa kuweza kueleza jambo likaeleweka Wapo kama Mzee Adam Simbeye wa this week in perspective na wazee wa namna hiyo wengi wasomi wanaoelewa masuala haya ya mikataba,

linapokuja suala la mambo ya Msingi ya Nchi Tafadhari akina Mwijaku sijui baba levo wakae kwenye miziki na media huko mambo ya msingi wataalamu wawaeleze wananchi kinaga ubaga, kuliko kuwatumia watu watakao watibua watu au kuwa mislead na serikali ikaeleweka visivyo kumbe si lengo la serikali waseme hivo,

USHAURI WANGU
1. Kama Tumekaa na TICTS miaka zaidi ya 20, aongezewe mwaka mmoja huku serikali na wadau waanze kuufanya mchakato upya kwa kutangaza magazet ya serikali na kwenye telvisheni ya Taifa kiwepo kipindi maalumu cha kuuelezea mkataba kwa kiswahili tu na kidadavuliwe na wataalamu, ifanyike hivyo kila week mara tatu kwa muda maalumu ndani ya week 52,

2. Mwekezaji naye aelezwe kwamba kuna ABCD tunataka wananchi waelezwe ili kuzuia baadae asije kuja raisi wa kariba ya wale wasifuata sheria kama fulan akaufutilia mbali ,

MWISHO TANZANIA NI ZAIDI YA CHADEMA,CCM,ZANZIBAR,TANGANYIKA,ACT,UISLAMU,UKRISTO AU UPAGANI,


Britanicca
Kama hatujui uendeshaji wa bandari wa kisasa tutaandika nini sisi tuliozoea umepitwa na wakati. Wao ndio waandike wataendeshaje.
 
Ngoja nikwambie... TOR zimeandaliwa na DP World, serikali hajaandaa TOR wala kutangaza publicly kutaka wazabuni wakuwekeza na kuendesha bandari. Ni Samia na watu wake walienda Uarabuni kwa interest zao, wakachagua DP World basi na kusaini vitu wanavyovitaka. Kwa hiyo, maswali yakitaalamu yakiulizwa, hawataki kujua na wanaishia kusingizia udini na Uzanzibar.

Lakini kinachosikitisha zaidi ni kwamba serikali unapeleka bungeni muswada wa kuhalalisha DP World isifuate sheria zilizopo za nchi juu ya uwekezaji wa raslimali za asili. Kwanini wanawapa exemption watu hawa?
 
 
Habari za siku nyingi, nimekuwa kimya kidogo tokea sakata laBandari limeanza,

Uwekezaji ni mzuri sana na hasa unapofuata misingi sahihi, hasa kwa bandari zetu hizi zinataka mapinduzi makubwa sana kuto au kuondoa ukiritimba uliopo,

hivo siwezi kupingana na aliyeleta hoja ya kuwakaribisha wawekezaji, japo naweza pingana naye kwa namna sakata linavyopelekwa au lilivyobebwa,

A. KWANINI NAUNGA MKONO HOJA
Bandari yetu imekuwa ni ya hovyo sana kwa miaka mingi mno, kupotea kwa mali za wateja, kuchelewa kwa huduma, kutozwa tozo zisizo sahihi, kuharibu mali wakati wa utoaji,
kwenye suala la mwekezaji bandarini isiishie kwenye kuleta mikono ya kupakua mizigo au kuweka tehama tu, bali hata usimamizi wa mapato na mchakato mzima wa kumtoza mteja uwe wazi na makusanyo yaelekee sehemu husika,


B.MAPUNGUFU KATIKA MCHAKATO MZIMA
Natambua fika kwamba wenye bandari sisi ndo ilibidi tuande draft ya jinsi gani tunataka bandari iendeshwe alafu tumpe anayekuja kuwekeza, najua hilo litakuwa limefanyika ila kama yamefanyika basi zitakuwa zimepitiwa hatua hizi

Mwenye bandari sisi ndo ilibidi kuandaa proposal na tena kuna hatua.
1. Unaandaa hadidu za rejea yaani terms of reference (TOR).

2. Unaandaa tangazo ili wazabuni waombe kufuatana na vigezo vyako vya kwenye Hadidu za rejea yaani terms of reference (TOR)

3. Unatangaza tenda ili watoa huduma waombe kufuatana na vigezo vya kwenye Hadidu za rejea.

4. mnafungua tenda mbele ya wazabuni.

5. Mnachuja wazabuni kufuatana na vigezo.

6. Mkimpata anayewafaa mnamfahamisha kupitia offer letter.

7. Anajibu offer letter

8. Wewe mwenye zabuni ambaye ndiye unahitaji huduma unaandaa MKATABA. Unawapa draft Upande wa pili nao wanaupitia wakikubaliana mnasaini.

Nadhani huu utaratibu au unaofanana na huu ulifuatwa. Tunasubiri CAG akija kwenye ukaguzi asije kusema trillion kadhaa zilipotea kwa sababu ya kutofuata taratibu za MKATABA.

C.UDINI NA UKANDA
Ukiwasikiliza vijana wengi mtandaoni kwa sasa hawajibu hoja bali hisia zimejengeka tayari ndani yetu au yao kwamba wenda Wazanzibar wanauza Tanganyika, wakati huo huo Wazanzibar wanatetea hata kila lisilotetewa kisa watekelezaji wanatoka upande wao, hapa ningeshauri kwanza vijana wazichambue hoja zote za msingi, tuweke ukanda na udini pembeni ili sasa tuongee points, juzi kuna sheik mmoja nimemuona anamparua Prof Issa Shivji, kama mtoto mdogo bila kujua mzee shivji ni Miongoni mwa wanazuoni 7 waliopewa direct approach ikulu na kutoa maoni na katika maoni ambayo uwa yanazingatiwa sana ni ya Issa, anatokea mtu anajiita Sheik bila kujibu hoja anambagua kwa rangi yake, hilo suala halikuwa sahihi kabisa, Masheik na Ma Askofu Umakini katika kuyaongelea masuala ya msingi kama haya, hasa nisifiche MMEPWAYA

D. CCM INATUMIA WATU WA HOVYO KUFIKISHA UJUMBE
Chama changu pendwa cha CCM mmetumia watu wa hovyo sana kufikisha ujumbe au kuelimisha jamii nina mifano

--Hili suala la uwekezaji au ubinafsishaji kwenye bandari wapinzani wametupiga bao kwenye kutumia watu wajanja na wajuzi wa mambo kudadavua undani, na ndo maana kila mwananchi wa kawaida anadhani au anajua bandari imeuzwa tayari kwakuwa wamejadili masuala ya msingi, na hata wasio wapinzani wamejadili mambo ya msingi haswa
Mfano Mama Anna Tibaijuka alieleza kwa kina juu ya usalama wa anga (air space) kwamba mkataba kwa kipengele alichosoma kuna sehemu inasema kwamba bandarini pale sehemu kadhaa ft kadhaa kwenda juu hatutakuwa na mamlaka nayo, hili suala halijajibiwa zaidi ya kusema na kushambuliwa kwamba ESCROW ni ya Tibaijuka, mara anamtetea Karamagi wa TCTS, Je hoja yake imejibiwa?

lissu yeye kazungumzia suala la watakapokuwa na bandari kavu hatutaruhusuwa kujenga feeder roads, kashambuliwa kwa matusi je hii hoja imejibiwa?

mkataba hauna ukomo ni hoja ya kila mtu, mbona nayo haijibiwi?
Mgawanyo wa jinsi gani tutapata share haikuwekwa wazi, basi inabidi CCM watumie wataalamu kueleza kwamba uwenda itasemwa hapo baadae au kuna sababu kadha wa kadha kutosemwa,

Chakushangaza Watetezi wa CCM ni Steve Nyerere ambaye hata wasanii wenzake hawamkubali popote hata kwenye sekta ya usemeji walimkataa, ndo CCM inampa airtime kusemea mambo mazito,
Mtu kama Manara huyo ndo kaaribu kabisa kwa maelezo yake yamejaa na ubaguzi ndani yake kwamba watu wa mikoani hawaruhusiwi kuhoji bandari, are we serious?

CCM au Serikali ina watu wengi wa kuweza kueleza jambo likaeleweka Wapo kama Mzee Adam Simbeye wa this week in perspective na wazee wa namna hiyo wengi wasomi wanaoelewa masuala haya ya mikataba,

linapokuja suala la mambo ya Msingi ya Nchi Tafadhari akina Mwijaku sijui baba levo wakae kwenye miziki na media huko mambo ya msingi wataalamu wawaeleze wananchi kinaga ubaga, kuliko kuwatumia watu watakao watibua watu au kuwa mislead na serikali ikaeleweka visivyo kumbe si lengo la serikali waseme hivo,

USHAURI WANGU
1. Kama Tumekaa na TICTS miaka zaidi ya 20, aongezewe mwaka mmoja huku serikali na wadau waanze kuufanya mchakato upya kwa kutangaza magazet ya serikali na kwenye telvisheni ya Taifa kiwepo kipindi maalumu cha kuuelezea mkataba kwa kiswahili tu na kidadavuliwe na wataalamu, ifanyike hivyo kila week mara tatu kwa muda maalumu ndani ya week 52,

2. Mwekezaji naye aelezwe kwamba kuna ABCD tunataka wananchi waelezwe ili kuzuia baadae asije kuja raisi wa kariba ya wale wasifuata sheria kama fulan akaufutilia mbali ,

MWISHO TANZANIA NI ZAIDI YA CHADEMA,CCM,ZANZIBAR,TANGANYIKA,ACT,UISLAMU,UKRISTO AU UPAGANI,


Britanicca

Asante sana mkuu....Tanzania ni kubwa kuliko sisi waja
 
Walau Britannica umekuwa very neutral, fair na mkweli. Thanks. Kwanza, serikali inatumia watu kama Mwijaku kwa sababu ili kuja kuelezea aina ya mkataba huu, lazima uung'oe ubongo kwenye fuvu. Ndo maana haina watu credible wa kuisemea. Jinsi suala lilivyoendeshwa, mizengwe ilivyojaa, rushwa ilivyo wazi na kadhalika, imepromote issues ulizozitaja kama udini, ukanda, chuki, na kadhalika.
 
Walau Britannica umekuwa very neutral .fair na mkweli. Thanks .Kwanza serikali inatumia watu aina ya Mwijaku kwa sababu ili kuja kuelezea aina ya huu mkataba lazima uung'oe ubongo kwenye fuvu. Ndo maana haina watu credible wa kuisemea. Jinsi suala lilivyoendeshwa, mizengwe ilivyojaa, rushwa ilivyo wazi nk imepromote issues ulizozitaja kama udini, ukanda , chuki nk.
Naam mkuu nimetafakari mengi si kwamba mimi upepo ulikuwa haunipitii kwamba mkuu sema hili sema lile nikajikita kwenye u busy alafu nikatafiti why nguvu ya kuupinga mkataba ni kubwa na why nguvu ya kushawishi tuukubali ni kubwa, nikaona kuna mambo neutral tutayasahau sasa
 
Umeongea kwa adabu na kuwatunzia heshima wahusika, sisi wengine tumeandika sana sana juu ya haya mambo, hatupingi uwekezaji sema je maslahi ya nchi yamezingatiwa kwenye mkataba? Na maswali yote yajibiwe inavotakiwa tutaenda pamoja
 
Habari za siku nyingi, nimekuwa kimya kidogo tokea sakata laBandari limeanza,

Uwekezaji ni mzuri sana na hasa unapofuata misingi sahihi, hasa kwa bandari zetu hizi zinataka mapinduzi makubwa sana kuto au kuondoa ukiritimba uliopo,

hivo siwezi kupingana na aliyeleta hoja ya kuwakaribisha wawekezaji, japo naweza pingana naye kwa namna sakata linavyopelekwa au lilivyobebwa,

A. KWANINI NAUNGA MKONO HOJA
Bandari yetu imekuwa ni ya hovyo sana kwa miaka mingi mno, kupotea kwa mali za wateja, kuchelewa kwa huduma, kutozwa tozo zisizo sahihi, kuharibu mali wakati wa utoaji,
kwenye suala la mwekezaji bandarini isiishie kwenye kuleta mikono ya kupakua mizigo au kuweka tehama tu, bali hata usimamizi wa mapato na mchakato mzima wa kumtoza mteja uwe wazi na makusanyo yaelekee sehemu husika,


B.MAPUNGUFU KATIKA MCHAKATO MZIMA
Natambua fika kwamba wenye bandari sisi ndo ilibidi tuande draft ya jinsi gani tunataka bandari iendeshwe alafu tumpe anayekuja kuwekeza, najua hilo litakuwa limefanyika ila kama yamefanyika basi zitakuwa zimepitiwa hatua hizi

Mwenye bandari sisi ndo ilibidi kuandaa proposal na tena kuna hatua.
1. Unaandaa hadidu za rejea yaani terms of reference (TOR).

2. Unaandaa tangazo ili wazabuni waombe kufuatana na vigezo vyako vya kwenye Hadidu za rejea yaani terms of reference (TOR)

3. Unatangaza tenda ili watoa huduma waombe kufuatana na vigezo vya kwenye Hadidu za rejea.

4. mnafungua tenda mbele ya wazabuni.

5. Mnachuja wazabuni kufuatana na vigezo.

6. Mkimpata anayewafaa mnamfahamisha kupitia offer letter.

7. Anajibu offer letter

8. Wewe mwenye zabuni ambaye ndiye unahitaji huduma unaandaa MKATABA. Unawapa draft Upande wa pili nao wanaupitia wakikubaliana mnasaini.

Nadhani huu utaratibu au unaofanana na huu ulifuatwa. Tunasubiri CAG akija kwenye ukaguzi asije kusema trillion kadhaa zilipotea kwa sababu ya kutofuata taratibu za MKATABA.

C.UDINI NA UKANDA
Ukiwasikiliza vijana wengi mtandaoni kwa sasa hawajibu hoja bali hisia zimejengeka tayari ndani yetu au yao kwamba wenda Wazanzibar wanauza Tanganyika, wakati huo huo Wazanzibar wanatetea hata kila lisilotetewa kisa watekelezaji wanatoka upande wao, hapa ningeshauri kwanza vijana wazichambue hoja zote za msingi, tuweke ukanda na udini pembeni ili sasa tuongee points, juzi kuna sheik mmoja nimemuona anamparua Prof Issa Shivji, kama mtoto mdogo bila kujua mzee shivji ni Miongoni mwa wanazuoni 7 waliopewa direct approach ikulu na kutoa maoni na katika maoni ambayo uwa yanazingatiwa sana ni ya Issa, anatokea mtu anajiita Sheik bila kujibu hoja anambagua kwa rangi yake, hilo suala halikuwa sahihi kabisa, Masheik na Ma Askofu Umakini katika kuyaongelea masuala ya msingi kama haya, hasa nisifiche MMEPWAYA

D. CCM INATUMIA WATU WA HOVYO KUFIKISHA UJUMBE
Chama changu pendwa cha CCM mmetumia watu wa hovyo sana kufikisha ujumbe au kuelimisha jamii nina mifano

--Hili suala la uwekezaji au ubinafsishaji kwenye bandari wapinzani wametupiga bao kwenye kutumia watu wajanja na wajuzi wa mambo kudadavua undani, na ndo maana kila mwananchi wa kawaida anadhani au anajua bandari imeuzwa tayari kwakuwa wamejadili masuala ya msingi, na hata wasio wapinzani wamejadili mambo ya msingi haswa
Mfano Mama Anna Tibaijuka alieleza kwa kina juu ya usalama wa anga (air space) kwamba mkataba kwa kipengele alichosoma kuna sehemu inasema kwamba bandarini pale sehemu kadhaa ft kadhaa kwenda juu hatutakuwa na mamlaka nayo, hili suala halijajibiwa zaidi ya kusema na kushambuliwa kwamba ESCROW ni ya Tibaijuka, mara anamtetea Karamagi wa TCTS, Je hoja yake imejibiwa?

lissu yeye kazungumzia suala la watakapokuwa na bandari kavu hatutaruhusuwa kujenga feeder roads, kashambuliwa kwa matusi je hii hoja imejibiwa?

mkataba hauna ukomo ni hoja ya kila mtu, mbona nayo haijibiwi?
Mgawanyo wa jinsi gani tutapata share haikuwekwa wazi, basi inabidi CCM watumie wataalamu kueleza kwamba uwenda itasemwa hapo baadae au kuna sababu kadha wa kadha kutosemwa,

Chakushangaza Watetezi wa CCM ni Steve Nyerere ambaye hata wasanii wenzake hawamkubali popote hata kwenye sekta ya usemeji walimkataa, ndo CCM inampa airtime kusemea mambo mazito,
Mtu kama Manara huyo ndo kaaribu kabisa kwa maelezo yake yamejaa na ubaguzi ndani yake kwamba watu wa mikoani hawaruhusiwi kuhoji bandari, are we serious?

CCM au Serikali ina watu wengi wa kuweza kueleza jambo likaeleweka Wapo kama Mzee Adam Simbeye wa this week in perspective na wazee wa namna hiyo wengi wasomi wanaoelewa masuala haya ya mikataba,

linapokuja suala la mambo ya Msingi ya Nchi Tafadhari akina Mwijaku sijui baba levo wakae kwenye miziki na media huko mambo ya msingi wataalamu wawaeleze wananchi kinaga ubaga, kuliko kuwatumia watu watakao watibua watu au kuwa mislead na serikali ikaeleweka visivyo kumbe si lengo la serikali waseme hivo,

USHAURI WANGU
1. Kama Tumekaa na TICTS miaka zaidi ya 20, aongezewe mwaka mmoja huku serikali na wadau waanze kuufanya mchakato upya kwa kutangaza magazet ya serikali na kwenye telvisheni ya Taifa kiwepo kipindi maalumu cha kuuelezea mkataba kwa kiswahili tu na kidadavuliwe na wataalamu, ifanyike hivyo kila week mara tatu kwa muda maalumu ndani ya week 52,

2. Mwekezaji naye aelezwe kwamba kuna ABCD tunataka wananchi waelezwe ili kuzuia baadae asije kuja raisi wa kariba ya wale wasifuata sheria kama fulan akaufutilia mbali ,

MWISHO TANZANIA NI ZAIDI YA CHADEMA,CCM,ZANZIBAR,TANGANYIKA,ACT,UISLAMU,UKRISTO AU UPAGANI,


Britanicca
Wasemapo mwisho huthibitisha mantiki 'the end justify the means' ndio kiipatacho serikali kwa kuleta watu wa hovyo kuthibitisha kuwa wenye weledi katika haya hawakuhusishwa tangu mwanzo.
 
Ngoja nikwambie... TOR zimeandaliwa na DP World, serikali hajaandaa TOR wala kutangaza publicly kutaka wazabuni wakuwekeza na kuendesha bandari. Ni Samia na watu wake walienda Uarabuni kwa interest zao, wakachagua DP World basi na kusaini vitu wanavyovitaka. Kwa hiyo, maswali yakitaalamu yakiulizwa, hawataki kujua na wanaishia kusingizia udini na Uzanzibar.

Lakini kinachosikitisha zaidi ni kwamba serikali unapeleka bungeni muswada wa kuhalalisha DP World isifuate sheria zilizopo za nchi juu ya uwekezaji wa raslimali za asili. Kwanini wanawapa exemption watu hawa?
Andika vizuri kwanza ndo nisome uandishi wako unatia uvivu wa kusoma au hujui kiswahili
 
Maada nzuri ila ulituambia kuwa " Kama Urusi itaivamia Ukraine basi una left jf" . Hujatekeleza.

Sasa nikukosoe kidogo kwa nia ya kujenga kujenga

1. Wanaopinga kuuzwa bandari sio wapinzani bali ni watanganyika wote kwa ujumla bila kujali itikadi wala dini zao. Rejea shekhe Ponda

2. Wanaounga mkono ni wazanzibar kwa kuwa mama ni wa kwao waziri na katibu wa wizara pia.

3. Watanganyika wanaounga mkono ni wanne tu waliohongwa ili tumbo zao zishibe. Nao form two dropouts Kitenge, Zembwela, Baba Levo na Manara.

Usitugawe watanganyika kwenye hili tumeungana hatutaki kuuzwa.

Tunahitaji uwekezaji wenye tija.

Mkataba ufutwe tutoe masharti sisi siyo wao.
 
Back
Top Bottom